SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu 10 za iPhone za bei rahisi 2022 (Na sifa zake)

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 18, 2022

Hii ni orodha ya simu 10 za iphone zenye bei inayoanzia laki mbili mpaka milioni moja na nusu.

Utaona simu za apple iphone za bei rahisi za ambazo zimetoka kuanzia mwaka 2015 mpaka 2022

Pia utafahamu sifa na ubora wa kila iphone iliyopo kwa ufupi.

Itasaidia kuelewa kama simu inafaa kwa wakati uliopo ama la.

Asilimia kubwa ya simu hizi ni used ama zilirudishwa kiwandani na kurekebishwa(refurbished)

iPhone XR

Simu ya apple iPhone XR imetoka mwaka 2018

Ni simu ya 4G yenye kamera moja nzuri inayoweza kuchukua mpaka video za 4k kwa spidi inayofika 60fps

iPhone xr ni simu ambayo haipitshi maji hata ukiizamisha kwenye kina cha mita moja kwa muda wa nusu saaa

iphone xr ya bei rahisi

Simu ina bodi ngumu yenye vioo vya gorilla glass upande wa nyuma na mbele.

Simu nyingi mpya za android zinazidiwa na iPhone xr kiutendaji.

Sababu kubwa processor yake aina ya Apple A12 Bionic ina nguvu sana.

Kwani ina alama zinazozidi 1000 kwenye geekbench

Simu inaweza kupokea mfumo endeshi mpya wa iOS 15.4.1 bila shida

Bei ya iPhone XR Tanzania

Bei ya iPhone XR yenye ukubwa wa 64GB inafika shilingi 545,670/=

Ni bei ya masoko ya mtandaoni ebay

Ila kwa Tanzania bei yake inaweza ikazidi hapo

Unaweza kuagiza kwa ebay na simu ikakufikia kiurahisi

Bei ya chini ya laki sita inastahili kwa sababu bado simu ina ubora mwingi unaoizidi simu ya Tecno Camon X

iPhone 11

Simu ya iphone 11 ni iphone ambayo ilitoka mwishoni mwa 2019

iPhone 11 haipitishi maji simu ikidumbukia kwenye kina cha mita mbili kwa muda wa nusus saa

Ina bodi ngumu kupasuka kwani inatumia kioo cha gorilla glass

iphone ya bei rahisi iphone 11

Ina mtandao wa 4G aina ya LTE cat 18 wenye kasi inayofika 1200Mbps

Kioo cha iPhone 11 ni cha ips lcd na resolution yake ni 828 x 1792 pixels

Kiuwezo, simu inazizidi simu za android za daraja kati zote na nyingine za daraja la juu za 2020-2022

Kwa sababu processor yake ya apple  a13 bionic nguvu yake ni kubwa

Bei ya iPhone 11 Tanzania

Bei ya iPhone 11 ya GB 64 ni shilingi 847,530.00/= kwa soko la ebay.

Kwa Tanzania hasa maduka ya simu makumbusho bei inaweza kuzidi 900,000/=

Ni bei inayoendana na simu mpya ya Samsung Galaxy A53 5G

Lakini Samsung Galaxy A53 5G inazidiwa na apple iphone 11

iPhone SE 2020

Simu ya iPhone SE 2020 ni simu ndogo ya iphone ya mwaka 2020.

Simu ina utendaji unaoendana na iphone 11.

Ila kuna vitu vimepungua kwenye se 2020

Ila utendaji wake ni mkubwa kuliko  redmi note 11 pro plus 5g

simu ya iphone bei rahisi

Kwa sababu inatumia processor ya apple a13 bionic.

Ni simu ambayo haipitishi maji ikizama kwa kina cha mita moja moja kwa muda wa nusu.

Betri yake ni ndogo na ukaaji wa chaji si mkubwa

Bei ya iphone se 2020

Bei ya iPhone se 2020 ya gb 64 ni shilingi 464,400.00/= kwa masoko ya ebay.

Kwa Tanzania kwenye maduka ya kariakoo bei yake inavuka 600,000/=

iPhone 8

iPhone SE ni simu ya iphone iliyotoka mwaka 2017

Simu inaweza kupokea toleo jipya la iOS 15.4.1 toka toleo la iOS 11

Ni simu nyingine yenye uwezo wa kuzuia maji kupenya.

iphone 8 bei rahisi

Betri yake ina ukubwa wa 1821mAh

Na linakaa chaji masaa machache yapatayo 66 kama simu haitumikii mara kwa mara

Kioo chake kina resolution ndogo ya 750 x 1334 pixels

Na bodi yake ni ngumu.

Uwezo wake wa processor unaizidi mbali sana simu ya redmi note 10 na Samsung Galaxy A52S.

