SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya infinix hot 30 na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 30, 2023

Simu ya Infinix Hot 30 imeingia sokoni mwishoni wa mwezi wa tatu 2023

Ni simu mpya ya infinix 2023 ya daraja la kati yenye utendaji wa wastani na inayoweza fanya kazi vizuri kwenye vitu tofauti tofauti

infinix hot 30 showcase

Bei ya Infinix Hot 30 kwa Tanzania ni zaidi ya laki nne

Bei yake inachagizwa zaidi na kuja na kiwango kikubwa cha memori na pia utendaji wa kuridhisha kama utakavyoona kwenye hii makala

Bei ya Infinix Hot 30 ya GB 256

Kwa maduka ya hapa Tanzania bei yake ni shilingi 465,000/=

Hii ni infinix ambayo ipo tofauti na simu kama infinix smart 6 kwenye maeneo mengi

Ukianzia chaji,kioo, kamera na nguvu ya processor utaona sababu za msingi kwa nini bei ya simu inakaribia laki tano

infinix hot 30 summary

Ndio maana hata ukiangalia ubora wa picha, picha zinatoka vizuri japo si kwa kiwango kama cha simu za samsung galaxy s23 au iphone 14

Ila kwa kuzingatia bei simu inaendana na ubora wake

Na bei hiyo pia inaipeleka simu kwenye ushindani  na simujanja kutoka Tecno, Redmi, Samsung na Motorola

Sifa za Infinix Hot 30

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G88
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 13
  • XOS 12.6
Memori 256GB na RAM 8GB
Kamera Kamera MBILI

  1. 50MP,AF(wide)
  2. 0.08MP(Depth)
Muundo Urefu-6.78inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 465,000/=

Upi ubora wa Infinix Hot 30

Hot 30 ina kioo chenye refresh rate kubwa kinachofanya simu kuwa nyepesi unapotachi

Ni simu ndefu hivyo skrini inakuwa nzuri zaidi kama unapenda kusoma vitabu

Inakaa na chaji muda mrefu na chaji yake inajazaa betri kwa muda mfupi

Ina utendaji wa wastani unaofaa kwa kazi nyingi za kwenye simu

Inakuja na memori yenye uwezo wa kuhifadhi mafaili mengi

Kamera yake inatoa picha nuzri hasa kwenye mwanga mwingi

Uwezo wa Network

Mtandao unasapoti mpaka mtandao wa 4G pekee

Kwani processor iliyotumika haisapoti 5G

Inatumia 4G ya LTE Cat 7 ambayo kasi yake ya kupakua vitu ni 300Mbps

Kwa maana kama unapakua gemu la Call of duty lenye 2GB simu itamaliza kudownload kwa sekunde 55

infinix hot 30 network

Mitandao mingi hapa Tanzania huwa ina spidi ya 4G ambayo ni ngumu kufika 100Mbps

Hivyo uwezo wa network ya 4G wa hii infinix unaweza usinufaike nao

Ila kwa 5G inawezekana japokuwa inapatikana sehemu chache

Pia 4G yake ina masafa yote ya mitandao ya simu iliyopo nchini

Hakuna mtandao utakaogoma kwenye intaneti

Ubora wa kioo cha Infinix Hot 30

Infinix Hot 30 inakuja na kioo cha IPS LCD chenye resolution ya 1080×2460 pixels(full hd+)

LCD huwa havina ubora mkubwa kwenye usahihi wa rangi ukilinganisha na kioo cha amoled

Ila lcd ikiwa na resolution kubwa muonekano wa vitu unakuwa mzuri kama ilivyo kwenye hii simu

Na pia skrini yake ina refresh rate inayofika 90Hz

infinix hot 30 display

Ukiwa unaperuzi(kuscroll) kioo kinakuwa na kasi ya haraka na muonekano wenye kuvutia macho

Simu inakupa chaguo la kuzima hii refresh rate kwa sababu refresh rate kubwa hula chaji nyingi

Uangavu wa kioo ni nits 500, kwa maana ukiwa kwenye jua kioo kinaweza kisitoe mwanga mkubwa wa kuonyesha vitu vizuri

Nguvu ya processor MediaTek Helio G88

MediaTek Helio G88 ndio chip inayoipa nguvu simu ya hot 30

Utendaji wake sio mkubwa kama processor ya Dimensity 700 ila utaweza kufanya vitu vingi unavyovihitaji

Utendaji wake wa kiwango cha kati unasababishwa na sehemu yenye nguvu(zipo mbili) kutumia muundo wa Cortex A75

infinix hot 30 processor

Wakati core kwa ajili ya kazi zinoumi nguvu ndogo zipo SITA.

Hata hivyo magemu mengi yanacheza vizuri ila Yale makubwa utalazimika kupunguza ubora wa graphics.

