SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na Bei ya Simu ya Tecno Pova 5g [Sifa Kiundani]

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 6, 2022

Simu ya Tecno Pova 5G ni simu ya 5G kutoka tecno

Hii ni moja ya simu ya daraja la kati ya mwaka 2021 inayoweza kuchuana na simu nyingi za redmitecno pova 5g muonekano

 

Hivyo uwezo wake wa utendaji unaifanya bei ya tecno 5G kuwa zaidi ya laki sita

Itakulazimu kufamu sifa zake na ubora wake kamera, kioo, bodi, processor na network ili ujiridhishe kama bei yake inakidhi vigezo

Ufafanuzi wote unapatikana kwenye hii posti

Bei ya Tecno Pova 5G Tanzania

Bei ya tecno pova 5g ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 8 ni shilingi 670,000/=

Pova 5G ni tofauti na Tecno Pova ya kawaida

Kiubora 5G ina vitu vingi vizuri hasa kwa kutazama uotfauti wa sifa za tecno pova 5g na tecno pova

Sifa za simu ya Tecno Pova 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Dimensity 900
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.4 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G68 MC4
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 11
  • HIOS 8.0
Memori UFS 3.1, 128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu (tecno macho matatu)

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 2MP
  3. QVGA
Muundo Urefu-6.9 inchi
Chaji na Betri
  • 6000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 670,000/=

Upi ubora wa Tecno Pova 5G

Ubora wa tecno pova 5g unapatikana kwa kiasi kikubwa kwenye utendaji

Kwa sababu simu inatumia processor ambayo ina nguvu kutoka kwa kampuni ya mediatek

Ina ubora wa kuweleka upande wa kioo

tecno pova 5g summary

Kutokana na kioo kuwa na resolution kubwa

Ina uwezo mkubwa wa kukaa na chaji masaa kwa maana betri yake ni kubwa sana

Simu ina mfumo wa memori unaopeleka data kwa kasi kubwa ya kusafirisha

Kasi kubwa inaimarisha utendaji wa simu

Uwezo wa Network

Tecno pova 5g inasapoti mtandao wa 5G na 4G kwa pamoja

Aina ya 4G simu inayotumia ni LTE Cat 18

Kasi ya LTE Cat 18 ni 1200 Mbps ambayo ni sawa na 150MBps

tecno pova 5g network

Kwa maana faili la ukubwa wa 1500MB litadownloadiwa kwa sekunde kumi

Kwa bahati mbaya hakuna mtandao wa simu unaotoa kasi hiyo hapa Tanzania

Lakini cha muhimu ni kuwa simu inakubali 4G ya mitandao yote Tanzania

Ubora wa kioo cha Tecno Pova 5G

Kioo cha tecno pova 5g ni cha aina ya IPS LCD

Kiubora, ips inaachwa mbali na vioo aina ya amoled ambavyo unaweza vimetumika kwenye simu ya tecno camon 18 premier

Ila kitendo cha kio chake kuwa na resolution ya 1080 x 2460 kinaongeza ubora wa screen kuonyesha vitu vizuri

Na kioo pia ni chepesi kutokana na kuwa na refresh rate ya 120Hz

Refresh rate kubwa huwa inafaa sana kucheza gemu

Japokuwa ulaji wa chaji huongezeka

Nguvu ya processor MediaTek Dimensity 900

Pova 5G inatumia chip ya mediatek dimensity 900 kufanya kazi zote zinazofanywa na simu

Dimensity 900 ni processor ya simu ya daraja la kati yenye idadi ya core nane (octa core)

Utendaji wake ni mkubwa

Kwenye app ya geekbench dimensity 900 ina alama 711 kwenye core moja

tecno pova 5g processor

Alama hizi ni nyingi kuliko zile za Helio G80 ya samsung galaxy a32

Utendaji mkubwa wa chip unachangiwa na uwezo wa kimuundo wa core kubwa na core ndogo

Uwezo wa core kubwa

Tecno hii yenye dimensity 900 ina core zenye nguvu kubwa zipatazo mbili

Kila core inafanya kazi kwa spidi inayofika 2.4 GHz

Hii inamaanisha processor yake ina mizunguko bilioni 2.4 kwa sekunde

Kila mzunguko mmoja unaweza kufanya kazi nne

Hivyo chip inaifanya simu kuweza kufungua app nyingi za kila aina kwa wakati mmoja kirahisi

Kwani muundo wa core zake ni Cortex A78 ambao ina matumizi madogo ya umeme kwa utendaji mkubwa

Uwezo wa core ndogo

Processor ina core sita zenye uwezo mdogo

Spidi ya kila core haizidi 2.0 GHz

Na zinatumia core aina ya Cortex A55

Hizi ni core ambazo zinatumia umeme mdogo sana

Na utendaji ni wa chini

Huwa ni maalumu kwa ajili ya shughuli ndogondogo simu inazofanya

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya tecno pova ina ukubwa wa 6000mAh

Ukubwa huu unaipa simu nafasi ya kukaa na chaji masaa ya kutosha kuliko kawaida

Ila simu inaweza chukua masaa zaidi ya matatu kujaa

Kwa sababu chaji yake haina kasi kubwa ya kupeleka chaji

Kasi yake ni 18W

Ukubwa na aina ya memori

Kuna toleo la aina moja tu la pova 5g upande wa memori

Ukubwa wa tecno hii ni GB 128 na RAM ya GB 8

Aina ya memori simu inayotumia ni UFS 3.1

Kasi ya UFS 3.1 kwa kusoma data ni 2100MBps na kuandika data ni 1200MBps

Spidi hiyo inafanya simu kufungua app kwa haraka

Hivi karibuni samsung imetangaza ujio aina ya memori yenye kasi zaidi ya UFS 4.0

Uimara wa bodi yaTecno Pova 5G

Kiujumla bodi ya pova 5g inatumia plastiki upande wa nyuma na pembeni

Ila tecno haijatumia vioo vya gorilla kuzuia simu kuvunjika

tecno pova 5g bodi

Hivyo ni muhimu kuweka kava na screen protector

Simu ni ndefu na urefu wake ni inchi 6.9

Kwa mtu anaependa simu ndefu basi tecno hii itamfurahisha kwa kiasi kikubwa

Ubora wa kamera

Tecno Pova 5G ni tecno macho yenye kamera moja tu iliyowekewa PDAF

PDAF iko taratibu kutambua kitu kinachopigwa picha ukilinganisha na dual pixel pdaf

Kamera mbili zilizabaki zina resolution ndogo

tecno pova 5g kamera

Na nyingine haitoi picha nzuri kabisa

Kamera hiyo ni aina ya QVGA

Kamera zake zinaweza kurekodi video za full hd pekee kwa spidi ya 30fps

Japokuwa dimensity 900 inaweza kuchakata video za 4K bila shida

Ubora wa Software

Simu inakuja na androdi toleo la 11 na mfumo wa HIOS 8.0

HIOS 8.0 una mpangilio wenye icon kubwa upande wa notification

Pia mpangilio wa settings una icons unaorahisisha mtumiaji kufanya uchaguzi mzuri

Pia ina app ambayo inaonyesha hali hewa ya eneo ulilopo mubashara kabisa

Yapi Madhaifu ya Tecno Pova 5G

Tecno Pova 5G ina mfumo mbovu wa kamera

Kamera zake haziwezi kurekodi video za 4K

Pia kamera zake mbili zina uwezo mdogo wa kutoa picha nzuri

Simu haiwezi kupiga picha eneo pana sana kwa kuwa hakuna kamera ya ultrawide

Kioo cha tecno kinaonyesha rangi chache kwa kuwa ni cha ips lcd

Simu haina uwezo wa kuzuia maji kwa sababu hakuna viwango vya IP-Ratings

Neno la Mwisho

Kwa mtumiaji anayejali utendaji wa simu pekee tecno pova 5g itakupa pafomansi kubwa

Hivyo bei yake ni rafiki

Lakini pia kwa bei hiyo hiyo unapata simu ya Redmi note 11 pro plus 5g ambayo ina vitu vya ziada

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram