SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya iPhone 14 Plus na Sifa Zake Muhimu (2023)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

January 16, 2023

Simu ya iPhone 14 Plus ni iphone ya mwaka 2022 ambayo bado ni mpya kwa mwaka 2023

Bei ya iPhone 14 Plus kwa Tanzania ni zaidi ya milioni moja na nusu ama zaidi kutegemeana na ukubwa wa memori

Kumbuka iPhone 14 Plus ni toleo jipya lililotoka miezi ya mwishoni mwaka 2022

iphone 14 plus mbele

Ukiitazama vitu vipya ambavyo vimewekwa kwenye simu utaelewa sababu ya kuwa na bei kubwa

Kwenye makala hii kuna ufafanuzi wa sifa za iphone 14 plus zinazoipa simu ubora unaochangia bei yake kuwa ghari

Bei ya iPhone 14 Plus ya GB 256

Bei ya hii simu kwa hapa Taznania inafika shilingi 2,800,000/=

Bei ya GB 128 ni nafuu japo si kwa utofauti mkubwa.

Kuna vitu vingi vinavyoifanya simu  kuuzwa hiyo bei kama utakavyoona baadae

iphone 14 plus summary

Lakini kitu kikubwa ni uwezo mkubwa wa kiutendaji wa processor unaochangia simu hii kuzipita simu nyingi za Android

Ubora wa processor unaisaidia hii simu kukaa na betri masaa mengi kuliko hata iphone 12 pro max

Sifa za Simu ya iPhone 14 Plus

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) -2×3.23 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.82 GHz Blizzard
  • GPU-Apple GPU (5-core)
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED,
Softawre
  • iOS 16
Memori NVMe, 256GB,128GB, 512GB na RAM  6GB
Kamera Kamera MBILI

  1. 12MP, dual pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4323mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 2,800,000/=

Upi ubora wa iPhone 14 Plus

Kikawaida simu zinazouzwa kwa bei kubwa huzingatia ubora kwenye nyanja karibu zote

Kitu ambacho kipo kwa simu za apple

Kwa mfano, iphone 14 plus inakubali masafa ya mitandao karibu yote duniani

Kwa maana unaweza ukasafiri na simu sehemu yoyote duniani na ikafanya kazi

Kuna baadhi ya simu kama umeagiziwa kutoka Marekani ikija Tanzania inashindwa kushika network

Lakini kwa iphone karibu zote hazipo hivyo

Pia hii ni simu ambayo imewekewa ulinzi wa kutopitisha maji endapo ikidumbikia kwenye maji

Hii inakupa uhuru wa kuitumia simu hata kwenye mvua ikiwa inanyesha

Uwezo wa Network

Simu ya iphone 14 plus ni simu ya 5G inayokubali pia 3G na 4G

Ina uwezo wa kupakua faili kwa sekunde chache kwani ina 5G inayokubali masafa ya mmWave

mmWave ni aina ya masafa ya 5G yanayosafirisha data kuanzia masafa ya 24GHz na kuendelea

iphone 14 plus network

mmWave inatoa spidi inayofikia 2Gbps ambayo ni sawa na 255MBps kwa maana file ukubwa wa MB 255 simu inadownload kwa sekunde moja tu

Taasisi ya Signal Research Group ya Marekani iliripoti kasi inayofikia 2Gbps kwenye mji wa Tokyo Japan

Aina hii ya 5G ni tofauti na ya Vodacom Tanzania kwani yenyewe ni ya masafa ya kati

Kiujumla hupaswi kuwaza kuhusu network ya simu hii kama mtandao upo vizuri

Ubora wa kioo cha iPhone 14 Plus

iPhone 14 Plus inatumia kioo cha OLED kinachoitwa Super Retina XDR OLED

Super Retina XDR OLED kimeundwa na apple wenyewe kwa kushirikiana na samsung

Lengo kubwa ni kupunguza mapungufu ambayo yanatokea mara kwa mara kwenye vioo vya OLED kama vile burn-in

Apple wanadai vioo vya XDR OLED vinatoa taswira nzuri ya muonekano kutokana na kuwa na resolution kubwa, usahihi wa rangi, uwezo  wa kuonyesha rangi nyeusi halisi na rangi nyeupe halisi na kuwa na uwezo kuonyesha rangi nyingi

iphone 14 plus display

Kivyovyote vile, vioo vya OLED huwa vina ubora mkubwa ukilinganisha na vioo vya IPS LCD

Ukizingatia iPhone 14 plus kioo chake kina HDR10, Dolby vision na Uangavu unaofikia kiwango cha nits 800

Nits zikiwa nyingi zinasaidia simu kuonyesha vizuri kabisa ikiwa inatumika juani kwenye mwanga mkali

Mwanga mwingi wa jua huwa unasababisha baadhi ya simu kutoonyesha vitu vizuri mpaka uweke mkono kwa juu

Nguvu ya processor Apple A15 Bionic

Kwenye upande wa simu janja apple huzipita kampuni nyingi linapokuja swala la kuwa processor za simu zenye nguvu

Processor ikiwa na nguvu inakuwa na utedaji wa haraka na ufanisi wa matumizi madogo ya betri

Simu ya iphone 14 plus inatumia chip apple A15 Bionic

Ni chip ambayo inatumika kwenye iPhone 13 Pro Max kitu kinachofanya hii simu kuzidiwa na iPhone 14 Pro kwa mbali.

iphone 14 plus processors

Hii chip ina idadi ya core 6 na inatumia GPU aina ya Apple GPU (5 cores)

Moja ya kazi kubwa ya GPU ni katika kucheza magemu, gpu yenye nguvu hufanya gemu kuchezeka kwa muonekano mzuri bila kukwama wala kuganda

Bila gpu hutoweza kucheza gemu kwenye simu.