Vinginevyo unaweza kukuta simu inapata joto Sana na pia kucheza gemu kwa kukwama

Mfano wa magemu hayo ni genish impact na call of duty

Uwezo wa betri na chaji

Chaji inayokuja na Tecno Ina Kasi ya wati 33

Chini ya masaa mawili simu inajaa kwa 100% kutokana 0%

Ukiwa huitumii Sana betri yake inaweza kudumu mpaka siku mbili

infinix hot 30 charge

Ukiwa muda wote unatumia intaneti na basi inaweza chukua mpaka masaa 15 kuisha chaji.

Sababu ya ukaaji wa chaji ni kuwa betri Ina ukubwa wa 5000mAh na chip ya simu haitumii nguvu kubwa Sana kufanya kazi zake na pia uangavu wa kioo sio mkubwa

Ukubwa na aina ya memori

Aina ya memori iliyopo kwenye hii simu ni eMMC 5.1

Huu ni mfumo kwa Sasa hautumiki na simu mpya nyingi kwani usafirishaji wake wa data sio mkubwa kama mfumo UFS 2.1 na kuendelea

Kama unawasha simu ya UFS 2.1 na ya eMMC 5.1, basi ya UFS itawahi kuwaka

Kuna toleo moja tu la Infinix upande wa memori ambayo Ina GB 256 na RAM 8

Simu inarushusu kuongeza kiwango Cha RAM mpaka GB 16

Uimara wa bodi ya Infinix Hot 30

Bodi ya Infinix hot 30 Ina muundo wa flati ikiwa ni plastiki upande wa nyuma

Hivyo basi ni muhimu kutumia kava na uzuri utakuta kwenye box

infinix hot 30 body

Simu Haina viwango vya IP vinavyoashiria uwezo wa kuzuia maji kupenya kama ikizama ndani ya maji

Pia ni muhimu kuweka skrini protekta kulinda kioo Cha simu kwani Haina vioo vya gorilla

Ubora wa kamera

Idadi ya kamera za Infinix hot 30 ni mbili ila kiuhakisia ni kamera moja tu inyopiga picha

Kwa sababu kamera ya pili yenye lenzi ya depth huwa haipigi picha Bali kwa ajili ya kupima kitu kinachopigwa picha na umbali wa kamera

infinix hot 30 camera

Kamera kubwa inakuja na megapixel 50 na ulengaji wa AF (sio PDAF)

Muonekano wa picha ni mzuri japo kuna kiwango Cha noise kwa mbali

infinix hot 30 camera 1

Ila usahihi wa rangi sio wa kiwango kikubwa(rangi nyeusi inkuwa n mng’ao usioendana na m

Ubora wa Software

Hii infinix inakuja na android 13 na mfumo wa XOS 12.5

Hapa kuna maelezo kuhusu mfumo wa android 13

Moja ya applikesheni utakayoipata kwenye hii simu ni AI Gallery inayokupa uwezo wa kuhariri picha kwa kutumia teknolojia ya artificial inteligence

infinix hot 30 software

Mfumo wa AI unasaidia kufanya editing kwa kuzingatia rangi sahihi za vitu unavyovihariri

Ila simu inakuja na app nyingi(bloatware) ambazo nyingi sio muhimu kwako

Kuna baadhi zinaweza kutoka lakini nyingine hazitoki

Washindani wa Infinix Hot 30

Kuna simu nyingi za hivi karibuni na za miaka ya nyuma kidogo ambazo unapata kwa bei ya hot 30 au zenye uwezo sawa na kuzidiana kidogo

Kuna simu ya Xiaomi Poco M4 5G ambayo ina 5G na utendaji unaizidi hii simu, bei ya poco kwa Tanzania ni shilingi laki nne na thelathini

Mshindani mwingine ni Samsung Galaxy A14, hii ina kamera tatu ikiwemo kamera ya kupiga eneo pana yaani ultrawide ambayo haipo kwenye  hot 30 bei yake ni chini ya laki nne na nusu

Simu janja nyingine Redmi Note 11 yenye utendaji unaoendana na hii simu ila redmi inakuja na kioo cha amoled, kamera nne na pia uwezo wa kuzuia vumbi na maji ya kiwango cha kunyunyuzia

Wakati redmi note 11 bei yake ni shilingi laki nne

Pia mshindani mwingine ni Simu ya Tecno Pova 3

Neno la Mwisho

Infinix hot 30 ni toleo zuri kwa walio na bajeti ndogo

App karibu zote zitafanya kazi, na anayetafuta simu inayokaa  na chaji masaa mengi hii simu itamfaa

Ila kama unahitaji vitu vya ziada kwa bajeti hii washindani wake wanaweza kuwa mbadala

Maoni 28 kuhusu “Bei ya infinix hot 30 na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram