SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Google Pixel 10 na bei zake (ubora na sifa)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

August 31, 2025

Mbabe wa kamera upande wa simu ametoa matoleo mapya

Si mwingine bali ni Google Pixel 10

Google Pixel 10 unaweza kuiona kuwa haina tofauti na Pixel 9

Lakini haipo hivyo google pixel 10 ya 2025 imeboreshwa hasa upande wa utendaji

Hiki ni kipengele muhimu ambacho simu za Samsung na iPhone zimekuwa zikiipita Google mara nyingi

Hizi ndio simu tunazoenda kutazama

  • Google Pixel 10
  • Google Pixel 10 Pro
  • Google Pixel 10 Pro XL
  • Google Pixel 10 Pro Fold

Google Pixel 10

Google Pixel 10 ni simu ya kimo kifupi cha inchi 6.3

Bei yake ni shilingi milion 3.5 kwa hapa Tanzania

Kimo hiki kinafiti vizuri kwenye mkono hivyo ni rahisi kushika

Kioo chake ni cha OLED chenye refresh rate ya 120Hz na HDR10+

google pixel 10

Teknolojia ya hdr10+ inaongeza kwenye skrini kina kikubwa cha rangi na hivyo kioo huonyesha vitu kwa ustadi

Betri ina mAh 4970 sio kubwa ukilinganisha na matoleo ya simu nyingi siku hizi

Inakuja na kamera tatu pamoja na RAM ya GB 8 na memori ya GB 128 au 256

Google Pixel 10 Pro

Bei ya Google Pixel 10 Pro ni shilingi milioni 4

Kimo chake ni inchi 6.3 kama ilivyo simu ya kwanza

Kioo chake kimeboreshwa zaidi kwa kuwekwa LTPO OLED

-google pixel 10 pro

Inakuja na processor iliyoboreshwa zaidi ya Tensor G5

Betri ina ukubwa wa 4870mAh na chaji ya wati 30

Inakuja na kamera tatu za ukubwa wa 50MP kwa 48MP

Google Pixel 10 Pro XL

Google Pixel 10 Pro bei yake ni shilingi milioni 5.7

Inakuja na RAM ya GB 16 na prosesa ya Tensor G5

Pia inakuja na kamera zipatazo tatu

google pixel 10 pro xl

Betri yake ina ukubwa wa 5200mAh na chaji ya wati 45

Kioo chake ni cha LTPO OLED chenye HDR10+

Inakuja na Android 16 na itapata maboresho kwa miaka 7 mfululizo

Google Pixel 10 Pro Fold

Google Pixel 10 Pro Fold ni simu ya kujikunja

Yaani unaweza itumia kama simu ya kawaida na ukiikunjua inakuwa tablet

Upana wake ukiikunjua ni inchi 8

Betri yake ina ukubwa wa mAh 5015

google pixel 10 fold

Na pia ina kamera tatu

Na inatumia kioo cha Foldable LTPO OLED

Bei yake ni shilingi milioni 5.7 kwa hapa Tanzania

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

pixel thumbnail

Simu za google pixel za bei rahisi zenye utendaji mzuri (2025)

Simu mpya za Google Pixel hupatikana kwa bei kubwa ambayo kwa Tanzania ni wachache wanayomudu Simu za google pixel hutengeneza simu za madaraja ya juu kama uonavyo iPhone Hivyo katika […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

huawei mate

Simu Bora 15 Duniani 2024 (na zitakazotamba 2025)

Kwa mwaka 2024, soko la simu janja yaani smartphone duniani lilitawaliwa na makampuni ya Apple, Samsung, Xiaomi, Vivo na Oppo Kwa hapa Afrika kampuni ya Samsung inaongoza kwa mauzo ikifuatiwa […]

pixel 9 pro fold

Simu Mpya za Google Pixel 2024 na bei zake

Kuna matoleo yapatayo manne ya simu mpya za google ambayo yametoka mwaka 2024 Matoleo yote yanatofoautiana kwa kiasi fulani kwenye muundo na baadhi ya vitu kama utakavyoona Hivyo, bei zake […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company