SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya sasa ya Samsung Galaxy S10 5G na Sifa Zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

July 17, 2023

Samsung Galaxy S10 5G ni simu ya mwaka 2019 iliyopo kwenye kundi la daraja la juu kwa wakati huo

Ni simu ya mwanzo kuja na teknolojia ya 5g.

Japokuwa ina miaka minne tangu iingie sokoni ila bado ni simu shindani kwa simu za mwaka 2023

samsung galaxy s10 showcase

Ndio maana bei ya samsung galaxy s10 5g inaendana na bei za simu mpya za madaraja ya kati

Hii inatokana na sifa zake nyingi kuendelea kuwa kubwa hata kwa sasa

Bei ya Samsung Galaxy S10 5G ya GB 256

Kwa Tanzania, Samsung Galaxy S10 5G inauzwa shilingi 770,000

Hii simu ina utendaji wa kuridhisha unaoziacha matoleo mengi ya sasa

Pia vitu vingine vinavyoifanya simu na bei hii ni ubora wa kamera, kioo na uwezo wa kupokea matoleo mapya ya android

Kitendo cha simu kukubali toleo lingine la android kunaipa simu thamani mpya hata kama inakuwa na muda mrefu tangu imetoka

Kwa kuangalia sifa zake zote utapata picha kiundani juu ya ubora wa samsung s10 5g

Sifa za Samsung Galaxy S10 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 9820
  • Core Zenye nguvu ya ziada(2) – 2×2.73 GHz Mongoose M4
  • Core Zenye Nguvu(2)-2×2.31 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.95 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G76 MP12
Display(Kioo) Super Amoled
Softawre
  • Android 9
  • One UI 4.1
Memori UFS 2.1, 256GB,512GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu

  1. 12MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(telephoto)
  3. 16MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 770,000/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy S10 5G

Galaxy S10 5G inakuja na kioo chenye ubora wa kuonyesha rangi nyingi kwa ustadi

Ina mfumo mzuri wa kamera unaopiga picha nzuri

Inatumia muundo wa memori unaosafirisha data kwa kasi

Utendaji wake mkubwa kutokana na aina ya chip iliyotumika

Inakubali kupokea matoleo mengine ya android mbali na toleo inalokuja nalo

Betri yake inadumu n chaji kwa masaa kwa sababu ni kubwa

Chaji yake inapeleka umeme unaowahi kulijaza betri kwa muda mfupi

Uwezo wa Network

Hii ni simu ya 5G lakini ina masafa machache ukizingatia 2019 5g haikusambaa sana

Kuna uwezakano wa kutopata 5g kwa baadhi ya mitandao ya simu hapa nchini

Mbali na hivyo simu ina mtandao wa 4G aina ya LTE Cat. 20

Aina hii ya 4G inaweza kudownload faili kwa kasi inayofika 2000Mbps

samsung galaxy s10 5g network

Kwa bahati mbaya kwa hapa Tanzania kiwango hiko kinabaki kuwa ni namba

Kwani hakuna mtandao wa simu unaotoa kasi hiyo kwa sasa

Kikawaida mitandao mingi nchini ikienda sana ni 75Mbps (bado ni kubwa hata hivyo)

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy S10 5G

Kioo cha samsung galaxy s10 5g ni aina ya super amoled chenye resolution kubwa ya 1440 x 3040 pixels

Kioo cha super amoled kina muundo unaoifanya kuonyesha rangi nyingi kwa usahihi

Mfano ni muonekano wa rangi nyeusi, kwenye super amoled rangi hukolea na kuonekana kuwa halisi tofauti na vioo vya ips lcd.

Na ubora wa kioo chake unachagizwa na uwepo wa HDR10+

samsung galaxy s10 5g display

HDR10+ ina ongeza kioo uangavu na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi zinazidi bilioni 12

Hivyo skrini hujitahidi kuonyesha vitu kwa muonekano halisi kama vinavyoenakana kwenye mazingira yake duniani

Uwepo wa HDR10+ inamaanisha kioo kina uangavu mkubwa

Nguvu ya processor ya Exynos 9820

Exynos 9820 ndio processor inayoipa uwezo samsung s10 5g kufanya kazi zake

Imeundwa katika sehemu nane huku sehemu zenye nguvu kubwa ya kiutendaji zipo nne (mbili zina nguvu kubwa zaidi)

Zenye nguvu zinatumia muundo wa Cortex A75 na Mongoose M4

Utendaji wa hizi ni mkubwa kiasi fulani na ulaji wake wa umeme ni wati 2

Japokuwa hizi core za mongoose zilizoonyesha udhaifu hivyo samsung waliamua kuachana nazo

Kwenye app zinazocheki nguvu za utendaji wa processor exynoss 9820 ina alama 800 ambazo ni nyingi

Kwani inaizid processor ya mediatek dimensity 800 ambayo ipo kwenye simu ya Oppo A94 5G

Uwezo wa betri na chaji

Simu inakuja na betri yenye ukubwa wa 4500mAh

Japo siku hizi betri huwa na ujazo wa 5000mAh ila 4500mAh ni kubwa

Kwa mfano samsung s10 5g inakaa na chaji kwa muda wa masaa yanayozidi 12 simu ikiwa kwenye intaneti

Chaji yake ina ukubwa wa 25W ambayo ndani ya dakika 80 inajaza simu kwa 100%

Hivyo simu inakaa muda mfupi kuijaza

Hii samsung inasapoti wireless charge(kuchaji bila kutumia waya)

Unaigusisha simu na kifaa fulani kisha chaji inaanza kuingia

Ni nadra kwa simu za nyingi za matoleo ya kati kwa sasa kuwa na mfumo huu

Japo tecno wameweka kwenye Tecno Camon 20

Ukubwa na aina ya memori

Samsung Galaxy S10 5G zipo za matoleo mawili kwenye upande wa memori

Kuna ya GB 256 na ya GB 512

Zote zinatumia memori zenye muundo wa UFS

Hivyo kasi ya kusafirisha data ni nzuri kwani spidi yake inafika 1200MBps

Upande wa RAM zote zina GB 8

Kwenye simu za android RAM kubwa ni kitu cha msingi

Maana kama unacheza gemu sana sehemu kubwa ya RAM hujaa kitu kinachofanya simu kuwa nzito kiutendaji

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy S10 5G

Bodi ya samsung galaxy s10 5g ina uwezo wa kuzuia maji kupenya kwani ina viwango vya IP68

IP68 humaanisha kuwa simu inaweza kustahimili kutopitisha maji kama ikizama kwenye kina cha mita 1.5 kwa muda wa nusu saa

Kwenye skrini kumewekwa kioo cha Gorilla glass 6

samsung s10 5g body

Kwenye majaribio kioo cha gorilla glass kinaweza kuepuka kupasuka kama simu ikianguka kwa kimo cha mita 1.6

Hata hivyo simu kuotpasuka kunategemea na uso pamoja na asili ya eneo hivyo majaribio ya maabara pekee hayatoshi kutoa hitimisho

Ubora wa kamera

Ubora wa kamera wa Samsung Galaxy S10 5G hauna tofauti na ule S10 zingine

Ina jumla ya kamera tatu zote zina megpixel 12

samsung s10 5g camera

Megapixel 12 inatosha kupiga na kurekodi picha nzuri ukizingatia tayari simu ina teknolojia zinazohitajika kupiga picha vizuri

Kamera zake zote zina dual pixel pdaf zinazosadia kamera kulenga kitu kwa ustadi hivyo kukusanya data za kutosha cha kitu kinachopigwa picha

Ubora wa picha ni mkubwa na kiwango cha noise nyakati sio rahisi kuweza kukiona kwa macho

samsung s10 5g camera 2

Kmaera inajitahidi kutoa rangi zenye muonekano halisi

Kama kitu ni cheusi kitatokea kwa jinsi kinavyoonekana na sio kwa kuongeza mng’ao

Upande wa video simu inaweza kurekodi mpaka video za 4K na kwaa kiwango cha HDR10+

Si kawaida kuikuta kamera ya daraja ya kati ya mwaka 2023 kuwa na uwezo huo

Ubora wa Software

Wakati inatoka ilikuwa inakuja na android 9, kwa sasa inakubali mpaka toleo la android 12

Toleo jipya ni android 13 ambalo kwenye hii haipokei sapoti ila unaweza kuliweka kama ukiwa mtaalamu

samsung galaxy s10 5g software

Na pia inaweza kutumia mfumo wa One UI 4.1 ambapo toleo la sasa ni One UI 5

Hata hivyo software za android 12 na One UI 4.1 zina vitu karibu vyote vya muhimu vinavyohitajika na mtumiaji yoyote wa simu

Washindani wa Samsung Galaxy S10 5G

Kununua samsung galaxy s10 5g kwa mwaka 2023 itakulazimu kuangalia matoleo mapya ya simu za daraja la kati

Kwa sababu teknolojia imesogea mbele zaidi na inapatakana kwa bei nafuu

Mshindani wa kwanza kabisa ni simu ya Oppo Reno8 5G

Reno8 inaizidi kila kitu galaxy s10 5g isipokuwa kwenye kamera na bei ya oppo reno8 inakaribia laki tisa

Simu kali nyingine itakayokuja akilini ni Tecno Camon 20 Pro 5G

Camon 20 Pro 5G ina kioo chenye refresh rate inayogusa 120Hz na kamera ya 4K

Ambapo bei ya camon inaenda kwenye laki saba

Mshindani mwingine ni Redmi Note 12 5G

Neno la Mwisho

Simu ya Samsung Galaxy S10 5G bado ni simu nzuri kwa mwaka huu na miaka mingi ijayo

Bei yake inaendana na sifa zake na ni shindani kwa matoleo mapya ya daraja la kati

Lakini kumbuka bei hiyo  inaweza kukupa simu nzuri zaidi

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram