SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na bei ya simu ya redmi 9a (2022)

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 16, 2022

Simu ya redmi 9a ni simu ya daraja la mwisho iliyotoka mwaka 2020.

Japokuwa ni miaka miwili imepita ila inabaki kuwa moja ya simu nzuri ya bei rahisi kwa mwaka 2022

kioo cha redmi 9a

Ukichungulia sifa zake upande wa memori, betri na display utaona ina ubora wa kukidhi mahitaji ya mtumiaji wa kawaida wa simu

Bei ya redmi 9a ni chini ya laki tatu na inaendana kabisa kwa ubora na sifa zake

Bei ya Redmi 9A Tanzania

Bei ya redmi 9a yenye ukubwa wa GB 32 na ram ya GB 2 ni shilingi 280,000/= kwa maduka ya simu ya mitaa ya Kariakoo

Simu hii inauzwa bei kubwa kwa Tanzania

Kwa sababu bei halisi ya redmi 9a ya gb 32 ni shilingi 210,000/= aliexpress

Na redmi yenye ukubwa wa GB 64 na RAM ya GB 4, aliexpress inauzwa 242,000/=

Ukiwa na muda wa kutosha nunua simu aliexpress kuokoa pesa

Kama ilivyosemwa, bei inaendana na sifa zake na usitarajie maubwa kiubora

Sifa za Redmi 9A

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G25
  • Core KUBWA(4) – 4×2.0GHz Cortex A53
  • Core NDOGO(4) – 4×1.5GHz Cortex A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 10
  • MIUI 12
Memori eMMC 5.1, 128GB,64GB,32GB na RAM 4GB,2GB
Kamera Kamera moja

  1. 13MP,PDAF(wide)
Muundo Urefu-6.53inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
Bei ya simu(TSH) 242,000/=

Upi ubora wa simu ya Redmi 9A

Ubora wa redmi 9a upo kwenye ukubwa wa memori

Kwani inaruhsu kuhifadhi mafaili mengi kwenye simu

data za redmi 9a

Na betri yake inakaa na chaji muda mrefu

Ikizingatiwa utendaji wake hautumii umeme mwingi

Kioo chake kina resolution yenye unafuu ukilinganisha na simu nyingi zinazouzwa chini ya laki mbili na nusu

Uwezo wa Network

Redmi 9a inakubali aina zote za mtandao wa intaneti isipokuwa 5G

Aina ya 4G ya simu ni LTE Cat 7

Network ya LTE cat 7 inaweza kudownload faili kwa spidi inayofikia 300Mbps sawa na 37.5MBps

network ya redmi 9a

Ni spidi kubwa kama mtandao unakupa kasi ya namna hii

Ina network bands za 4G zipatazo 13

Simu inakubali intaneti za 4G za mitandao yote ya simu Tanzania

Ubora wa kioo cha Redmi 9A

Ni simu inayotumia kioo cha IPS LCD.

Kiubora, vioo vya IPS LCD huonyesha rangi chache ukilinganisha na vioo vya amoled

Hilo linasabababishwa na contrast ndogo

camera ya redmi 9a

Kiasi kinachofanya screen kutokuonyesha baadhi ya vitu kwa rangi halisi mfano rangi nyeusi

Uangavu wa kioo sio mkubwa kwani unafikia 460nits

Unaweza ukapata shida kuona vitu kwenye screen ukiitumia simu kwenye jua kali(ukiwa nje juani)

Nguvu ya processor Helio G25

Ubongo wa simu ya redmi 9a ni processor ya Helio G25

Ni chip ya daraja la mwisho

Ina core nane zilizogawanyika sehemu mbili.

Kiuhalisia core zote zina nguvu ndogo

processor ya simu ya redmi 9a

Kiasi cha kwamba inailazimu simu kucheza gemu kali kwenye resolution ya chini

Si kitu cha kuvutia kwa mpenzi wa magemu

Hii inasababishwa na kitendo cha core zote kuundwa kwa Cortex A53.

Kama umewahi pitia makala zetu nyingi, utakuwa unajua kuwa Cortex A53 ni core maalum kwa kazi ndogo ndogo

Jifunze: Jinsi ya kujua ubora wa processor za simu.

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya redmi 9a ni kubwa na ni aina ya Li-Po

Ukubwa wake ni 5000mAh.

Hii simu inaweza kukaa na chaji masaa mengi sana

Kwa sababu chip yake inatumia umeme kidogo mno

Na haina fast chaji

Hivyo basi itachukua masaa si chini ya matatu kujaza betri kwa 100%

Ukubwa na aina ya memori

Simu inatumia memori aina ya eMMC 5.1

Hii ni memori inayoifanya simu kuwa na kasi ndogo ya kuwasha simu kwa haraka na kufungua app kwa spidi.

Kwa sababu eMMC ina kasi ndogo ya kusafirisha data ukilinginasha na memori za UFS

Kuna redmi ya 32GB, 64GB, 128GB na ram 2GB, 3GB, 4GB na 6GB

Kadri memori inavyokuwa kubwa na bei yake inaongezeka

Uimara wa bodi ya Redmi 9A

Bodi yake sio imara na inaweza kupasuka kwa urahisi.

Hiyo inatokana na upande wa nyuma kuwa na plastiki

Na kwenye screen hakuna kioo cha gorilla

Kwa hiyo utahitaji kuweka protector na kava

Hivyo vitu viwili vitaimarisha ulinzi wa bodi ya simu na kuchunika kwa rangi

Simu ni ndefu na ni pana kiasi.

Na ina uzito unaozidi gramu 190

Ubora wa kamera

Simu ina kamera moja upande wa nyuma

Kamera inatumuia teknolojia ya ulengaji aina ya PDAF.

PDAF inafaa ukizingatia na aina ya simu na bei yake

Kamera yake ina HDR japo haiboreshi muonekano wa picha kwa ubora wa juu ukilinganisha na HDR10 au HDR10+

Kamera inaweza kurekodi video za full hd kwa spidi inayofikia 60fps

Ni simu chache sana za laki mbili zenye kamera ya ubora huu upande wa video

Ubora wa Software

Redmi 9a ni simu ya android 10 yenye mfumo wa MIUI 12.

Kuna matoleo mawili mapya ya android 11 na 12, lakini android 10 ina uzuri wake.

Android 10 ina app inayoweza kukuza sauti(sound amplifier)

Huu ni mfumo unaoweza kukata makelele na kukupa usikivu mzuri wa sauti

Kwenye app ya video ya android 10 kuna mfumo unaobadilisha sauti kuwa maandishi (Live Caption)

Video ikiwa inaplay maandishi yanatokea chini ya screen

Redmi 9a inakubali kuwekewa mfumo endeshi wa android 11

Yapi Madhaifu ya Redmi 9A

Simu ina kasoro nyingi kiujumla.

Lakini kumbuka simu za daraja la mwisho huwa ni za bei nafuu zanye ubora wa chini

Ukitazama display, kamera, network, bodi ya simu, spidi ya chaji, aina ya memori na uwezo wa processor na gpu

Utagundua kuwa ni simu ya kiwango cha chini sana

Neno la Mwisho

Kwa mtu mwenye bajeti ndogo kabisa ya simu hii ni simu yenye unafuu kiasi.

Na mtumiaji mpya wa smartphone atafurahia kuwa na hii simu.

Ila kama unataka kamera bora basi hii ni simu ya kuiepuka

Kwa sababu kamera nzuri inahitaji simu yenye utendaji wa juu

Kitu ambacho kinakosekana kwenye simu hii

Mshindani wa redmi 9a ni simu ya Samsung galaxy a13

Ila kiubora galaxy a13 ina utendaji wa juu zaidi na bei yake ni kubwa kiasi

Maoni 3 kuhusu “Ubora na bei ya simu ya redmi 9a (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram