SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Samsung 2025 na bei zake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

February 22, 2025

Mwezi wa Januari kampuni ya Samsung ilitangaza ujio wa matoleo matatu mapya ya Samsung Galaxy S25

Matoleo ya Samsung Galaxy S25 ni ya daraja la juu hivyo  ubora na bei huwa mkubwa

Mbali matoleo ya S-series, mwishoni mwa 2024 kuna matoleo ya daraja la kati na la mwisho yalitoka

Hii ni orodha ya samsung mpya na bei zake kwa mwaka 2025.

Samsung Galaxy S25 Ultra – milioni 3.5

Samsung Galaxy S25 Ultra ndio samsung yenye ubora zaidi kuliko samsung zote kwa sasa

Hii ni bei ya ukubwa wa GB 512

Utendaji wake ni mkubwa na inaambatana na mifumo yenye AI usahihi mkubwa katika kufanikisha jambo fulani

samsungs25ultra

Processor yake ni mpya na ni aina ya Snapdragon 8 Elite 3

Ina kamera nne ambazo lenzi zake ni wide, ultrawide, telephoto na periscope telephoto

Betri yake ina ukubwa wa 5000mAh na chaji yake inapeleka umeme wa wati 45 ambayo inachaji simu kwa haraka

Samsung Galaxy S25+ – milioni 2.8

Samsung Galaxy S25+ upande wa software na hardware zinafanana toleo la Ultra

Isipokuwa upande wa betri na kamera

Maana S25 Ultra kamera yake kubwa ina megapixel  200 ambapo Samsung Galaxy S25 Plus ina 50MP

samsungs25+

Kioo chake kina kina kikubwa cha rangi kwa sababu ya uwepo wa HDR10+

Na yenyewe inatumia processor ya Snapdragon 8 Elite 3 ambayo nguvu ya utendaji ni kubwa

Samsung Galaxy 25 – milioni 2.3

Hii ni samsung ya kamera tatu

Upande wa kimo hii simu ni fupi ukilinganisha na samsung zingine

Urefu wake ni inchi 6.1

Na hata betri yake lina ukubwa wa 4000mAh

samsungs25

Hivyo ukaaji wake wa chaji hautokuwa mkubwa kama Samsung Galaxy S25 Plus au Ultra

Na kama ilivyo kwa samsung zingine za mwaka 2025, na yenyewe itakuwa inapokea android mpya kwa miaka 7

Samsung Galaxy A06 5G – laki 3.5

Hii ni samsung inayotokana na Samsung Galaxy A06 ambayo ni ya daraja la chini

Utofauti mkubwa uliopo ni uwepo wa mtandao wa 5G

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu inatumia processor ya Mediatek Dimensity 6300

samsunga065g

Galaxy A06 ina kamera mbili ila kiuhalisia kamera yake ni moja tu

Betri yake ni kubwa(5000mAh) kasi ya kuchaji ni wati 25

Samsung Galaxy Z Fold Special – milioni 5.2

Hii ni simu ya kujikunja ambayo ilitoka mwishoni mwa 2024

Ukiikunjua upana wake unakuwa inchi 8

Ndio simu ya Samsung yenye bei kubwa kupititliza

samsungfoldspecial

Utendaji ni mkubwa a wenye nguvu kwani chip yake ni Snapdragon 8 Gen 3

Na ina kamera tatu huku kamera kubwa ikiwa na megapixel 200

Pia itakuwa inapokea updates kwa miaka saba

Samsung Galaxy A16 – laki 4

Samsung Galaxy A16 ni simu ya daraja la kati iliyotoka mwezi novemba 2024

Simu ina kamera tatu aina ya wide, ultrawide na macro

Ukubwa wa betri ni 5000mAh, na kasi ya juu ya kuchaji ni wati 25

samsunga16

Ina kioo cha super amoled chenye refresh rate ya 90Hz

La kufurahisha zaidi ni kuwa itakuwa inapokea matoleo mapya ya android kwa miaka 6

Ni nadra kukuta simu za laki nne kupata huduma kwa kipindi cha muda mrefu

Samsung Galaxy A16 5G – laki 5

Hii ni simu nyingine ya daraja inayosapoti mtandao wa 5G

Kama ilivyo mtangulizi wake na yenyewe itakuwa inapata toleo jipya la android kwa miaka sita

Hii simu ina waterproof aina ya IP54

Yaani inaweza kuzuia maji ya kiwango cha kunyunyulizika

Mfano wa mvua za manyunyu

Na yenyewe pia ina kioo cha super amoled chenye refresh rate ya 90Hz

Samsung Galaxy S24 FE – milioni 1.2

Unataka samsung galaxy s24 ya bei nafuu?

Basi Samsung Galaxy S24 FE ndio mbadala sahihi

samsungs24fe

Hautopata mambo yote ya Samsung Galaxy S24 ila kwa sehemu kubwa utaweza kupata hivyo vitu

Mfano kuwa na kamera inayoweza kurekodi video za 8K

Mng’ao wa video za 8K ni mkubwa na picha huonekana “clear” sana

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi15ultra

Simu mpya za Xiaomi(Redmi) 2025 na bei zake

Hii ni orodha ya simu mpya za redmi na Xiaomi ambazo zimetoka mwanzoni mwa 2025 na mwishoni mwa 2024 Simu zilizoorodheshwa zipo za bei kubwa na bei ndogo Hivyo basi […]

samsungs25thumb

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na sifa zake muhimu

Hii ni post inayoenda kukuonyesha kinaga ubaga juu ya ubora mkubwa wa simu mpya ya Samsung Galaxy S25 Ultra Samsung Galaxy S25 Ultra imeingia rasmi sokoni mnamo mwezi februari 2025 […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

huawei mate

Simu Bora 15 Duniani 2024 (na zitakazotamba 2025)

Kwa mwaka 2024, soko la simu janja yaani smartphone duniani lilitawaliwa na makampuni ya Apple, Samsung, Xiaomi, Vivo na Oppo Kwa hapa Afrika kampuni ya Samsung inaongoza kwa mauzo ikifuatiwa […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company