Apple A15 Bionic ina core (sehemu ya processor) mbili kwa ajili ya kufanya kazi kubwa ama kazi nyingi kwa wakati mmoja

Kwenye app ya nguvu za processor za simu, A15 Bionic ina alama 1700 kwenye geekbench na 795947 kwenye antutu

Hii inamaanisha uwezo wa iPhone 14 Plus ni mkubwa kuliko Samsung Galaxy S22+

Uwezo wa betri na chaji

Ukubwa wa betri wa iPhone 14 Plus ni 4323mAh

Unaweza ukadhani simu hii haikai na chaji kwa kuwa betri yake halijafika 5000mAh

Mambo yapo tofauti, kwani ni simu inayokaa na chaji muda mrefu sana kuliko hata zenye 5000mAh

Kwenye majaribio ya GSMArena, iPhone 14 Plus imeweza kukaa na chaji kwa masaa 16 simu ikiwa inaperuzi intaneti muda wote

iphone 14 plus chaji

Na imestahamili ukaaji wa chaji wa masaa 11 ilipokuwa inaperuzi intaneti kwa mtandao wa 5G

5G inakula chaji kutokana na kasi kubwa ya kupokea na kutuma data

Kwa bahati mbaya simu haiji na chaji, utalazimika kununua chaji kama hauna chaji ya iPhone

Ukubwa na aina ya memori

Unaweza ukamiliki apple yenye ukubwa wa GB 128, 256 au GB 512

Ukubwa wa memori unasababisha bei kuongezeka kama ilivyo kawaida

Aina ya memori za simu zote za apple huwa ni NVMe

NVMe ni aina ya memori ambayo ina uwezo wa kusoma na kuhifdhi faili kwa kasi inayofika 5444MBps

Spidi hii inaiwezesha simu kufungua app kwa haraka, kuzima ama kuwaka kwa sekunde chache na kukopi mafaili ndani ya muda mfupi

Memori yenye kasi inaboresha utendaji wa simu, iphone zote za 2022 zinatumia RAM ya 6GB

Uimara wa bodi ya iPhone 14 Plus

Bodi ya iPhone 14 Plus imeundwa kwa alminiamu upande wa pembeni

Na glass za gorilla nyuma na mbele

Bodi yake imetengenezwa iweze kuzuia maji kupenya hata ikiwa imezama kwenye kina cha maji cha mita 6 kwa muda wa nusu saa

Ni tofauti na baadhi ya simu zingine ambazo huhimili kwenye kina cha mita 1.5

iphone 14 plus body

Vioo vya gorilla na vyenyewe ni himilivu simu ikianguka urefu mkubwa (kimakadirio mita 2)

Simu hii inasapoti laini mbili au moja inategemea na soko lengwa

iPhone 14 Plus zinazouzwa Marekani hazina sehemu ya kuwekea laini bali hutumia eSIM (embeded SIM)

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera mbili upande wa nyuma na kamera moja upande wa mbele (selfie camera)

iphone 14 plus kamera

Kamera zake zinatoa picha na video kwa usahihi mkubwa rangi na muonekano halisi

Inatumia ulengaji aina ya dual pixel pdaf ambao hufanya kamera ya simu ifokasi kwa haraka inapopiga kitu kinachotembea mfano ukiwa unapiga ndege anayepaa angani

iphone 14 plus photo quality

Uwezo mwingine ni kurekodi video za 4K kwa idadi ya fremu mpaka 60fps na video za full hd mpaka 240fps

Video yenye fps kubwa inakuwa ni “smooth” kwa maana video iliyorekodiwa inakuwa inaonyesha kila hatua

Kwenye mwanga hafifu simu inajitahidi kwa kiasi kuonyesha vitu bila kuathiriwa na mwanga mdogo hasa nyakati za usiku

Japokuwa mapungufu yapo ambayo ni ngumu kwa mtumiaji wa kawaida kutambua hizo “noises”

iphone 14 plus low light camera

Ubora wa Software (iOS 16)

Kila toleo jipya la iphone huambatana na mfumo mpya endeshi

Ambapo matoleo ya 2022 yana iOS 16.

Kufahamu vitu vipya vya iOS 16 unaweza pitia, makala ya simu ya iphone 14 pro max

Yapi Madhaifu ya iPhone 14 Plus

Simu haina sehemu ya kuweka memori kadi

Inatoa changamoto ya kutanua memori simu inapojaa hasa toleo la GB 128

Kwa mwingine GB 128 ni nyingi ila ukiwa unarekodi sana video za 4K memori itajaa tu

Neno la Mwisho

iPhone 14 Plus haina tofauti kubwa na iPhone 13 Pro Max

Ikizingatiwa zote zinatumia chip ya aina moja

Bei ya iPhone 14 Plus inaweza kukupa iPhone 13 Pro Max ambayo inakuja na kamera tatu

Kwani kuna aina moja ya kamera haipo kwenye hii simu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram