SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu za Vivo na bei zake (2025-2026)

Miongozo

Sihaba Mikole

December 1, 2025

Hii ni orodha ya baadhi ya simu mbalimbali za vivo

Katika kundi hili kuna vivo za bei rahisi na vivo za bei kubwa

Kama hujui kampuni hii hutoa matoleo ya madaraja yote

Kwa hiyo zipo za ubora mkubwa sana na vivo za ubora wa kawaida

Orodha iliyopo inakurahisishia kuchagua vivo kali bila kujali aina ya vivo unayotaka kununua

Vivo Y500 Pro

Vivo Y500 Pro ni simu iliyotoka novemba 2025

Bei yake ni shilingi  laki saba (700,000) kwa hapa Tanzania

Bei yake inaakisi ubora katika maeneo matatu yafuatayo

1-vivo y500

Uimara wa bodi, skrini na utendaji

Upande wa bodi ina cheti cha IP68 waterproof ya kuzuia maji hata simu ikizama kwenye kina kirefu  cha mita 1.5

Utendaji wake pia ni mkubwa kutokana na kutumia prosesa ya Mediatek dimensity 7400

Vivo Y19s

Bei ya Vivo Y19s ni shilingi 330,000 kwa hapa Tanzania

Kadri bei ya simuinavyokuwa ndogo ndivyo vitu ubora hupungua

Hii simu ubora upo kwenye uwepo wa waterproof ya IP54

Na pia uwepo wa betri kubwa inayofikia 5500mAh

2-vivo y19s

Na kiasi fulani upande wa kamera sio mkubwa sana

Kiujumla hii simu ni nzuri zaidi kwa mtu mwenye matumizi ya kawaida ya kila siku

Kama ni mpenzi wa kamera, magemu na nguvu kubwa ya utendaji itakulazimu uiangalie vivo inayofuata

Vivo X300 Pro

Vivo X300 Pro ndio vivo bora zaidi kwa wakati huu na yenye ubopra katika vipengele karibu vyote

Hivyo bei yake sio ya kawaida kabisa maana inachuana na iPhone 17 Pro na Samsung Galaxy S25 Plus

Kwa Tanzania bei yake ni shilingi 4,200,000 (milioni nne na laki mbili)

3-vivo x300 pro

Haya ni baadhi ya maeneo yenye ubora mkubwa zaidi kwenye hii simu

Utendaji wake una nguvu sana kwa sababu ina chip ya Mediatek dimensity 9500

Kamera yake ni kali naweza sema kuliko hata simu zote kwa sasa

Betri yale ni kubwa na kasi ya kuchaji ni kubwa pia

Vivo V60e

Vivo V60e ni simu ya daraja la kati ila bei yake ni shilingi 850,000

Inatumia prosesa yenye nguvu ya wastani ya Mediatek dimensity 7360 Turbo

Hivyo vitu vingi vinafanyika kwa ufanisi bila kukwama kwama

4-vivo v60e

Ina waterproof ya IP68, hata ikizama kwa muda wa nusu saa maji hayataingia ndani ya simu

Pia betri yake ni kubwa ina mAh 6500 japokuwa ukaaji wa chaji bado unacheza kwenye masaa 12

Itakuwa ikipokea android mpya kwa muda wa miaka mitatu mfululizo

Vivo Y31

Vivo Y31 imetoka rasmi septemba 2025 na ni simu ya daraja la kati

Bei yake kwa Tanzania ni shilingi 54o,000

Ubora mkubwa wa hii simu upo kwneye utendaji

5-vivo y31

Hii inasababishwa na kutumia prosesa aina ya Snapdragon 4 Gen 2

Utendaji wake ni wa wastani ila inaweza kufanya mambo mengi bila shida

Maeneo mengine simu ina uwezo wa kawaida

Vivo Y400

Simu ya Vivo Y400 haina tofauti sana na Vivo Y31

Isipokuwa vivo y400 imewekewa mfumo wa memori zaidi kuliko vivo y31

Bei ya Vivo Y400 ni shilingi 750,000

Pia betri yake ina mAh 6000 ni ndogo kuliko Y31

vico y400

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu inatumia chip ya Snapdragon 4 Gen 2

Pia inakuja na kioo cha Amoled ambacho huwa na kina kikubwa cha rangi

Vivo Y31 Pro

Simu ya Vivo Y31 Pro inauzwa shilingi 550,000 kwa hapa Tanzania

Inatumia mfumo mwa meoroi wa UFS 3.1 ambao una kasi kubwa ya kuchaji

Pia chaji inapeleka umeme mpaka wa kiwango cha juu cha wati 90

7-vivo y31 pro

Upande wa memori, inatumia RAM ya GB 8

Vitu vingine simu inafanana tu na vivo y31

Vivo T4 Pro

Bei ya Vivo T4 Pro kwa Tanzania ni shilingi 850,000

Ukiona bei ya kiwango hiki jua simu ina vitu vizuri

Maeneo ambayo Vivo T4 Pro yana ubora mkubwa ni yafuatayo

8-vivo t4

Kwanza ni simu imara inayoweza kuzuia maji hata ikiwa imezama kwenye maji mengi

Hii inaonyeshwa na simu kuwa na cheti cha IP68 na IP69

Na skrini yake ina kikubwa cha rangi kutokana na uwepo wa teknolojia ya HDR10+

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

simu-bora-thumbnail

Simu bora duniani za ubora mkubwa (2025)

Hizi hapa ni orodha ya simu bora za bei  zinazoanzia milioni mbili kwenda mbele Ndizo simu janja zilizo kamili kwenye vipengele vingi Hivyo ni simu bora duniani kwa mwaka 2025 […]

bei ndogo

Simu za laki tatu zenye ubora wa kuridhisha kwa 2025

Iwapo unapanga kununua simu chini ya laki tatu au zisizozidi laki nne usitarajie kupata simu yenye ubora mkubwa Kwa maana usitarajie kamera kali na utendaji mkubwa Ila kwenye hii post […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

vivo_thumbnail

Bei ya Vivo Y19s na Sifa Zake Muhimu

Vivo Y19s ilitoka mnamo mwezi wa kumi mwaka 2024 Ni simu ya daraja hivyo gharama yake sio kubwa sana Kwa Tanzania, bei ya Vivo Y19s ni shilingi LAKI NNE Hii […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company