SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

March 27, 2024

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024

Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa

Ndio maana bei ya Samsung Galaxy A35 kwa Tanzania inafika shilingi laki tisa na nusu kwa yenye GB 128

showacase

Na bei inaweza kuzidi hapo kutegemeana na mabadiliko mengine

Sasa swali la kujiuliza kwa nini bei yake inaonekana kuwa ni kubwa?

Sababu kubwa ni sifa zake hasa upande wa utendaji, kamera, kioo, software, uimara wa bodi na mengineyo

Fuatilia kufahamu namna zitakavyokufaa kwa matumizi yako

Sifa za Samsung Galaxy A35

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 1380
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.4 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G68 MP5
Display(Kioo) Super Amoled, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
  • One UI 6.1
Memori  256GB,128GB na RAM 8GB,6GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 950,000/=

Uwezo wa Network

Samsung Galaxy A35 inasapoti mpaka mtandao wa 5G

Na inasapoti aina zaote tatu za 5G ikiwemo masafa ya kati ambayo yanatumika na mitandao mingi hapa Tanzania

5G ina kasi kubwa japo kwa Tanzania usambaaji wake haujaenea meaneo mengi

Na kwa kiasi kikubwa inapatikana maeneo machache ya Dar es Salaam

Hata hivyo simu ina 4G pia aina ya LTE Cat 18 yenye kasi inayofika 3790Mbps

Ambayo ni kubwa ila usitarajie kupata kasi hii ya 4G kwa hapa nchini

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A35

Kioo cha Samsung Galaxy A35 ni cha super amoled chenye resolution ya 1080×2340 pixels

Kioo chake kina refresh rate ya 120Hz kitu kinacholeta muonekano wakati wa kuperuzi ama ukiwa unacheza gemu

Uzuri wa kioo hiki cha samsung ni dynamic, kwa maana kasi ya refresh rate itaongezeka kulingana na aina ya matumizi kwa wakati huo

display

Unajua kuwa refresh rate kubwa hutumia umeme mwingi hivyo betri inaweza isha haraka

Hivyo sio nyakati zote refresh rate ya 120Hz inaweza ikawa inahitajika

Pia kioo kina uangavu mkubwa hivyo utaweza kuitumia hata juani na ukawa unaona vitu vizuri

Nguvu ya processor Exynos 1380

Samsung Galaxy A35 inatumia chip yenye utendaji wa wastani ya Exynos 1380

Hii ni processor imeundwa na samsung wenyewe

Inaweza kucheza gemu nyingi bila kusababisha simu kupata joto jingi

processor

Haya ni maboresho makubwa kwani kipindi cha nyuma Exynos zilikuwa na changamoto ya kupata moto sana

Kwenye App inayopima nguvu za processor yaani Geekbench 6, Exynos 1380 ina alama 999

Ukitazama ni kuwa nguvu yake inaachwa mbali sana na Snapdragon 8 Gen 3 hata hivyo Exynos 1380 ni chip inayopiga kazi kubwa kwenye vitu vingi na unaweza usione tofauti

Uwezo wa betri na chaji

Betri yake ina ukubwa wa 5000mAh na chaji yake inasapoti kupeleka umeme wa wati 25

Hii simu inaweza kukaa na chaji kwa takribani masaa 12 ukiwa unaperuzi intaneti

Hivyo kwa matumizi ya kawaida simu inaweza kukaa na chaji hata siku nzima

chaji

Kwenye kasi ya kukaa na chaji hii simu inaweza kuchukua takribani dakaika 86 kujaa kwa asilimia 100 kutoka 0

Ni muda mdogo na pia unaweza kuitumia simu kwa masaa mengi

Ukubwa na aina ya memori

Kuna mtoleo ya aina mbili upande wa memori na RAM

Zipo Galaxy A35 za GB 128 na RAM ya GB 6 au GB 8

Na pia zipo zenye ukubwa wa GB 256 na RAM ya GB 8

Hizi memori zote zinahifadhi mafaili mengi na zinatosholeza kufungua vitu vingi kwa wakati mmoja bila kukwama

Uzuri ni kuwa hizi simu zinatumia memori aina ya UFS ambazo kasi yake ya kusafirisha data huwa kubwa

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A35

Bodi ya Samsung Galaxy A35 ni imara kwenye kuzuia maji kwani ina waterproof

Inakuja na viwango vya IP67 vinavyoashiria simu kutoingia maji kama ikizama kwenye kina cha mita moja kwa muda wa nusu

Kwa maana kama kama simu ikizama kwenye ndoo ya maji ukirudi utaikuta na ikiwa inafanya kazi

Galaxy A35 inakuja na skrini protekta ya kioo cha Gorilla Glass Victus+

Kiuzoefu ni kuwa Gorilla Glass Victus+ huwa ni kioo kigumu kupasuka ila huwa vinaweza kuchunika kirahisi ikigusana na coin(sarafu)

Hii ni kwa mujibu ya waliowahi tumia simu zilizoekewa hivi vioo

Kiujumla Samsung Galaxy A35 ni simu yenye bodi imara

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera zipatazo tatu na kamera kubwa ina megapixel 50

Simu inapiga picha nzuri katika nyakati zote yaani kwenye mwanga hafifu(usiku) na kwenye mwanga mwingi

Kamera zake zinajitahidi kwa kiasi kikubwa kutoa picha zenye rangi halisi

kamera

Hazizidishi uangavu unaofanya kinachopigwa picha kung’aa sana kuliko uhalisia

Kamera zina mfumo wa OIS unaotuliza video wakati ukirekodi huku ukiwa unatembea

Na cha kuvutia zaidi ni kuwa kamera yake inarekodi mpaka video za 4K ambazo zinakuwa na muonekano mzuri zaidi

Ubora wa Software

Samsung Galaxy A35 inatumia Android 14 na One UI 6

One UI 6 inakuja na mifumo mingi ya akili bandia, kwa mfano kwenye kuedit picha

One UI 6 inakupa uwezo wa kuindoa baadhi ya vitu vilivyotokea kwenye picha iwapo uvihitaji vioonekano

Kwa mfano umepiga picha baa bia zikaonekana na wewe unataka uondoe zile picha

Basi One UI 6 inakupa huo uwezo bila kuathiri ubora wa picha

Kitu cha kufurahisha ni kuwa hii simu itakuwa inapokea matoleo mapya ya Android kwa muda wa miaka minne

Yaani mmiliki wa hii simu atakuja kutumia mpaka Android 18 kitu kinachoipa thamani simu muda mrefu

Washindani wa Samsung Galaxy A35

Pamoja na uzuri wote wa hii simu, kuna kampuni za China ni tishio kwa samsung kwenye kipengele hiki

Simu kutoka china zinauzwa kwa bei ya chini hapa na huku zikiwa na ufanano mwingi kwenye vipengele mbalimbali

Mfano mzuri ni Redmi Note 13 Pro+, vitu vingi unavyoviona kwenye Galaxy A35 vinapatikana kwenye Redmi Note 13 Pro+ ya 2023

Haitoshi ni kuwa Redmi Note 13 Pro+ inakuja na chaji yenye kasi ya 12oW na kioo chenye teknoljia za ziada kama HDR10+ na simu ina water proof ya IP68

Lakini cha kufurahisha na kustajaabisha Redmi bei yake ni shilingi laki nane na nusu

Huu ni mfano mmoja kati ya mifano mingi, hivyo Samsung ana kazi ya ziada kupambana na simu kutoka China

Neno la Mwisho

Bei ya Samsung Galaxy A35  inaendana kwa kiasi kikubwa na sifa zake katika nyanja nyingi

Kwa mtumiaji wa simu ambaye anataka kununua toleo la Samsung Galaxy S20 used hana haja ya kufanya hivyo

Kwa Ubora wa Galaxy A35 unaizidi S20 ambayo kwa sasa ina miaka minne

Ila kama unataka kitu kizuri zaidi yapo matoleo yenye ubora zaidi ya hii kwa bei ya chini

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram