SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ujio wa Simu mpya za Tecno Camon 40

Simu Mpya

Sihaba Mikole

March 15, 2025

Huu mwezi wa tatu 2025 tecno imetangaza ujio wa matoleo mapya ya Tecno Camon 40

Simu hizo ni

  1. Tecno Camon 40
  2. Tecno Camon 40 Pro 5G
  3. Tecno Camon Pro
  4. Tecno Camon 40 Premier

Kwenye hii post utafahamu baadhi ya sifa za muhimu za kila tecno

Na tecno kali zaidi kati ya zilizotangazwa

Tuzame kiundani na kwa kifupi sana.

Tecno Camon 40

Tecno Camon 40 inakuja na mfumo endeshi wa Android 15

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu inatumia processor ya Mediatek Helio G100 Ultimate

camon 40

Inakuja na memori ya GB 128 na GB 256 na RAM ya GB 8 ama 12

Betri yake kubwa ina mAh 5200

Pia ina kamera mbili kubwa ikiwa na megapixel 50

Tecno Camon 40 Pro 5G

Kioo cha Tecno Camon 40 Pro 5G kina refresh rate ya 144hz ambazo huwa ni smooth

Hii ni tecno iliyowekwa waterproof aina ya IP68 ambayo inaashilia maji hayatoingia kwenye simu ikizama kwenye kina ch mita 2

camon 40 pro 5g

Upande wa kamera, zipo kamera mbili moja ya 8MP na nyingine ya 50MP

Ukubwa wa memori ni GB 256 ila RAM unaweza pata ya GB 8 na GB 12

Kasi yake ya kuchaji ni 45W na betri ukubwa wake ni 5200mAh

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu ya utumiaji wa chip ya Dimensity 7300

Tecno Camon 40 Pro

Tecno Camon 40 Pro ni simu ya daraja la kati

Utendaji wake ni wa wastani kwani processor yake ni Helio G100 Ultimate

Kioo chake ni cha amoled chenye refresh rate ya 120Hz

camon 40 pro

Kasi yake ya kuchaji ni 45W na betri yake ina 5200mAh

Ukubwa wa memori ni wa aina moja ambayo ni GB 256 NA RAM ya GB 8

Ina kamera mbili pekee ambapo kamera kubwa imewezeshwa OIS

OIS hufanya kamera kutulia wakati ukiwa unarekodi video huku unatembea

Tecno Camon 40 Premier

Tecno Camon 40 Premier ndio tecno bora zaidi kati ya zilizotangazwa

Ina kamera tatu na zote ukubwa wake ni 50MP

Kamera ya Periscope Telephoto inasapoti ya optical zoom inayoweza ku-zoom mara tatu

Chaji yake inapeleka umeme wa wati 70 na betri lake lina ukubwa wa 5100mAh

Kioo chake ni cha LTPO AMOLED chenye refresh rate ya 144Hz

Na yenyewe ina waterproof ya IP68

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

tecno camon 40 pro thumb

Bei ya Tecno Camon 40 Pro na Sifa zake za muhimu mpya

Hapa utaenda kufahamu bei halisi ya Tecno mpya ya 2025 Tecno hiyo ni Tecno Camon 40 Pro ambayo imezinduliwa mwezi wa tatu Camon 40 Pro inafanana kiasi flani na Camon […]

samsungA56

Bei ya Samsung Galaxy A56 na sifa zake muhimu

Hii ni posti yenye maelezo ya kina kuhusu bei ya Samsung Galaxy A56 na sifa zake Utafahamu bei yake kulingana na ukubwa wa memori Na pia utofauti uliopo kati ya […]

xiaomi15ultra

Simu mpya za Xiaomi(Redmi) 2025 na bei zake

Hii ni orodha ya simu mpya za redmi na Xiaomi ambazo zimetoka mwanzoni mwa 2025 na mwishoni mwa 2024 Simu zilizoorodheshwa zipo za bei kubwa na bei ndogo Hivyo basi […]

samsungs25thumb

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na sifa zake muhimu

Hii ni post inayoenda kukuonyesha kinaga ubaga juu ya ubora mkubwa wa simu mpya ya Samsung Galaxy S25 Ultra Samsung Galaxy S25 Ultra imeingia rasmi sokoni mnamo mwezi februari 2025 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company