SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya infinix hot 30i na Sifa Zake Zote

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 30, 2023

Simu ya Infinix Hot 30i ni infinix mpya iliyotoka pamoja na toleo la Infinix Hot 30

Tofauti ya Hot 30i na Hot 30 ni nguvu ya kiutendaji ambapo hot 30 ina memori kubwa na kioo kizuri

infinix hot 30i showcase

Ila kiutendaji infinix hot 30 inaizidi kidogo mwenzake

Ndio maana bei ya infinix hot 30i inaikaribia kidogo hot 30

Ukisoma sifa zake zote utagundua utofauti mdogo baina ya simu hizi mbili

Bei ya Infinix Hot 30i Tanzania

Infinix ya GB 128 kwa hapa nchini inapatikana kwa bei ya shilingi 315,000/=

Kikawaida matoleo ya hot yenye harufi “i” huuzwa kwa bei nafuu zaidi

Hii ipo tofauti kwani uwezo wake ni mkubwa na unaizidi simu ya hot 12i ambayo unaweza ipata kwa laki mbili na nusu

Hivyo bei kubwa isikushangaze, kinachopaswa kujiuliza ipi ya kuichukua kati ya matoleo mawili ya hot 30

Jibu linategemea na nini unapendelea kwenye simu, fuatilia sifa zake uelewe

Sifa za Infinix Hot 30i

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Unisoc T606
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×1.6 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.6 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MP1
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 12
  • XOS 10.6
Memori UFS 2.1, 128GB na RAM 4GB
Kamera Kamera moja

  1. 8MP,AF(wide)
Muundo Urefu-6.56inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 315,000/=

Upi ubora wa Infinix Hot 30i

Simu inatumia mfumo wa memori wenye kasi kubwa ya kusafirisha data

Inadumu na chaji muda mrefu

Utendaji wake ni wa kuridhisha

Ina kioo chenye refresh rate kubwa inayofanya simu kuwa laini wakati wa kuperuzi

Inakuja na nafasi kubwa unayoweza kuhifadhi vitu vingi

Urefu wake ni wa wastani

Mambo mingine yana ubora wa kawaida kama utakavyoona kwenye maelezo yaliyopo

Uwezo wa network

Simu inasapoti mtandao mpaka wa 4G aina ya LTE Cat 7

LTE Cat 7 ina kasi ya juu kabisa ya 300Mbps sawa na 37MB/s

Hii inamaanisha kama mtandao wa simu unakupa kasi hii basi faili la 37MB linaalizika kudownload kwa sekunde moja

Tanzania, mitandao ya simu za mkononi hawatoi kiwango hiko cha spidi

Hata hivyo kutokana  na gharama za intaneti kuongezeka unaweza usifurahie kasi hii hata kama ikiwepo

Pamoja na kuwa simu imetoka mwaka 2023 ila haijaja na 5G

Kuna simu za 5G nyingi za chini ya laki tano ila hapa Infinix wamejisahau

Uzuri kuwa mitandao ya Vodacom na Tigo wameanzisha hii huduma japo haijasambaa sana

Ubora wa kioo cha Infinix Hot 30i

Kioo cha infinix hot 30i ni cha ips lcd chenye refresh rate ya 90Hz

Resolution ya kioo sio kubwa kwani kina 720 x 1612 pixels, baadhi ya zitaonekana kuwa kubwa sababu ya ujazo mdogo wa pixels

Ila ukiwa unacheza gemu utafurahi kwa sababu ya kiwango kikubwa cha refresh rate

infinix hot 30i display

Ikiwa kubwa inafanya simu ni nyepesi ni skrini kubadilika kwa unadhifu pindi unapotachi

Hasara ya refresh rate kubwa ni kutumia umeme mwingi wa betri

Hata hivyo hii simu betri yake ni kubwa

Unagavu wa kioo unafika nits 500, kwenye jua kali kioo kinaweza kisionyeshe kwa mwanga mwingi

Nguvu ya processor Unisoc T606

Ni kawaida kwenye simu za android kukuta chip zilizotengenezwa Taiwan(mediatek) au Marekani(Snapdragon)

Unisoc ni kampuni ya china, chip zake nyingi huwekwa kwenye simu za daraja ya chini ama la kati

Utendaji wa Unisoc T606 unaenda na kuzidiwa kidogo na chip ya Helio G88 iliyopo kwenye Tecno Spark 10 Pro na Hot 30

infinix hot 30i processor

kwenye app ya kupima nguvu za processor ya geekbench, hii processor ina alama 311

Hivyo sio chip nzuri kucheza magemu yanayohitaji nguvu kubwa kama PUBG Mobile 2018

Kiujumla ina core(sehemu) nane ambapo core zenye nguvu zaidi zinatumia muundo wa Cortex A75

Kitu kikubwa zaidi utakachonufaika na Unisoc T606 ni ulaji mdogo wa umeme kwa gharama ya utendaji

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya infinix hot 30i ina ukubwa wa 5000mAh

Na kasi ya chaji yake ni wati 18

Kasi ya chaji inaweza kujaza betri kwa muda unaozidi masaa mawili

Ukiwa unatumia intaneti muda wote bila kuzima data hii simu inaweza kukaa masaa zaidi ya 15

kwa mtumiaji asiyetumia intaneti mara kwa mara atashuhudia ukaaji wa muda mrefu

Hii ni sehemu nyingine ambao 30i inazidiwa na hot 30 ambayo ina chaji ya wati 33

Ukubwa na aina ya memori

Simu inatumia memori aina ya UFS 2.2 ambayo kasi yake ya kusafirisha data 1200MBps

Kasi hii inafanya simu kuwaka kwa haraka na appliksheni kufunguka kwa sekunde chache

Pia Hot 30i ina toleo moja tu lenye memori ya GB 128 na RAM GB 4

Hata kama memori itajaa kuna sehemu ya kuongeza memori kadi tofauti na simu za siku hizi za madaraja ya juu

Uimara wa bodi ya Infinix Hot 30i

Bodi ya Infinix hot 30i ni ya plastiki, plastiki huwa ni rahisi kupauka rangi ukilinganisha na simu zenye vioo

Kuimarisha ubora utakaokaa muda mrefu ni vizuri ukawa unaitumia kavaa mara kwa mara

Simu haina viwango vya IP hivyo inamaanisha haina uwezo wa kuzuia maji pindi ikizama kwenye kina kikubwa

Umakini unahitajika hasa unapotumia kwenye mvua au unapoenda kuogelea

Pia ina kimo cha wastani na sio nzito sana

Ubora wa kamera

infinix hot 30i ina kamera mbili na haina ulengaji wa PDAF

Kamera kubwa ina megapixel 13, wakati kamera ya pili sio ina lenzi ambayo haipigi picha (yaani ni depth)

infinix hot 30i kamera

Kwa kuangalia haraka ni kuwa mfumo wa kamera sio mzuri sana

Sio kwa sababu ina megapixel 13, hapana, kiwango cha 13MP ni kikubwa kutoa picha nzuri

Ila ukosefu wa teknolojia ya pdaf ni ishara  kuwa hii kamera ni ya kawaida sana

infinix hot 30i kamera photo quality

Upande wa video simu inaweza kurekodi video za full hd(1080p)

Na haina OIS kwa ajili ya kutuliza video wakati ukirekodi huku ukiwa unatembea

Ubora wa Software

Ungetaraji kuwa simu yoyote ya mwaka 2023 inafaa ije na Android 13

Ila kwa infinix inakuja na Android 12 na mfumo XOS wa zamani kidogo yaani XOS 10.6

infinix hot 30i software

Hakuna tofauti kubwa sana kati Android 12 na 13

Ila simu kuwa na mfumo zaidi inapendeza

Mfumo mpya unaipa simu thamani kubwa na muda mrefu wa kutumia appliksheni mbalimbali bila shida

Washindani wa Infinix Hot 30i

Mshindani wa kwanza na mkubwa zaidi kwa hii simu ni Tecno Spark 8C

Spark 8C ina mfanano wa kila kitu mpaka utendaji ila tecno ina bei ndogo zaidi

Mshindani mwingine ni Samsung Galaxy A04 na Redmi Note 10 5G

Bei ya simu za samsung na redmi ni chini ya laki nne kwa sasa

Faida ya hot 30i ni kuwa inakuja na memori kubwa ila mambo mengine yanafanana

Hata pixel 3 iliyotumika ni mshindani wa hii simu

Neno la Mwisho

Infinix Hot 30i ni kama mbadala wa toleo la infinix hot 30

Kwa maana kama bajeti imebana sana unaweza ukasogeza siku

Ugumu utakaopata hii simu ni kwenye bei kwani inaipeleka kwenye ushindani mkali na matoleo mengi ya laki nne

Maoni 28 kuhusu “Bei ya infinix hot 30i na Sifa Zake Zote

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram