SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Oppo Yenye Kamera Nzuri na Ubora wa Picha

Brand

Sihaba Mikole

May 27, 2023

Kuna matoleo mengi ya simu za oppo zenye ubora tofauti tofauti

Zipo ambazo zina ubora wa kati, wa juu na wa chini

Katika hizo, nyingi zinajitahidi kuwa na kamera zinazotoa picha na video nzuri ila kuna toleo kinara

oppo find x6 pro

Kiufupi ni kuwa Oppo yenye kamera nzuri kwa sasa ni Oppo Find X6 Pro ambayo imetoka mwaka 2023 mwezi januari

Bei yake ni kubwa na inazidi milioni, kwenye hii post utaona ubora wa picha na aina ya kamera za Oppo Find X6 Pro

Idadi na Aina ya Kamera

Upande wa nyuma find x6 pro ina kamera zipatazo tatu (macho matatu) na upande wa mbele(selfie) kuna kamera moja

Simu ina kamera aina ya periscope telephoto maalumu kwa kuchukua vitu vilivyopo umbali mrefu kidogo na kamera

Kwa mfano kitu kipo mita 20 na unataka kitokee vizuri basi kamera ya telephoto ndio hustahili kufanya kazi hiyo

oppo find x6 pro kameras

Aina ya kamera iliyopo ni Ultrawide ambayo hutumika kupiga picha kwenye eneo pana

Kwa mfano upo uwanjani na unataka uwanja wote utokee kwenye picha, camera ya ultrawide itaifanya hiyo kazi

Na aina nyingine ya kamera ni kamera kuu ambayo ndio hutumika mara kwa mara, aina hii hujulikana kama wide

Kamera zote zinakuja zikiwa na megapixel 50

Ukitaka kujua kamera nzuri ya simu anagalia teknolojia zinazoambatana nazo hata kabla kuangalia muonekano wa picha wa hizo kamera

Teknolojia zilizopo kwenye kamera

Mfumo wa kamera za Oppo Find X6 Pro unakuja na vitu vingi vya uboreshaji wa kamera kati upigaji picha na kurekodi video

Hivi vinahusisha

Mult-directional PDAF, ni aina ya teknolojia inayosaidia kamera kurenga kitu moja kwa moja bila mpigaji kupoteza kukilenga anachotaka kukipiga picha

Zipo teknolojia za ulengaji nyingi ila kisasa zaidi ni hiii mult directional pdaf ambayo huchukua data nyingi ili iweze kukilenga na kukitambua kitu kinachopigwa picha

Iko fasta na inasaidia simu kupiga vizuri palipo na mwanga hafifu

Kitu kingine ni OIS, hii hutuliza kamera wakati ukirekodi video huku ukiwa unatembea

Ni kamera mbili ndizo zilizowekewa OIS kwenye hii simu

Pia kamera zake mbili zina Laser AF, inafanya kazi kama PDAF yaani kuisaidia kamera kukitambua kitu kinachopigwa picha ila laser af inatumika zaidi kwenye mwanga mdogo

Teknolojia zingine ni Dolby Vison, gyro Eis , optical zoom

Kutokana na uwepo wa hivyo vitu muhimu, oppo ina mfumo mzuri unaoweza piga picha nzuri kwenye mazingira tofauti

Ubora wa Picha Kwenye Mwanga Mwingi

Moja ya kitu ambacho hutokiona kwenye hii oppo ni noise(chenga chenga)

Kamera zinakusanya data za kutosha hivyo muonekano wa picha kiubora ni mkubwa

Tukianza na kamera kuu, inaonyesha rangi za vitu kwa usahihi wa kiwango cha juu

Hii inamaanisha kuwa kamera inaweka mlinganyo sahihi kwenye utofautishaji wa eneo lenye kivuli na lisilo na kivuli

oppo find x6 pro mchana

Vitu vinaonekana kwa uhalisia hakuna kuzidisha kwa muangaza ambao unaweza mfanya mtu kuonekana kwa kung’aa sana

Ukiizoom picha hii bado ubora wa muonekano wa picha haupungui

Ubora wa picha wa kamera ya Ultrawide na Telephoto

Kwenye mwanga mwingi bado hizi kamera zinatoa picha nzuri

Rangi za vitu zina usahihi na “dynamic range” inafanya kazi vizuri

Kwa maana balansi ya mwanga na vivuli kamera inafanya kwa usahihi

Mwanga mwingi hauthiri eneo lenye kivuli kidogo

oppo find x6 pro ultrawide

Ukitazama muonekano wa anga uhalisia ni wa kiwango cha juu kwenye mawingu meupe yanaonekana kama yalivyo

Ukiizoom hii picha unaweza usione kiwango cha noise kwa sababu kamera ina uwezo wa kukusanya data za kutosha

Upande wa ubora wa picha kwenye telephoto pia utendaji ni kuridhisha

Kumbuka kuwa telephoto ni maalumu kwa ajili ya kupiga kitu ambacho kipo mbali

Kwenye simu nyingi ambazo hazina hii kamera ubora wa picha unapungua ukiizoom kamera ili upige hiko kitu

Ila kwenye oppo ubora unabaki palepale hasa ukikuza mara tatu

oppo find x6 pro telephoto

Kama unavyoweza kuona kuwa hakuna upotevu wa pixel kama ilivyo kwenye digital zoom

Usahihi wa rangi za vitu ni wa kiwango cha kuridhisha

Na ukiikuza picha zaidi bado vitu vinaonekana na kiwango cha noise ni kidogo vilevile

Ubora wa Picha kwenye mwanga hafifu

Kwenye mwanga hafifu ndio eneo la muhimu zaidi kujua ubora wa kamera za simu

Simu zenye kamera nzuri zinapiga picha zinazoonyesha vitu kwa ustadi mkubwa kwenye mwanga mdogo

Utendaji wa kamera za oppo zote tatu ni mzuri

Kiwango cha chengachenga(noise) ni kidogo na kama una jicho la haraka unaweza usigundue

Chukulia mfano wa hii picha.

oppo find x6 pro low light

Kwenye eneo la kuria upande wa mti kuna mwanga mdogo sana lakini unaweza ukaona rangi ya majani ya mti

Utofautisha wa vivuli na mwangaza umejitahidi kwa kiasi kikubwa

Ukizoom eneo gorofa vitu vinaonekana japo kiwango noise unaweza ukakiona

Kamera za hii simu zinajitahidi nyakati za usiku kwa sababu ya uwepo Laser AF inayosaidia simu kurenga vizuri hata palipo na kiwango cha chini cha mwanga

oppo find x6 pro usiku

Ubora wa selfie kamera

Kwa mpenzi wa kujipiga picha kamera ya mbele ni kipaumbele kikubwa sana kuliko hata kamera za nyuma

Kamera ya selfie ya oppo find x6 pro haina mambo mengi sana kama ilivyo kwa selfie ya iphone 14 pro max

Hivyo ubora wake ni wa kawaida ila bado kiwango cha picha ni kizuri tena inaizidi Tecno Spark 10 Pro

oppo find x6 pro selfie camera

Kama uonavyo ni kuwa picha imechukuliwa kwenye mwanga mdogo

Ubora wa picha ni mzuri na pia kuna kiwango cha chenga chenga kwa mbali hasa kwa vitu ambavyo vipo mbalimbali

Hivyo kamera inajikita zaidi kupiga picha uso ukiwa karibu sana

Ubora video

Kamera za Oppo Find X6 Pro zinaweza kurekodi mpaka video za 4K

Na zina teknolojia ya utulizaji wa kamera pindi ukirekodi huku ukiwa unatembea

Teknolojia hufahamika gyro-EIS

Ni kweli inatuliza ila mitikisiko ipo kwa kiasi fulani bado anayerokidi atalazimika kutuliza mkono pindi akiwa anatembea

Video ya 4K inarekodi video ya ubora sana nyakati zenye mwanga wa kutosha

Nyakati za usiku noise(chengachenga) kwa mbali zinaweza kuonekana

Tazama hii screenshot toka kwenye video ya 4k kwa kiwango cha 30fps

oppo find x6 pro

Hata hivyo kamera inajitahidi kuonyesha rangi za vitu na kiza hakijaathiri muonekano wa sehemu zenye mwanga mwingi

Kila kitu kinaweza kuonekana kama kinavyoonekana kwenye mazingira halisi

Kamera za Ultrawide na Telephoto pia utendaji wake ni wa kiwango kizuri unaporekodi video

Ila kamera ya ultrawide haina OIS (Optical Image Stabilization) na hivyo basi kuliza mkono unaporekodi video kwa kutembea kunahitajika

Bei ya Oppo Find X6 Pro

Kama ilvyo ada simu yoyote yenye kamera kali sana bei yake huwa ni kubwa vilevile

Hivyo basi bei ya oppo find x6 pro ni zaidi ya shilingi milioni mbili za Tanzania

Kwa sasa hii simu inapatikana ndani ya mipaka ya china tu

Ila unaweza ukaagizia na ikakufikia ulipo

Hitimisho

Opoo Find X6 Pro ni moja ya simu bora kabisa duniani kwa sasa zinazoongoza kuwa na kamera nzuri

Inakupa uwezi wa kurekodi na kupiga picha vizuri iwe usiku ama mchana

Mfumo wake wa kamera unasaidia kutoa picha zenye ubora mzuri

Kwa mtu mwenye bajeti ya kutosha anaweza akaimiliki hii simu

Kumbuka ubora wake haupo kwenye kamera pekee yake na kwenye mambo mengine pia.

Maoni 4 kuhusu “Oppo Yenye Kamera Nzuri na Ubora wa Picha

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail oppo

Simu mpya 12 nzuri za Oppo na bei zake 2024

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka sasa 2024 tayari kampuni ya OPPO toka china wametoa simu zaidi ya 15 za madaraja mbalimbali Hapa utakutana na orodha ya simu mpya za […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram