SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu za laki tatu zenye ubora wa kuridhisha kwa 2025

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

May 6, 2025

Iwapo unapanga kununua simu chini ya laki tatu au zisizozidi laki nne usitarajie kupata simu yenye ubora mkubwa

Kwa maana usitarajie kamera kali na utendaji mkubwa

Ila kwenye hii post kuna simu zote za laki tatu na chini ya laki nne zenye memori kubwa na utendaji wa wastani

Ubora ambao unakuwezesha kutumia app za muhimu zinazokidhi mahitaji yako

Aina za simu ni kutoka makampuni yafuatayo

  1. Infinix
  2. Samsung
  3. Xiaomi
  4. Oppo
  5. Vivo
  6. Tecno
  7. Realme

Sasa tuzitazame sifa za muhimu zinazohitajika zaidi na watumiaji wa simu wengi

Infinix Smart 9

Infinix ni simu yenye kamera ambayo ukubwa wake ni megapixel 13

Inaweza kurekodi video za full hd pekee

Bei yake ya GB 64 ni shilingi laki mbili na sabini (270,000)

smart9

Ina betri ya ukubwa wa 5000mAh ila kasi ya chaji yake ni wati 10 kama kiwango cha juu

Utendaji ni wa wastani kwa sababu inatumia chip ya Helio G81 ambayo inatumia core aina ya Cortex A75 kwenye yenye nguvu kubwa

Inakuja na mfumo endeshi wa Android 14 Go edition na haitopata android inayofuata

Infinix Smart 9 HD

Simu ya Infinix Smart 9 HD inauzwa kiasi cha shilingi 250,000 (laki mbili na nusu)

Hii ikiwa na ukubwa wa GB 64 na RAM ya GB 4

Pia ina kamera yenye ukubwa wa MP 13 haina vitu vingine vya ziada

Betri yake ina ukubwa wa mAh 5000 na chaji ya kasi ni wati 10

Utendaji sio mkubwa ukilinganisha na infinix smart 9

Hii inatokana na smart 9 hd kutumia processor Helio g50 ambazo zinatumia muundo wa Cortex A53

Tecno Spark 30C

Tecno Spark 30C inauzwa shilingi laki tatu na elfu ishirini

Iwapo simu za mbili za mwanzo hadhikizi unachotaka Tecno Spark 30C ni mbadala sahihi

Kuanzia skrini, inakupa refresh rate ya kiasi cha 120Hz

3-tecnospark30c

Kamera kubwa na lenzi moja ya usaidizi na kamera yake ina ukubwa wa megapixel 50

Utendaji wake ni mzuri unaoweza kusukuma vitu vingi japo si kwa ukubwa sana ila inafaa

Kizuri zaidi ina waterproof ya kuzuia maji ya kunyunyuluzika

Betri uku0bwa wake ni mAh na inachaji mpaka wati 18

Samsung Galaxy A06

Samsung Galaxy A06 kuipata kwa bei ya shilingi laki mbili na tisini

Haina tofauti kubwa na Tecno Spark 30C

Isipokuwa Samsung inaahidi kuipa simu maboresho kwa muda wa miaka miwili

Yaani itapata hadi android 16

4-samsunga06

Inatumia chip ya Mediatek Helio G85, hivyo utendaji wake ni wa wastani

Kamera yake ni kubwa na ina megapixel 50

Pia ina kamera nyingine ambayo haina umuhimu wa kihivyo

Samsung Galaxy A05

Samsung Galaxy A05 ni simu ya mwaka 2023 ila bado inaendana na wakati wa sasa

Bei yake kwa sasa ni shilingi laki mbili na sabini

Inasapoti chaji ya wati 25 hivyo betri yake ya mAh 5000 inawahi kujaa kwa haraka

5-samsunga05

Utendaji wake uko sawa na Galaxy A06 kwa sababu zinatumia processor moja

Ina kamera mbili na kamera kubwa ina 50MP

Inakuja na android 13 na haipati toleo lingine jipya

Tecno Pop 9

Bei ya Tecno Pop 9 ni shilingi 270,000 ikiwa ni ya GB 64

Utendaji wake ni mzuri kwa sababu inatumia chip ya Unisoc T615

Kamera yake ukubwa ni megapixel 13 ikiwa na ulengaji wa PDAF

6-tecnopop9

Inakuja na mfumo endeshi wa Android 14 Go Edition

Kioo chake kinakuja na refresh rate ya 120Hz

Chaji inasapoti umeme wa wati 15

Redmi 14C

Bei ya Redmi 14C ni shilingi laki tatu na nusu (350,000)