Bei ya iPhone 8 Tanzania

Bei ya iphone 8 yenye ukubwa wa  64GB inafika shilingi 397,062.00/= kwa masoko ya ebay

Kwa maduka mengi ya simu ya kariakoo simu haizidi 500,000/=

Na maduka mengine kinondoni bey yake inazidi 600,000/=

iPhone 8 Plus

Simu ya iPhone 8 Plus ni simu ya mwaka 2017 yenye iOS 11

Simu inaweza kupokea mfumo mpya endeshi wa iOS 15.4.1

Processor yake ya apple a11 bionic ina nguvu na inazizidi simu nyingi mpya za android

iphone 8 plus ya bei nafuu

Betri ya iPhone 8 Plus ni dogo linalokaa masaa machache na chaji

Ukiwa unapiga simu masaa mengi simu itaisha chaji baada ya masaa 21

Kioo cha iphone 8 plus ni cha aina ips lcd chenye resolution 1080 x 1920 pixels

Simu ni fupi upande wa kimo

Bei ya iphone 8 plus Tanzania

Bei ya iPhone 8 plus yenye ukubwa wa 64GB inafika shilingi 464,400.00/= ebay

Ila kwa wauza simu wa maduka ya kariakoo bei kubwa zaidi ya 530,000/=

iPhone XS

Simu ya iPhone XS ni simu ndogo yenye kimo cha inchi 5.8

Simu imetoka mwaka 2018

Inatumia processor yenye nguvu aina ya Apple A12 Bionic.

iphone ya bei rahisi iphone xs

A12 Bionic inaizidi processor ya snapdragon 695 na dimesnity 1200

Hizi ni processor zilizotumiwa na simu nyingi za androiza daraja kati za mwaka 2020-2022

Betri yake ni dogo na linakaa na chaji masaa machache vilevile

Simu ina iOS 12 na inaweza kupokea toleo la iOS 15.4.1

Kioo cha iPhone xs ni cha oled chenye resolution kubwa ya 1125 x 2436 pixels.

Ni simu ambayo haipitishi maji

Bei ya iPhone XS Tanzania

Bei ya iPhone XS ya ukubwa wa GB 64 inafika shilingi 534,060.00/= ebay

Baadhi ya maduka ya kinondoni bei yake inazidi 600,000/= ila haivuki shilingi 700,000/=

iPhone X

Simu ya iPhone X ni simu yenye kimo cha inchi 5.8 ya mwaka 2017

Simu ina kioo cha OLED chenye resolution kubwa ya 1125 x 2436 pixels

Kioo kina ubora wa kuonyesha vizuri kwa sababu kina hdr10 na dolby vision

Inatumia processor yenye utendaji mkubwa

iphone ya bei nafuu iphone x

Processor yake ya Apple A11 Bioni inazipita simu nyingi mpya za android za madaraja ya kati

Betri lake ni dogo na halikai na chaji muda mrefu

iPhone X inaweza kupokea toleo jipya la iOS 15.4.1

Kamera yake si nzuri kwani haina dual pixel pdaf na hairekodi video ya 4K

Bei ya iPhone X Tanzania

Bei ya iPhone x ya ukubwa wa gb 64 inafika shilingi 487,620.00/=

Lakini kwa maduka ya simu dar es salaam bei yake inazidi 700,000/=

iPhone 7

Simu ya iPhone 7 ni iphone ya mwaka 2016

Kimo cha iphone 7 ni kidogo kwani inchi zake 4.7

Simu ina utendaji wa kuridhisha upande wa processor.

simu ya iphone bei rahisi iphone 7

Kwani chip ya apple a10 inaizidi mbali chip ya snapdragon 678 iliyomo kwenye Redmi note 10 ya 2021

Ina kamera moja yenye uwezo wa chini kwa sasa

Betri yake ni dogo na halitunzi chaji muda mrefu kwani ukubwa wake ni 1960mAh

Kioo cha iphone 7 ni aina ya ips lcd na kina resolution ndogo

Bei ya iPhone 7 Tanzania

Bei ya iPhone 7 ya ukubwa wa GB 32 ni shilingi 273,996.00/= ebay

Kuna maduka ya kariakoo yanayoiuza simu kwa shilingi laki tatu mpaka laki tatu na nusu

Hii ni simu ambayo wakati wake unaenda kuisha

iPhone 6s

Simu ya iPhone 6S ni simu ya mwaka 2015.

Ina kimo kifupi cha inchi 4.7

Simu haina uwezo wa kuzuia maji kupenya

Kioo cha iphone 6s ni cha aina ya ips lcd chenye resolution ndogo ya 750 x 1334 pixels

iphone ya bei rahisi ya iphone 6s

Hivyo ubora wake ni mdogo

Utendaji wake ni wa kawaida kwa sababu processor yake inachuana na snapdragon 678

Betri yake haikai na moto muda mrefu kwani ni dogo (1715mAh)

Bei ya iPhone 6s Tanzania

Bei ya iPhone 6s ya ukubwa wa 16GB inafika shilingi 270,000/= kwa Tanzania.

Lakini hii bei ni kubwa.

Kwa sababu iphone 6s ya GB 32 ni shilingi 227,556/= kwenye duka la mtandaoni la ebay

iPhone SE 2022

Simu ya iPhone SE 2022 ni toleo jipya la mwaka 2022 la iPhone

Ni simu yenye kimo kifupi cha inchi 4.7

Utendaji wa simu upande wa processor unazizidi simu karibu zote za android

Kwa sababu iPhone SE 2022 inatumia chip yenye nguvu zaidi kwa sasa ya ya Apple A15 Bionic

simu ya iphone bei rahisi

Simu ina kamera moja inayoweza kurekodi video za 4k kwa spidi mpaka ya 60fps

Betri yake haikai na chaji muda mrefu.

Ina betri dogo lenye ukubwa wa 2018mAh

Bei ya iPhone SE 2022 Tanzania

Bei ya iPhone SE 2022 inafika shilingi 1,302,642.00/=

Hii ni bei ya SE ya ukubwa GB 64

Maduka mengine hapa Tanzania bei ya simu itakuwa kubwa zaidi ya shilingi 1.3M

Maoni 16 kuhusu “Simu 10 za iPhone za bei rahisi 2022 (Na sifa zake)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram