SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Nzuri za iPhone na Bei Zake 2022

Brand

Sihaba Mikole

February 19, 2022

Jibu jepesi, simu za iphone zote ni nzuri.

Kwa nin?

Apple imejikita zaidi kuunda simu za gharama na hadhi ya juu

Hivyo wanajitahidi kwa kila namna kutengeneza smartphone yenye vitu vingi vizuri.

Ubora wa simu za iphone unatofautiana.

Tangu 2018 mpaka 2022 kuna matolea zaidi ya 11 ya iphone ambayo bado yapo sokoni pia.

Kwa wakati uliopo si kila simu ya iphone inafaa.

Hapa kuna orodha ya simu nzuri za iphone ambazo zinaweza kushindana na matoleo ya simu kutoka brand zingine za mwaka 2022.

Hizi ni iPhone ambazo zinapokea update za IOS kila mara kwa maana zinakubali apps zote.

Hizi ni baadhi.

Ni vizuri kuelewa ubora wa kila iphone kwa kuangazia sifa za simu husika.

iPhone 11

Simu ya iphone 11 inatumia processor yenye uwezo mkubwa kiutendaji aina ya Apple Bionic A13.

Procesor ya bionic A13 ina modem inayosapoti mtandao wa 4g hivyo simu haina 5g.

Bionic A13 inaweza kufanya kazi kubwa kuliko processor mpya zenye 5G ambazo zimetoka 2020-2021.

Processor ya Dimensity 810 inazidiwa zaidi ya mara na Bionic A13.

Hii inamaanisha iPhone ya mwaka 2019 inaizidi mbali Redmi note 11(china) ya mwaka 2021

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A13 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.65 GHz Lightning
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Thunder
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Liquid Retina IPS LCD
Softawre
  • iOS 13
Memori NVMe, 64GB,128GB,256GB na RAM 4GB
Kamera Kamera mbili

  1. 12MP, dual pixel PDAF(main)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12MP(selfie camera)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 3110mAh-Li-Ion
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 1,039,500/=

Kioo chake sio cha Super Retina Oled ambacho kinaonyesha vitu kwa uharisia kuliko IPS LCD.

IPS LCD za apple hufahamika kama Liquid Retina.

Simu hii inatumia iOS 13 ila inaweza kupokea iOS 15.3 ambayo ni mpya.

Mfumo wake wa memori ni tofauti na mifumo wa UFS unaotumiwa na simu za android.

NVMe ni mfumo unaotumika kwenye iPhone una kasi kubwa ya kuhifadhi vitu kuliko UFS.

Kuna aina tatu za iphone 11 upande wa memori kama jedwari linavyoonesha.

Betri yake aina ya Li-Ion ni dogo na mfumo wa chaji wake 18W unajaza betri kwa haraka.

Simu si ndefu ni fupi upande wa kimo.

Simu ina kamera mbili upande wa nyuma, zote zina megapixel 12.

Mfumo wa kamera una OIS na dual pixel PDAF.

OIS hutuliza video wakati ikichukuliwa huku mchukuaji video akiwa anatembea.

Dual pixel PDAF hufanya kamera kurenga kitu kinachopigwa kwa usahihi hivyo kutokea vizuri

Pamoja na kuwa kamera zake zinakosa optical zoom bado iphone ina kamera nzuri.

Kamera ambazo zinaweza kurekodi video za 4K

iPhone 11 Pro

Simu ya iphone 11 pro ni toleo moja na iphone 11.

Utofauti wa simu hizi mbili upo katika pande zifuatazao.

  • Kimo
  • Ujazo wa betri
  • Kioo(Display)
  • Memori
  • Bei
Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A13 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.65 GHz Lightning
  • Core Za kawaida(4) –  4×1.8 GHz Thunder
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • IOS 13
Memori NVMe, 64GB,256GB,512GB na RAM 4GB
Kamera Kamera TATU

  1. 12MP,PDAF(main), Dual pixel
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
  4. 12MP(selfie kamera)
Muundo Urefu-5.8inchi
Chaji na Betri
  • 3046mAh-Li-Ion
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 1,386,000/=

iPhone 11 ni ndefu kuliko iPhone 11 pro kwa sababu pro kimo chake inchi 5.8

iPhone 11 pro ina kamera iliyoongezeka ambayo ni telephoto yenye kupiga vitu ambavyo vipo mbali kiasi.

Telephoto ya iphone 11 pro inatumia optical zoom kukuza kitu kilichopo mbali.

Ila zoom yake ni ndogo, inakuza kitu mara mbili.

Kioo chake ni cha OLED, Apple wanakibrand kama super retina XR OLED.

Kina resolution kubwa na ni angavu hata ukiwa unaitumia kwenye jua, screen itaonyesha vitu vizuri.

Upande wa memori upo sawa na iphone 11 ila kuna iphone 12 pro ambayo ina ukubwa wa 512GB.

Betri yake ni dogo hivyo umeme wa wati 18 unaweza kujaza betri hili mapema.

Ukaaji wa betri wa hii simu si wa kuridhisha sana.

Betri yake inadumu kwa masaa 13 simu ikiwa inatumia intaneti.

Kwenye majaribio ya betri ya gsmarena iphone 12 pro inakaa na chaji masaa 17 ukiwa unaongea

iPhone 11 Pro Max

Simu ya iPhone 11 pro max ni ndefu kuliko iphone 11 na iphone 11 pro.

iPhone 11 pro inafana vitu vingi na simu ya iPhone 11 Pro Max.

Tofauti kubwa ipo tu upande wa betri.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • Apple A13 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.65 GHz Lightning
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Thunder
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • IOS 13
Memori 64GB,256GB,512GB na RAM 4GB
Kamera Kamera TATU

  1. 12MP,PDAF(main), Dual pixel
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
  4. 12MP(selfie kamera)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 3969mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 1,476,090/=

Betri yake na inakaa na chaji muda mrefu kuliko iphone 11 zingine.

Kmarea zipo nne na iliyoongezeka ni ya Ultrawide ambayo hupiga eneo pana.

iPhone 12

Mwaka 2020 apple walizindua iphone toleo la 12 moja wapo ni iPhone 12.

Simu ya iphone 12 inatumia processor ya Apple A14 Bionic.

Apple wanadai A14 uwezo wake umeongezeka kwa 40% ukilinganisha na processor zilizotangulia.

App kama GeekBench 5 zinazopima uwezo wa chip zinaonyesha Bionic A14 kuwa na nguvu kubwa kiutendaji.

Kwa maana hiyo app zinazotumia nguvu kubwa zinafunguka kwa wepesi na haraka bila kukwama.

Processor iliyopo kwenye iphone 12 inakubali aina zote tatu za 5G.

Aina tatu za 5G ni mmWave, Mid Band na Low Band 5G.

Matoleo ya iPhone 12 yanashindana na samsung matoleo ya S20.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A14 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.1 GHz Firestorm
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Icestorm
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • IOS 14.1
Memori NVMe, 64GB,128GB,256GB na RAM 4GB
Kamera Kamera mbili

  1. 12MP,PDAF(main)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12MP(selfie camera)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 2815mAh-Li-Ion
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 1,386,000/=

Simu ina iOS 14.1 lakini inakubwali kuwekwa iOS 15.3

Kioo kilichopo cha OLED kimeboreshwa upande wa uangavu tofauti na iPhone 11.

Upande wa kamera zipo kamera mbili ambazo zinarenga na kupiga picha vizuri.

Kubwa kamera kubwa inapitisha mwanga wa kutosha na zote kamera kuu ina OIS na dual pixel PDAF.

iPhone 12 ni ndefu kiasi kwani ina kimo cha 6.1

Betri yake ni ndogo la 2815mAh.

Mfumo endeshi wa iOS huwa una matumizi mazuri ya umeme hivyo betri yake inaweza kukaa na chaji kwa masaa 12 ikiwa kwenye intaneti.

Udogo wa betri unachangia umeme wa chaji wa 18W kujaza betri kwa haraka.

iPhone 12 zipo za aina, kuna za 64GB, 128GB na 256GB.

Kitu kimoja ambacho karibu simu zote za iPhone inacho ni IP68.

IP68 huonyesha uimara wa simu kuzuia maji kupenya ndani simu.

Ukiidumbukiza iphone 12 kwenye maji ya kina cha mita 6 maji hayatopenya ndani ya simu kwa muda wa nusu saa.

https://www.youtube.com/watch?v=Lv1kofMtpFs

iPhone 12 Pro

Simu ya iPhone 12 Pro pia inatumia processor Apple Bionic A14.

Tofauti iliyopo kati ya iPhone 12 Pro na iphone 12 ni upande wa kamera.

Vitu vingine vinafanana.

iPhone 12 Pro ina kamera nne.

Kamera mbili zilizoongezeka ni telephoto na TOF 3D LiDAR

Kirefu cha Light Detection and Ranging.

Ni kamera ambayo inatoa miyale ya mwanga kuscan vitu vinavyopigwa picha.

LiDAR hutumika sana kwenye Augmented Reality.

Augmented Reality ni kitendo cha kuweka vitu kwenye picha au video ambayo havikuwepo.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A14 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.1 GHz Firestorm
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Icestorm
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • IOS 14.1
Memori NVMe, 64GB,128GB,256GB,512GB na RAM 6GB
Kamera Kamera nne

  1. 12MP,PDAF(main), Dual pixel
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
  4. TOF 3D LiDAR scanner (depth)
  5. 12MP(selfie kamera), SL 3D(Biometric sensor)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 2815mAh-Li-Ion
  • Chaji-20W
Bei ya simu(TSH) 1,963,500/=

iPhone 12 pro zipo za aina tatu ambazo ni 64GB, 128GB na 256GB

iPhone 12 Pro Max

Simu ya iPhone 12 Pro max ni ndefu kuliko iphone 12 na iphone 12 pro.

Pia iPhone 12 Pro max ram yake ni kubwa.

Pia iphone 12 pro max ina betri kubwa na chaji yake inapeleka umeme mwingi kiasi wa 22W.

Sifa zingine zipo sawa.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A14 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.1 GHz Firestorm
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Icestorm
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • IOS 14.1
Memori NVMe, 64GB,128GB,256GB,512GB na RAM 6GB
Kamera Kamera TATU

  1. 12MP,PDAF(main), Dual pixel
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
  4. TOF 3D LiDAR scanner (depth)
  5. 12MP(selfie kamera), SL 3D(Biometric sensor)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 3687mAh-Li-Ion
  • Chaji-22W
Bei ya simu(TSH) 2,286,900/=

iPhone 13

Matoleo ya iPhone 13 yazinduliwa mwaka 2021 yakiwa yanatumia mfumo endeshi na processor mpya.

Processor yenye uwezo mkubwa kuliko processor yoyote ya simu kabla ya ujio wa processor ya Snapdragon 8 gen 1.

Apple A15 Bionic ina modem ambayo inasapoti mtandao wa 5G.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.22 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz  Blizzard
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED,
Softawre
  • iOS 15
Memori NVMe,

128GB,256GB,512GB

na RAM 4GB

Kamera Kamera mbili

  1. 12MP,PDAF(main), Dual pixel
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(selfie kamera), SL 3D(Biometric sensor)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 3240mAh-Li-Ion
  • Chaji-23W
Bei ya simu(TSH) 2,217,600/=

Apple 13 ina kamera mbili upande wa nyuma.

Kamera kuu inayo OIS na dual pixel PDAF ambazo hufanya video na picha kupigwa kwa ubora.

Betri lake lina ukubwa 3240mAh na mfumo wake wa chaji unapeleka umeme wa 23Wati.

Hivyo betri hili dogo linaweza kujaa kwa haraka.

Matoleo ya iPhone 13 yanasifika kwa ukaaji wa chaji.

Simu ya iPhone 13 inauwezo wa kuzuia maji kupenya endapo ikidumbukia kwenye maji ya kina cha mita 6 kutokana na kuwa IP68.

Bodi ya iphone 13 upande wa nyuma na mbele imeundwa kwa glasi ya gorilla ambayo huwa ni ngumu kuchunika na kupasuka.

Mfumo wake wa memori una kasi na iphone 13 zipo za aina tatu kama jedwali linavyoonekana upande wa memori.

Upande wa ram simu inatumia RAM ya 4GB.

iPhone 13 Pro

Simu ya iphone 13 pro ina kamera nne.

Display iliyopo kwneye hii simu ni sawa na ile iliyopo kwenye iPhone 13 ambayo ni OLED.

Kamera zilizoongezeka ni Ultrawide na LiDAR.

iPhone 13 pro inatumia RAM yenye ukubwa wa 6GB

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.22 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz  Blizzard
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • iOS 15
Memori NVMe , 128GB, 256GB,512GB, 1TB na RAM 6GB
Kamera Kamera nne

  1. 12MP,dual pixel PDAF(main),
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
  4. TOF 3D LiDar Scanner(depth)
  5. 12MP(selfie camera),SL 3D(biometric sensor)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 3095mAh-Li-Ion
  • Chaji-23W
Bei ya simu(TSH) 2,310,000/=

Betri yake imepungua ujazo tofauti na mtangulizi wake.

iPhone 13 pro zipo za matoleo manne(Kuna yenye memori ya 1T yaani 1000gb)

iPhone 13 Pro Max

Simu ya iphone 13 pro max ina fast chaji inayopeleka umeme mwingi wa wati 27.

Hivyo betri lake kubwa la 4352mAh linajaa ndani ya muda mfupi.

Ni simu inayokaa sana na chaji ukilinganisha na samsung s21 ultra.

iPhone 13 pro max ni ndefu kuliko iphone 13 pro na iphone 13.

Ukizitazama sifa za simu ya iphone 13 pro max nyingi zinafanana na iphone 13 pro.

Kila sifa iliyopo kwenye iphone 13 ipo kwenye iphone 13 pro na iphone 13 pro max

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.22 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz  Blizzard
  • GPU-Apple GPU(5-core)
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • iOS 15
Memori NVMe,

128GB,256GB,512GB,

1TB na RAM 6GB

Kamera Kamera nne

  1. 12MP,dual pixel PDAF(main),
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
  4. TOF 3D LiDar Scanner(depth)
  5. 12MP(selfie camera),SL 3D(biometric sensor)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4352mAh-Li-Po
  • Chaji-27W
Bei ya simu(TSH) 2,538,690/=

iPhone XR

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A12 Bionic 
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.5 GHz Vortex
  • Core Za kawaida(6) – 4×1.6 GHz Tempest
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Liquid Retina IPS LCD
Softawre
  • iOS 12
Memori NVMe,64,128GB,256GBna RAM 3GB
Kamera Kamera MOJA

  1. 12MP,PDAF(main)
  2. 7MP(SELFIE camera), SL 3D(biometric sensor)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 2942mAh-Li-Po
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 713,790/=

Wazo moja kuhusu “Simu Nzuri za iPhone na Bei Zake 2022

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram