SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Tecno Camon 11 na Sifa Zake (2022)

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

May 1, 2022

Simu ya tecno camon 11 ni simu ambayo imetoka mwaka 2018.

Bei ya tecno camon 11 ni chini ya shilingi laki mbili.

Tecno camon 11

Ni simu ambayo haiendani na nyakati za sasa

Utafahamu ubora wake kwa kuzijua sifa za simu husika

Bei ya tecno camon 11 Tanzania

Bei ya tecno camon 11 ya 32GB kwenye maduka ya Tigo ni shilingi 319,999/=

Ila sasa kiuhalisia simu haistahili kuuzwa kwa zaidi ya laki mbili

Unataka kujua sababu?

Zisome kila sifa ya camon 11

Sifa za tecno camon 11

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio A22
  • Core Zenye nguvu(-) –
  • Core Za kawaida(4) – 2.0 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 8.1
Memori eMMC 5.1, 64GB,32GB na 3GB,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 13MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.2inchi
Chaji na Betri
  • 3750mAh-Li-Po
Bei ya simu(TSH) 320,000/=

Upi ubora wa tecno camon 11

Kiuhalisia simu ya tecno cammon sio simu nzuri.

Kwa maana ina vitu vilivyo chini ya ubora kwa asilimia kubwa

Kikubwa ni kuwa ni simu ya 4G yenye spidi ya kuridhisha kama utakavyoona kwenye kipengele cha network

Mambo mingine yana ubora wa chini

Uwezo wa Network

Simu ya tecno camon 11 inatumia 4G aina ya LTE Cat 7

LTE Cat 7 inaweza kudownload faili kwa spidi inayofika 300Mbps

Tecno camon 11 network

Hivyo kama mitandao ya simu inatoa spidi hii basi mafaili makubwa yatamalizika kudownload muda mfupi

Simu ina masafa ya mtandao wa 4G ya aina tisa

Na ina masafa yote yanayotumika na mitandao ya simu Tanzania

Ubora wa kioo cha tecno camon 11

Kioo cha tecno camon 11 ni cha aina ya IPS LCD.

Hiki ni kioo kizuri kama kinakuwa na resolution kubwa

Ila camon 11 ina resolution ndogo ya 720 x 1500 pixels

Hivyo ubora wa kioo kuonyesha vitu kwa ustadi ni wa wastani

Kiubora, vioo vya amoled vinaizidi mbali vioo vya ips lcd.

Ndio maana simu kama camon 18 premier inakuwa na bei kubwa

Nguvu ya processor MediaTek Helio A22

Simu ya tecno camon 11 inatumia processor ya MediaTek Helio A22

Helio A22 ina jumla ya core nne.

Hizi ni core ndogo ambazo hutumika kufanya kazi ndogo

Kwa sababu zinatumia muundo wa Cortex A53

Ni muundo unaoifanya simu kuwa na nguvu ndogo ya kiutendaji

Kwenye geekbench helio a22 ina alama 161

Hii inafanya simu kupata shida wakati wa kucheza gemu kama Call of Duty: Mobile

Uwezo wa betri na chaji

Simu ina betri lenye ujazo mdogo wa 3750mAh

Hivyo ukaaji wa chaji ni mdogo

Na simu haina chaji yenye kasi.

Tarajia simu kuchukua masaa mengi kujaza betri dogo la 3750 mAh

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo mawili ya camon 11 upande wa memori.

Kuna tecno ya GB 32 na Tecno ya GB 64

Utendaji nndogo wa simu unachangiwa na memori ya eMMC 5.1 iliyopo kwenye simu hii

kwa sababu memori eMMC zina kasi ndogo ya kusafirisha data ukifananisha na memori za UFS

Bei yake inaweza kuwa kubwa zaidi kutokana na ukubwa wa memori

Uimara wa bodi ya tecno camon 11

Bodi ya tecno camon 11 si imara kwa sababu imeundwa kwa plastiki upande wa nyuma

Bodi za plastiki zina kawaida ya kuchunika rangi kadri umri wa simu unavyoenda

tecno-camon-11-bodi-ya-simu

Na pia haijawekewa ulinzi wa kioo cha gorilla upande wa mbele

Hivyo kava na screen protector inahitajika kuimarisha ulinzi wa simu

Bila hivyo simu ikidondoka kimo kirefu inaweza kuvunjika

Ubora wa kamera

Simu ina kamera mbili pekee upande wa nyuma.

Kamera kubwa ina resolution ya 13MP na inatumia teknolojia ya ulengaji ya kawaida sana

Kwa hiyo ubora wa picha wa kitu kinachotembea unaweza kuwa mdogo

Tecno camon 11 camera

Kiujumla mfumo wake wa kamera sio wa kuvutia.’

Simu haiwezi kurekodi video za 4k bali inarekodi video za full hd pekee.

Anayerekodi video anapaswa kutuliza mkono kwa sababu simu inakosa OIS

Ubora wa Software

Tecno camon 11 inakuja na toleo la android 8.1

Ni toleo ambalo bado linakubali apps nyingi za play store

Japokuwa kwa sasa kuna toleo jipya android 12

Kwa bahati mbaya simu haipokei toleo lingine la android

Yapi Madhaifu ya tecno camon 11

Simu ina mapungufu kwenye kila kitu unachokifahamu kinachounda simu

Ukianza na memori haina kasi inayoongeza ufanisi wa kiutendaji

Kamera zake hazitoi picha za kuvutia

Kioo chake kina resolution ndogo

Utendaji wa simu ni mdogo kutokana na kuwa na kutumia chip yenye nguvu ndogo

Neno la Mwisho

Tecno Camon 11 inamfaa mtumiaji mwenye bajeti ndogo sana ya simu

Kwani hata mtumiaji mpya anaweza kupata simu nzuri kwa bei ya chini ya laki tatu

Kwa mpenzi wa magemu hatofaurahia kutumia simu

Kuna simu ya bei nafuu ya redmi 9a na pia tecno spark 8 pro yenye utendaji wa kuridhisha

Wazo moja kuhusu “Bei ya Simu ya Tecno Camon 11 na Sifa Zake (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram