Samsung wamezindua simu mpya ya Samsung Galaxy S26 Ultra
Imekuja na upekee fulani lakini hauleti utofauti mkubwa sana na Samsung GalaxyS25 Ultra
Kama ingekuwa ni mimi nisingeona haja ya kubadili simu
Ila kumbuka hayo mabadiliko madogo yana upekee wa kuvutia watu wengine
Tuitazame hii simu kiundani.
Bei ya Samsung Galaxy S26 Ultra
Kwa Tanzania Samsung Galaxy S26 Ultra inauzwa shilingi milioni 3.8
Hii ni bei ya Samsung Galaxy S26 Ultra ya GB 256
Kuna mpaka ya TB 1 na bei yake ni kubwa zaidi
Matoleo yote yana RAM za ukubwa wa GB 12
Na zinazumia mfumo wa memori zenye kasi zaidi wa UFS 4
Sifa za Samsung Galaxy S26 Ultra
| Sehemu Za Simu | Sifa za Simu |
|---|---|
| Network | 2g, 3g, 4g,5g |
| Processor(SoC) |
|
| Display(Kioo) | Dynamic LTPO AMOLED 2X, Refresh rate:120Hz |
| Softawre |
|
| Memori | , 256GB,512GB, 1TB na RAM 12GB |
| Kamera | Kamera NNE
|
| Muundo | Urefu-6.9inchi |
| Chaji na Betri |
|
| Bei ya simu(TSH) | 300,000/= |
Uwezo wa network
Samsung Galaxy S26 Ultra inasapoti aina zote za mitandao
Ukiwa mazingira yenye 5G utaweza kutumia mtandao huo wenye kasi
Na kwenye 4G itatumia aina hiyo ya mtandao
Ukiondoa aina ya mtandao, kwenye hii simu unaweza kutumia laini za eSIM
Hizi ni laini zinazokuwa ndani ya simu na uhitaji kuwa na laini ya plastiki
Ubora wa kioo
Ubora wa kioo ndio eneo lilofanyiwa maboresho makubwa zaidi
Maboresho haya yameleta faragha kwenye kioo
Na pia uwepo wa anti-reflective ambayo imeanza kuwekwa kwenye Samsung S25
Hii inasaidia kioo kuonyesha vitu vizuri pasipo kuludisha mwanga kuelekea kwenye macho
Kioo cha hii simu kinaweza kumzuia mtu wa pembeni asione unachokitazama kwenye simu
Tofauti na hapo mambo mengine yapo sawa
Nguvu ya utendaji
Utendaji wa simu umeongezeka zaidi kutokana na kutumia prosesa mpya
Prosesa hiyo ni Snapdragon 8 Gen 5
Kwenye app zinazopima uwezo wa utendaji zinaonyesha ongezeko la ufanisi zaidi
Hii prosesa ina utendaji mkubwa na inatumia kiasi kidogo cha umeme
Inaizidi hata prosesa za apple katika ufanisi wa utumiaji umeme
Qualcomm hawajaamua kuongeza uwezo wa kiutendaji zaidi bali wamelenga matumizi madogo ya nishati
Uimara wa bodi
Kama kawaida Galaxy S26 Ultra ina waterproof
Hii inaonyeshwa na uwepo wa cheti cha IP68
Ikiwa na maana simu haipitishi maji hata ikizama kwenye kina cha mita 1.5
Lakini kwa muda wa nusu saa
Samsung wamerudi kwenye bodi za Alumiam kutoka kwenye chuma aina Titanium
Ubora wa kamera
Hii simu ina kamera zipatazo nne
Kamera kubwa ikiwa na MP 200 kama tu mwaka uliopita
Hata ubora wa kamera ni jambo la kawida kwenye samsung za bei kubwa
KIujumla hii simu ina kamera nzuri kwenye upigaji picha na kurekodi video
Uwezo wa betri na chaji
Betri ya Samsung Galaxy S26 Ultra betri lake lina ukubwa wa 5000mAh
Ukiwa kwenye intaneti muda wote betri huchukua masaa 13
Ni tofauti na simu za China sasa hivi
Zinakuja na betri mno mfano ni Xiaomi 17 Pro Max
Hitimisho
Utofauti mdogo kati ya toleo hili na la mwaka jana unaweza ukamzuia mtu kuichukua hii simu
Lakini vitu vichache vipya vimeleta upekee mkubwa
Ubora wa skrini ni wa kiwango kikubwa hasa kwenye utunzaji wa faragha