SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Infinix Hot 60 na bei zake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

July 19, 2025

Infinix Hot 60 ni matoleo ya daraja kati yaliyoingia rasmi sokoni mnamo mwezi Julai 2025

Bei zake sio kubwa ni za wastani huku ukiwa na uhakika wa kupata mifumo mingi ya AI ambapo kwa brand zingine huweka kwenye simu za daraja juu

Infinix hot 60 zimekuja na maboresho upande wa betri, skrini na uimara wa bodi bila kusahau softaware

Hapa utaona simu zote za mpya za infinix hot 60 na bei zake kwa wakati huu kwa hapa Tanzania

Infinix Hot 60 Pro

Bei ya Infinix hot 60 Pro ni shilingi laki nne (400,000)

Hii ni infinix yenye ukubwa wa RAM GB 8 na ukubwa wa GB 128

Pia kuna infinix ya ukubwa wa GB 256 na bei yake pia ni kubwa zaidi ya GB 128

infinix hot 60 pro

Sifa kubwa nzuri za hii simu ina kioo cha amoled chenye refresh rate inayofika 144Hz

Ina ulinzi wa kioo aina ya Corning Gorilla glass 7i

Pia betri kubwa ya mAh 5160 na chaji ya wati 45 na uwezo wa kuchaji vifaa vingine kwa umeme wa wati 10

Infinix Hot 60i

Bei ya Infinix Hot 60i ni shilingi laki tatu (300,000)

Hii ikiwa na ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 8

Ndio infinix hot 60 yenye bei ndogo zaidi kati ya zilizotoka mwaka 2025

hot60i

Sifa yake kubwa ni kwamba bei yake ni rahisi ila inakupa mifumo mingi ya AI kama ilivyo kwenye simu za Infinix Note 50

Pia chaji inapeleka umeme mwingi wa wati 45

Na pia ina ulinzi wa waterproof aina ya IP64

Infinix Hot 60 Pro+

Infinix Hot 60 Pro+ ya GB 256 inauzwa shilingi laki tano na elfu therathini (530,000)

Hii ikiwa na ukubwa wa RAM ya GB 8

hot60pro+

Kisifa hii simu haina tofauti sana infinix hot 60 pro

Vitu vingi vinafanana

Kwenye makara zijazo tutazama kiundani kuangalia kila sifa na upekee wa simu

Maoni 8 kuhusu “Simu mpya za Infinix Hot 60 na bei zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix hot 60 pro thum

Bei ya Infinix Hot 60 Pro na sifa zake muhimu

Je unajua kuwa simu ya Infinix Hot 60 Pro inaiacha mbali Samsung Galaxy A16? Wakati huo Infinix Hot 60 Pro bei yake iko chini ukilanganisha Samsung Kwenye hii post utafahamu […]

camon 40

Bei ya Tecno Camon 40 na sifa zake muhimu

Simu za madaraja zinazotoka miaka ya karibuni zinashawishi kuachana na kununua simu za gharama kubwa Maana matoleo mapya yamekuwa na ubora wenye tofauti ndogo  na simu za bei kubwa Tofauti […]

Bei ya Infinix Note 50 na Sifa zake muhimu

Infinix wametoa matoleo mapya na yameshaanza kupatikana Tanzania Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 50 ambayo ina maboresho upande wa software, kioo na uimara wa simu kiujumla Kwa sifa […]

sony xperia xz3

Simu za Sony Xperia za bei rahisi kwa Tanzania

Simu ya Sony iliyotoka mwaka huu 2025 ni Sony Xperia 1 VII Bei yake unaijua ni shilingi ngapi? ni milioni nne na  laki tano huko duniani Ni bei kubwa sana […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company