SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora wa simu mpya ya Oppo K10(na bei yake)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

April 2, 2022

Niliposikia toleao jipya la Oppo k10 nikajua itakuwa ina sifa lukuki

Lakini kumbe simu mpya ya oppo k10 ina sifa chache zinazofutia na kushawishi

Kiuhalisia oppo inakuja na chaji yenye spidi kubwa

Display angavu juani

Na uwezo wa kuzuia vumbi kupenya

Ubora mwingine ni wa kawaida kama inavyoonekana kwenye chati za sifa.

Sifa za OPPO K10

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 680 4G
  • Core Zenye nguvu(2) -4×2.4 GHz Kryo 265 Gold
  • Core Za kawaida(6) –  4×1.9 GHz Kryo 265 Silver
  • GPU-Adreno 610
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 11
  • ColorOS 11.1
Memori UFS 2.2, 128GB na RAM 8GB, 6GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(macro)
  3. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.59inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 462,178.58/=

Upi ni ubora wa simu mpya ya oppo k10?

Ukitaka kujua ubora wa oppo K10 tazama kasi yake ya ujazaji wa betri.

Inachukua dakika chache sana simu kujaa

Oppo k10 ina kioo chepesi pale unapotachi.

Kamera yake kuu ina megapixel kubwa apperture ya kamera inapitisha mwanga mwingi

Simu inatumia mifumo ya memori yenye kasi kubwa kusoma na kuandika data

Swali…

Vipi kuhu ubora wa network na chipset.

Fuatilia ubora sifa zingine za oppo k10

Network

Simu mpya ya oppo k10 haina mtandao wa 5G

Na 4g ya simu ina bands chache.

Simu inaweza kudownload faili kwa kasi inayofikia 390Mbps

Kwa sababu aina ya 4G ililyopo kwenye simu ni LTE Cat 13

Kwa Tanzania, 4G ya Halotel na Airtel hazitoshika kwenye hii simu.

Kwa sababu haina bands za 7 na 28

Ubora wa kioo cha oppo K10

Kioo cha oppo a96 ni cha aina ya IPS LCD.

Japokuwa IPS LCD huonyesha rangi chache, lakini resolution yake ni kubwa

Ukubwa wa resolution ya 1080 x 2412 pixels unafanya display ya K10 kuonesha vitu vizuri

Uangavu wa kioo unafika 600nits

Kiwango cha 600nits unaipa screen mwanga wa kuonesha vitu kwa uzuri juani

Kioo cha hii simu ni chepesi ukiwa unaperuzi namba na majina ya simu.

Uwepesi wake unachangiwa na refresh kubwa ya 90Hz

Nguvu ya processor Snapdragon 680 4G

Simu ya oppo k10 inatumia processor ya simu ya snapdragon 680 4g

Snapdragon 680 4g ina nguvu za wastani

Core kubwa zina kasi inayofikia 2.4GHz

Na core ndogo zina kasi 1.9GHz

Kinachosababisha processor kuwa na nguvu ya wastani ni aina ya muundo iliyo nayo.

Kwani snapdragon 680 4g inatumia Kryo 265.

Tumeeleze uwezo wa snapdragon 680 4g kupitia ukurusa wa Oppo A96

Uwezo wa betri na chaji

Oppo k10 ni simu inayopaswa kukaa na chaji muda mrefu.

Ina betri kubwa lenye ujazo wa 5000mAh.

Simu nyingi za 5000mAh zinaisha chaji baada ya 13 na kuendelea simu ikiwa inatumia intaneti masaa yote

Oppo k1o inakuja fast chaji.

Umeme wa chaji ya oppo unafikia wati 33

Kwa mujibu wa oppo kiasi hiki hujaza simu kwa 50% ndani ya dakika 26

Ukubwa na aina ya memori

Oppo hii mpya inatumia memori za UFS 2.2

Kasi ya kusafirisha data huwa ni kubwa

Kuna aina mbili za oppo k10 upande wa memori

  1. 128GB na 6GB
  2. 128GB na 8GB

Ukubwa wa memori huu unaweza kuifadhi mafaili na app nyingi

Uimara wa bodi ya oppo K10

Bodi ya oppo k10 imetengenezwa kwa plastiki

Upande wa nyuma na fremu kote ni plastiki

Kwenye screen ndio kuna kioo lakini sio cha gorilla.

Bodi za plastiki si imara sana kwenye kuzuia michubuko ya rangi

Utahitaji kava na screen protector

Hii simu nzito kutokana na kuwa na uzito wa gramu 189

Ina viwango IP vinavyoonyesha uwezo wa simu kuzuia vumbi

Ubora wa kamera

Kamera za oppo k10 zipo tatu.

Simu haina kamera ya ultrawide na telephoto.

Hivyo kuzoom kunategemea app ya camera.

Kamera yake ina apperture ya f/1.8

Ni aina ya apperture inayopitisha mwanga wa kutosha

Ubora wa video

Oppo k10 inaweza kurekodi video za aina moja.

Video za full hd(1080p)

Na inarekodi video kwa spidi ndogo ya 30fps

Hata selfie kamera inarekodi aina moja tu ya video

Ubora wa Software

Simu mpya ya oppo k10 ni simu ya android 11 yenye software ya ColorOs 11.1

Kitu kimoja kinachovutia kwenye ColorOs 11.1 ni uwezo wa kuunganisha simu na kompyuta

Hautohitaji app ya ziada kuhamisha vitu kutoka kwenye simu kwenda kwenye kompyuta

App ya music ya colorOs inakupa studio ndogo ndani ya simu.

Inakuwezesha kuhariri rington kwa namna upendavyo

Hii pia inapunguza gharama za kutumia app ya ziada kuedit miziki

Android 11 ina vitu vingi vizuri.

Lakini kuna vitu vipya kama color extraction vilivyopo kwenye android 12

Bei ya oppo K10 Tanzania

Bei ya oppo k10 inafikia shilingi 463,000/= za Tanzania

Bei yake inaoneka ni nafuu.

Lakini kwa n bei hii unapata simu nzuri ya Vivo T1 5G

Vivo T1 5G ina chip yenye nguvu kuliko hii

Yapi Madhaifu ya oppo K10

Kamera za oppo hazitumii teknolojia bora zaidi za kurenga aina ya dual pixel pdaf

Simu haina kamera ya ultrawide kwa ajili ya kupiga picha eneo pana

Processor yake haina nguvu kubwa kiutendaji.

Oppo k10 inatumia bodi za plastiki na sio kioo.

Simu haina kioo cha gorilla glass ambavyo huwa ni vigumu kuchunika na kupasuka.

Teknolojia ya IPS LCD nyakati zake zinaisha.

IPS LCD inapata shida kuonyesha wa rangi nyeusi halisi.

Wakati vioo vya amoled huonesha vizuri.

Network yake ya 4G ina bands chache sana

Simu inakuja na android 11 wakati simu mpya nyingi zina Android 12

Neno la Mwisho

Ukitaka simu inayokaa na chaji muda mrefu oppo k10 ni chaguo sahihi

Kwa mtu ambaye utendaji si kipaumbele hana haja ya kuangalia uwezo wa chip

Lakini kwa mpenzi wa kamera nzuri anapaswa atazame machaguo mengine zaidi.

Kwa bahati mbaya,

Simu zenye kamera nzuri huuzwa bei ghari

Hivyo mnunuaji analazimika kuongeza bajeti

Vinginevyo utapata simu ya uwezo wa kawaida

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram