SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Apple iPhone 17 na Sifa zake muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

September 22, 2025

Bei ya Apple iPhone 17 kwa hapa Tanzania ni shilingi milioni tatu (3)

Hii ikiwa ni iphone yenye ukubwa wa GB 256 na RAM ya GB 8

iphone 17 showcase

Sasa basi, kwa nini utumie milioni tatu kwa ajili ya simu wakati Tecno Camon 40 bei yake ni 650k?

Sifa za iphone 17 zitakuonyesha utofauti mkubwa wa iphone na Tecno, pia simu zingine.

Hivyo basi hii post itakufafanulia kila sifa muhimu ya iphone 17

Sifa za Apple iPhone 17

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A19
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×4.26 GHz
  • Core Za kawaida(4) -4xX.X GHz
  • GPUApple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • iOS 26
Memori NMVe,256GB,512GB na RAM 8GB
Kamera Kamera mbili

  1. 48MP, dual pixel PDAF(wide)
  2. 48MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 3692mAh
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 3,000,000/=

Uwezo wa Network

Apple iPhone 17 inasapoti mitandao ya aina yote

Upande wa laini, inatumia laini za eSIM pekee kwa matoleo ya USA

Kwa nchi zingine zinasapoti laini za kawaida pia

network

Kwenye kudownload spidi yake inazidi zaidi ya 1000Mbps upande wa 5G

Sina uhakika kama 5G ya hapa Tanzania inasogea kiwango hiko

Kwa uzoefu wangu wa Airtel hufika 300Mbps

Ubora wa kioo cha Apple 17

Apple A17 inakuja na kioo cha LTPO OLED japo apple wanakiita super retina xdr

Ina kina kikubwa cha rangi kutokana na uwepo wa teknolojia za HDR10 na Dolby vision

Pia imewekewa refresh rate ya 120Hz ambayo haikuwepo toleo lililopita

Simu nyingi za Samsung zimekuwa zikitumia LTPO Amoled

display

Hiki kioo hudhibiti kiwango cha refresh rate kulingana na aina ya matumizi

Maana refresh rate kubwa hutumia umeme mwingi pia hivyo sio nyakati zote utahitaji kutumia 120Hz

Nguvu ya processor Apple A19

Mpaka sasa chip ya Apple A19 inazidiwa na Apple A19 Pro kiutendaji

Kwa mujibu wa app ya Geekbench Apple A19 inafika mpaka alama 3000

Pia hii chip ina ufanisi mzuri wa matumizi ya umeme

Kitu kinachofanya simu kukaa na chaji muda mrefu

Hii inamaanisha shughuli zinazohitaji nguvu kubwa bado hazitumii umeme kupitiliza

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya hii simu ina ukubwa wa 3692mAh

Ukitazama unaweza kuona ni ndogo

chaji

Kiuhalisia simu hii inakaa na chaji muda mrefu na inazizidi hata baadhi ya simu zenye 5000mAh

Ufanisi wa chaji unachagizwa na chip pia mfumo wake endeshi wa iOS 17

Uimara wa bodi ya Apple 17

Bodi ya Apple ni imara na ina uwezo wa kuzuia maji pindi simu ikizama kwenye kina kirefu

Kwa maana ina cheti cha IP68

Hii inamaanisha simu inaweza kuzuia maji hata ikizama kwenye kina cha mita 6

Pia imewekewa kioo cha Ceramic shield 2, hiki kioo kigumu zaidi ku-scratch na himilivu kupasuka kwenye kina cha mita mbili

Lakini hata hivyo vioo ni vioo tu umakini ni muhimu

Ubora wa kamera

iPhone 17 ina kamera mbili zote zikiwa na megapixel 48

Kamera zote zinatoa picha nzuri kwa kiwango kikubwa

Nyakati za mchana na hata mazingira ya mwanga hafifu vitu vinaonekana kwa uzuri

Inaweza kurekodi video za 4K kwa kiwango cha 60fps

kamera

Kamera zake zote zinaweza kutuliza mtikisiko wakati unarekodi video huku ukitembea

Hii inasaidiwa na uwepo wa sensor shift IOS

Ubora wa Software

iOS 26 haina tofauti kubwa na mfumo endeshi uliotangulia

iOS 26 inaweza kubadili rangi za icons kwa kuchukua rangi ya kava uliyoweka

Kitu kingine ni uwezo wa kupangalia home icons kwa namna unavyotaka

software

Mambo mengine ni uwepo wa matumizi ya AI

Japokuwa huku hakuna matumizi makubwa kama Samsung

Washindani wa Apple 17

Mshindani wa kwanza anaweza kuwa ni iPhone 16

Hizi simu mbili hazina utofauti mkubwa sana unaweza mshawishi kujipatia toleo jipya

Ikizingatiwa pia iphone 16 itapata ios 26 muda si mrefu

Pia Samsung Galaxy S25 ni mbadala sahihi

Neno la Mwisho

iPhone 17 ni moja ya simu bora mwaka 2025

Ila kulingana na bei yake unahitaji kuwa na sababu ya msingi sana kununua kama unayo iPhone 16

Kuna mabadiliko madogo sana kwenye toleo jipya

Wazo moja kuhusu “Bei ya Apple iPhone 17 na Sifa zake muhimu

  • Maoni yangu kuhusu IPhone 17 kitu gani kipya ambacho mmetuwekea ili niweze kuitambuwa hii iPhone 17 ni sim OG na siyo feki maana wajanja wengi sasa..

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsungs25thumb

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na sifa zake muhimu

Hii ni post inayoenda kukuonyesha kinaga ubaga juu ya ubora mkubwa wa simu mpya ya Samsung Galaxy S25 Ultra Samsung Galaxy S25 Ultra imeingia rasmi sokoni mnamo mwezi februari 2025 […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

huawei mate

Simu Bora 15 Duniani 2024 (na zitakazotamba 2025)

Kwa mwaka 2024, soko la simu janja yaani smartphone duniani lilitawaliwa na makampuni ya Apple, Samsung, Xiaomi, Vivo na Oppo Kwa hapa Afrika kampuni ya Samsung inaongoza kwa mauzo ikifuatiwa […]

No Featured Image

Bei na Ubora wa Samsung Galaxy S10 na iPhone 11 (2024-2025)

Samsung Galaxy S10 na iPhone 11 zilitoka rasmi mnamo mwaka 2019 Wakati zinatoka bei ya samsung galaxy s10 na iphone 11 zilikuwa zinazidi milioni moja Ila baada ya miaka mitano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company