SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na bei ya simu ya Redmi note 8 pro (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 18, 2022

Simu aina ya redmi note 8 pro ni simu ambayo imetoka mwaka 2019.

Ni simu ya 4G inayoweza kupokea toleo la Android 11 la mwaka 2021

Toleo android 11 linaifanya simu kuendana na nyakati za sasa

muonekano wa nyuma wa redmi note 8 pro

Ikizngatiwa sifa zake nyingi zinapatikana pia kwenye matoleo mapya ya simu za android

Bei ya redmi note 8 pro inapatikana chini ya laki tano kutegemeana na tolea lake

Bei ya Redmi Note 8 Pro Tanzania

Bei ya redmi note 8 pro ya GB 64 na RaM GB 8 inauzwa shilingi 390,000/=

Na redmi ya 128GB yenye ram 6GB inauzwa shilingi 425,000/=

Na toleo la mwisho la 128GB lenye ram ya GB 8 bei yake ni shilingi 450,000/=

Hizi ni bei za aliexpress bei za maduka ya Tanzania ni kubwa.

Sifa zake ziatupa uhalisia wa bei.

Sifa za Redmi note 8 pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G90T
  • Core Zenye nguvu(2) -2×2.05 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G76 MC4
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 9
  • MIUI 12.5
Memori UFS 2.1,128GB,64GB,256GB na RAM 8GB,6GB ,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.53inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 450,000/=

Upi ubora wa Simu ya Redmi note 8 pro?

Ubora wa redmi note 8 pro ni kamera yake yenye uwezo wa kurekodi kwa spidi kubwa

Simu ina bodi imara na ngumu kuvunjika

sifa za redmi note 8 pro

Inakubali kupokea tolea lingine la android

Bei yake ni rafiki na inavumulika kwa wenye bajeti ndogo

Utendaji wake ni wastani unaoweza kufungua applikesheni za aina nyingi

Japokuwa uwezo wake wa network umegawanyika

Uwezo wa Network

Network ya redmi note 8 pro ni ya 4G.

Simu ina masafa machache ya mtandao wenye kasi ya 4G

network ya redmi note 8 pro

Aina ya 4G inaweza kudownload spidi inayofikia 600Mbps kama kuna mtandao mzuri

Hii inachangiwa na LTE ya Cat 12

LTE yake inaweza kutumika kwenye mitandao yote ya simu nchini Tanzania

Ubora wa kioo cha Redmi note 8 pro

Kioo cha simu ya redmi note 8 pro ni aina ya ips lcd.

Vioo vya ips lcd vina rangi chache sababu ya contrast ndogo

Kitu kinachofaa bei ya kioo chake kuwa rahisi lakini ubora wa kuonyesha picha si mkubwa kama vioo vya amoled

Ila ubora wa kioo umeboreshwa na resolution kubwa ya pixels 1080 x 2340

Hivyo screen itaonyesha vitu kwa rangi zilizokorea kiasi

Nguvu ya processor Helio G90T

Processor aina ya helio G90T ina core nane.

Core kubwa zinaipa simu uwezo wa kucheza gemu ya Call of Duty: MobileĀ  kwa ubora wa 4K

Chip inapata alama za wastani kwenye app zinapima nguvu ya processor na gpu

Kwa mfano app ya antuntu inaipa alama 492 kwenye core moja.

Jua kuwa utendaji mzuri wa simu hupata alama angalau 500

Utendaji wa wastani unatokana na uwezo wa core kubwa kwenye spidi

Uwezo wa core kubwa

Core kubwa zipo mbili ambazo zinatumia muundo wa Cortex A76

Huu ni muundo umetumika kwenye processor aina ya Helio G95

Ila helio g95 ina nguvu zaidi, isipokuwa helio g90t ina spidi ya 2.05GHz

Uwezo wa core ndogo

Simu ina core ndogo sita zinazotumia muundo wa Cortex A55

Cortex A55 inaisadia simu kula chaji kidogo

Ni moja ya muundo unaofanya kazi ndogo kwa matumizi madogo ya betri

Uwezo wa betri na chaji

Ukubwa wa betri ya redmi note 8 pro ni 4500mAh

Uwezo wa betri kukaa na chaji ni masaa 114 ikiwa inatumika mara chache.

Na uimara wa ukaaji wa chaji ni masaa 15 simu ikiwa intaneti muda wote

Ila betri yake inapeleka umeme wa wastani wa wati 18.

Ni kiasi cha umeme kitakochojaza simu kwa masaa mengi yanayoweza fika matatu

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo matano ya hii simu kwenye ukubwa wa memori.

Ukubwa wa memori unaanzia GB 64 mpaka GB 256

Na ram zinaanzia GB 4 mpaka GB 8

Memori yake ina kasi kubwa ya kusafirisha data

Kasi kubwa hufanya simu kuwaka kwa haraka na app kufunguka kwa sekunde chache

Hii inasababishwa na aina ya memori ya UFS 2.1 kutumika.

Spidi ya kuandika na kusoma UFS 2.1 inafika 1200MBps

Uimara wa bodi ya Redmi note 8 pro

Upande wa nyuma simu ina kioo cha Gorilla Glass 5

Na pia Gorilla Glass 5 inalinda kioo cha redmi note 8 pro

Kuna majaribio yaliyofanywa na kampuni ya gorilla

Katika majaribio hayo, simu yenye kioo hiki haikuvunjika ilipondosha mara nyingi kwa kimo cha mita 1.2

Haihitaji screen protecto wala kava

Ubora wa kamera

Redmi note 8 pro ni simu ya macho manne

Kamera moja kubwa ya 48MP inatumia autofocus ya PDAF kwenye ulengaji.

kamera ya redmi note 8 pro

Dual pixel pdaf ina ulengaji wa ufanisi mkubwa kuliko PDAF

Kamera zake zinarekodi video za ubora wa aina tatu.

Kwani inarekodi video za full hd kwa spidi ya 30fps mpaka 120fps

Pia inaweza kurekodi video za 4K(Ultra HD) kwa spidi ya 30fps

Na video za HD kwa spidi inayofika 960fps

Na kitu kizuri simu inaweza kuondoa mitikisiko(yaani stabilization) wakati wa kurekodi video

Sababu kamera zinatumia Gyro-EIS

Ubora wa Software

Ukiimiliki simu kwa sasa utakuta Android 9 yenye MIUI 12.5

Lakini simu inakubali kupokea android 11.

Toleo la android 11 limeboreshwa applikesheni zake na mifumo yake.

Kwa mfano, utohaji wa ruhusa za app zinachukua data za simu ni tofauti na Android 9

Pia mfumo endeshi wa android 11 umewekewa app ya kurekodi screen.

Hivyo simu inakupunguzia muda wa kutafuta app ya namna hiyo

Yapi Madhaifu ya Redmi Note 8 Pro

Simu inatumia vioo vyenye uwezo mdogo wa kuonyesha rangi nyingi za kutosha

Kioo chake hakina hdr10 au hdr10+

Inatumia refresh rate ya kawaida hivyo kioo sio chepesi

4G yake ina masafa machache inayofanya baadhi ya mitandao duniani kutokubali 4G

Simu haina uwezo wa kuzuia maji kupenya kwani inakosa viwango vya IP67

Utendaji wa processor unapata shida ya kucheza baadhi ya gemu zenye graphics kubwa kwa ubora wa UHD

Hitimisho

Bei ya redmi note 8 pro inaifanya simu kuwa ya bei nafuu yenye ubora mkubwa

Ila kuna matoleo mapya ya simu yenye uwezo mkubwa kuliko note 8 pro

Mshindani wa simu hii ni redmi 10 na hata samsung galaxy a33

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram