SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya iPhone 17 Pro Max na sifa zake muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

November 20, 2025

Ni takribani imefika miezi miwili mpaka tangu iphone 17 pro max

iPhone 17 Pro Max ni moja ya simu kali kabisa iliyopo sokoni kwa sasa

Bei ya iPhone 17 Pro Max kwa hapa Tanzania ni shilingi milioni 4

Hapa kuna swali!

iPhone 16 Pro Max bado ina ubora wa hali ya juu kushinda simu nyingi mpya sokoni

Kwa nini mtu ashawoshike kumiliki simu hii mpya?

Majibu ya sahihi ya hili swali utayapa baada kuelewa sifa kamili za iphone 17 pro max zilizopo hapa

Bei ya iPhone 17 Pro Max (GB 256)

iPhone yenye ukubwa wa GB 256 na RAM ya GB 12 utaipata kuanzia milioni nne

Bei yake kubwa haichagizwi na ukubwa wa memori pekee

Memori ni sehemu ndogo kati ya sehemu nyingi za simu

showcase

Japokuwa bei za hii simu hupanda kulingana na ukubwa wa memori

Maana ipo mpaka ya GB 2000 (2TB) ambayo bei yake ni tofauti na hii

Sifa za iPhone 17 Pro Max

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A19 Pro
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×4.26 GHz
  • Core Za kawaida(4) –  4xX.X GHz
  • GPU-Apple GPU (6-core graphics)
Display(Kioo) LTPO Super Retina XDR OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • iOS 26
Memori NMVe, 256GB,512GB,1TB,2TB na RAM 12GB
Kamera Kamera TATU

  1. 48MP,dual pixel PDAF(wide)
  2. 48MP(ultrawide)
  3. 48MP(Telephoto)
Muundo Urefu-6.9inchi
Chaji na Betri
  • 4823mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 4,000,000/=

Uwezo wa network

Hii simu inakubali aina zote za mtandao

Hivyo ukiwa eneo lenye 5G utapata kasi kubwa ya mtandao

Pia simu inasapoti laini za eSIM

Kwa matoleo ya USA iPhone 17 Pro Max inatumia laini za eSIM pekee

Iwapo utakuwa unatumia toleo la huko hakikisha mtandao unaotumia unakubali laini za eSIM

Ubora wa kioo

Kioo cha hii simu ni cha aina ya oled

Vioo vya oled huwa na kina kikubwa cha rangi

Hivyo huonekana kwa uangavu mkubwa tofauti na vioo ips lcd

Pia kioo kina mwitiko mkubwa unapo-scroll na kutachi

display

Hii inasababishwa na uwepo wa kitu kinaitwa refresh rate inayofika hadi 120Hz

Uwepo wa teknolojia za Dolby na HDR10 kunaongeza zaidi kina cha rangi

Kwa kifupi ubora wa kioo cha iPhone 17 Pro Max ni mkubwa

Nguvu ya processor ya Apple A19 Pro

Kwenye prosesa za simu kwa wakati huu hakuna inayoifikia Apple A19 Pro kiutendaji na kiufanisi

Kwenye app ya geekbench inayopima nguvu za prosesa apple a19 pro huonyesha uwezo wa kufanya kazi kubwa nyingi

Kwani ina alama zinazokaribia 4000

Ina uwezo wa kufungua kurasa za mtandaoni zipatazo 229 kwa sekunde bila kukwama

Gemu zote zinacheza bila kukwama na kwa utumiaji mdogo wa umeme

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya iphone 17 pro max ni ndogo kuliko samsung galaxy s25 ultra

Lakini iPhone 17 Pro Max inakaa sana na chaji kuliko samsung

Hii inasababishwa na ufanisi mkubwa wa prosesa ya Apple A19 Pro

Pia mfumo endeshi ulioundwa vizuri wa iOS

Kasi ya kuchaji sio kubwa kwani kiwango cha juu ni wati 25

Hata hivyo iPhone 17 Pro Max haiji na kichwa cha chaji

Uimara wa bodi

Bodi ya iPhone 17 Pro Max ina uimara mkubwa katika maeneo haya

Kwanza ina cheti cha IP68

Hiki cheti kinaashiria uwezo wa waterproof wa kuzuia maji simu ikizama kwenye kina cha mita 6

Simu haitodhurika kwa muda wa nusu saa

Pia ina skrini prorekta ya Ceramic Shield 2

bodi

Protekta hii huweza kuathiriwa mkwarizo iwapo kioo kikikutana na kisu chenye matirio ya chuma

Pia protekta ni imara zaidi pale simu inapodondoka

Hata hivyo umakini ni kitu cha muhimu

Haijalishi simu ipo na aina ipi ya protekta

Ubora wa kamera

Kamera za iPhone 17 Pro Max zinapiga picha nzuri kwenye mazingira yote

Hasa kwenye mazingira ya mwanga mwingi, picha huonyesha usahihi mkubwa wa rangi

Rangi halisi za kinachopigwa picha hutokea kama kilivyo kwa sehemu kubwa

Kwenye mazingira ya mwanga mdogo kuna kiasi fulani cha noise

Hasa kama kitu kipo mbali

Unaweza kuangalia hii picha kwenye linki

Ubora wa Software

Simu za iPhone mpya 2025 zinatumia mfumo endeshi wa iOS 26

Moja ya sifa kubwa ya iOS ni ufanisi wa matumizi ya chaji

Apple wameuunda mfumo wa iOS kutumia vizuri chaji

Ndio maana iphone hukaa na chaji muda mrefu japo betri lake ni dogo

Eneo ambalo apple wameonekana kutopiga hatua kubwa ni AI

Wapo nyuma ukilinganisha na simu za Samsung na Google Pixel

Washindani wa iPhone 17 Pro Max

Ukitazama simu bora duniani utaona vyuma vingine vyenye simu kali

Pitia hii linki simu bora duniani 2025

Kiujumla matoleo ya daraja la juu kutoka samsung, xiaomi, vivo, google, oneplus nk wanatoa simu nzuri

Hivyo washindani ni wengi sana kwenye kitengo chake

Neno la mwisho

Japo iPhone 17 Pro Max ina maboresho kadhaa ila sio maboresho yanayoleta tofauti kubwa na iPhone 16 Pro Max

Kwa mmiliki wa iPhone 16 Pro Max anaweza asihangaike kuipata iphone mpya

Bei yake ni kubwa ila inaendana na sifa zake nyingi inazoambatana nazo

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone17thumbnail

Bei ya Apple iPhone 17 na Sifa zake muhimu

Bei ya Apple iPhone 17 kwa hapa Tanzania ni shilingi milioni tatu (3) Hii ikiwa ni iphone yenye ukubwa wa GB 256 na RAM ya GB 8 Sasa basi, kwa […]

samsungs25thumb

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na sifa zake muhimu

Hii ni post inayoenda kukuonyesha kinaga ubaga juu ya ubora mkubwa wa simu mpya ya Samsung Galaxy S25 Ultra Samsung Galaxy S25 Ultra imeingia rasmi sokoni mnamo mwezi februari 2025 […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

huawei mate

Simu Bora 15 Duniani 2024 (na zitakazotamba 2025)

Kwa mwaka 2024, soko la simu janja yaani smartphone duniani lilitawaliwa na makampuni ya Apple, Samsung, Xiaomi, Vivo na Oppo Kwa hapa Afrika kampuni ya Samsung inaongoza kwa mauzo ikifuatiwa […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company