Bei yake ipo juu kidogo ukilinganisha na simu zingine zilizopo hapa

Ila kiutendaji haina tofauti kubwa na simu zingine

Kitu cha ziada inakuja na skrini prtotecta yenye uwezo wa kuzuia michubuko

7-redmi14c

Inatumia Android 14 na haitopata Android 14

Kamera yake kubwa ina megapixel 50

Betri yake ukubwa ni mAh 5160, na chaji inapeleka hadi umeme wa wati 18

Oppo A3X

Oppo A3X inauzwa kwa shilingi 300,000 (laki tatu) japo kwa sasa inapatikana India

Betri yake ina ukubwa wa mAh 5100

Pia utendaji wake ni mzuri kutokana kutumia processor ya Mediatek Dimensity 6300

Ni simu inayopleleka chaji kwa kasi kubwa inayofika wati 45

8-oppoa3x

Hii inajaza simu kwa 50% ndani ya nusu saa

Kamera yake sio kubwa ina megapixel 8 tu ila ina ulengaji wa PDAF

Pi aina waterproof aina ya IP54

Vivo Y19s

Vivo Y19s inauzwa kwa kiasi cha shilingi laki tatu na nusu (350,000)

Kwa ufanano wa kiutendaji inaendana na Oppo A3X

Inakuja na toleo la Android 14 na haitokuwa na update ya android mpya

Betri yake ina ukubwa 5500mAh, inakaa na chaji muda mrefu

9-vivoy19s

Ila itachukua muda kujaa kwa sababu chaji inayosapoti kiwango cha juu ni wati 15

Utendaji wake pia ni wa kuridhisha kwani inatumia chip ya Unisoc Tiger T612

Ukubwa wa kamera yake ni megapixel 50

Realme C63

Bei ya Realme C63 ni shilingi 350,000 kwa Tanzania

Realme inaweza kuwa ni jina geni ila ni moja ya kampuni ya china inayotengeneza simu nzuri

Realme C63 ina kamera moja yenye megapixel 50

10-realmec63

Chaji yake inasapoti umeme wa wati 45 hivyo simu inawahi kujaa kwa haraka

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu ya uwepo wa processor ya Unisoc Tiger T612

Na inakuja na Android 14, haitapokea toleo lingine la Android

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix note 50 thumb

Ubora wa simu mpya za Infinix Note 50

Katika baadhi ya nchi, Infinix walitoa toleo jipya la Infinix Note 50 Matoleo hayo ni Infinix Note 50 4G Infinix Note 50s Infinix Note 50 Pro 4G Infinix Note 50 […]

tecno camon 40 pro thumb

Bei ya Tecno Camon 40 Pro na Sifa zake za muhimu mpya

Hapa utaenda kufahamu bei halisi ya Tecno mpya ya 2025 Tecno hiyo ni Tecno Camon 40 Pro ambayo imezinduliwa mwezi wa tatu Camon 40 Pro inafanana kiasi flani na Camon […]

samsungA56

Bei ya Samsung Galaxy A56 na sifa zake muhimu

Hii ni posti yenye maelezo ya kina kuhusu bei ya Samsung Galaxy A56 na sifa zake Utafahamu bei yake kulingana na ukubwa wa memori Na pia utofauti uliopo kati ya […]

Ujio wa Simu mpya za Tecno Camon 40

Huu mwezi wa tatu 2025 tecno imetangaza ujio wa matoleo mapya ya Tecno Camon 40 Simu hizo ni Tecno Camon 40 Tecno Camon 40 Pro 5G Tecno Camon Pro Tecno […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company