Hii ni orodha ya simu mpya za redmi na Xiaomi ambazo zimetoka mwanzoni mwa 2025 na mwishoni mwa 2024
Simu zilizoorodheshwa zipo za bei kubwa na bei ndogo
Hivyo basi utafahamu bei zake na sifa pamoja na ubora mkubwa kwenye kila simu iliyopo
Utaona simu ya Xiaomi iliyopo kwenye ligi moja na iPhone na Samsung
Tuzione sasa.
Xiaomi Redmi Note 14 Pro+ 5G
Bei ya Xiaomi Redmi Note 14 Pro+ 5G ni shiling milioni 1.1 ya ukubwa wa GB 256 na RAM GB 8
Utendaji wake unaweza kuhimili kucheza magemu tofauti bila shida
Kwani inatumia processor ya Snapdragon 7s Gen yenye ufanisi wa matumizi mazuri ya umeme
Ni simu yenye kamera tatu na kamera kubwa ina 200MP
Betri yake ina ukubwa wa 5110mAh na nguvu ya kuchaji ni kubwa ambayo ni 120W
Xiaomi Redmi Note 14 Pro 4G
Bei ya Xiaomi Redmi Note 14 Pro ni shilingi laki saba (700,000) ya ukubwa wa GB 256 na RAM GB 8
Na hii pia ina kamera tatu kubwa ikiwa na megapixel 200
Inakuja na mfumo endeshi wa Android 14 na haitopata toleo lingine
Betri yake ni kubwa sana ambayo ni 5500mAh ila chaji yake kasi ni 45mAh
Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu inatumia processor Mediatek Helio G100 Ultra
Xiaomi Redmi Note 14 5G
Bei ya Redmi Note 14 5G ya GB 256 na RAM GB 8 ni shilingi laki saba
Boresho kubwa kwenye hii simu ni uwepo wa mtandao wa 5G
Kwenye kamera yapo yaliyopunguzwa, kamera kubwa ina 108MP
Hii simu itapokea matoleo mapya ya android kwa miaka miwili
Betri yake ina ukubwa wa 5110mAh na chaji inapeleka kasi ya wati 45
Xiaomi Remi Note 14 4G
Bei ya Redmi Note 14 4G ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 6 ni shilingi laki tano (500,000)
Haina utendaji mkubwa ila utendaji wake ni wa wastani
Inatumia chip ya mediatek helio G99 Ultra
Mfumo wake wa kamera ni wakawaida hauna vitu vingi ila kamera kubwa ina 108MP
Hii simu inakuja na Android 14 na itapata matoleo mengine mara nne
Xiaomi Redmi 14C 5G
Bei ya Xiaomi Redmi 14C 5G ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 4 ni laki tatu na elfu hamsini (350,000)
Ni simu ya daraja la chini ila utendaji wake ni mzuri ukilinganisha na bei
Kwani inatumia processor ya Snapdragon 4 Gen 2
Simu itapokea matoleo mapya mawili ya Android
Upande wa kamera kuna kamera moja tu yenye megapixel 50
Betri yake ina mAh 5160 na spidi ya chaji ni wati 18(sio kubwa)
Xiaomi 15 Ultra
Xiaomi 15 Ultra bei yake ni shilingi milioni mbili na kaki tano (2,500,000)
Hii ndio simu yenye ufunano na matoleo ya iphone 16 ama Samsung Galaxy S25
Ina jumla ya kamera nne na kamera kubwa ina megapixel 200 huku zingine zikiwa na megapixel 50
Betri yake ni kubwa na ina mAh 6000 na chaji ya kasi ya 90W
Ina nguvu kubwa ya kiutendaji kwa sababu ina processor ya Snapdragon 8 Elite
Simu inakuja na Android 15 na itapata matoleo mapya ya android mara nne tu.
Xiaomi Poco X7 Pro
Bei ya Xiaomi Poco X7 Pro ni milioni moja na laki moja yenye GB 256 na RAM ya GB 8
Ina kamera mbili tu huku kamera kubwa ikiwa na 50MP
Inatumia processor ya Dimensity 8400 Ultra hivyo utendaji wake ni mzuri
Inakuja na mfumo endeshi wa Android 15 na hakuna taarifa kama itapata toleo jipya
Betri yake ni kubwa (mah 6000) na chaji yake inasapoti wati 90
Xiaomi 17
Bei ya Xiaomi 17 kwa Tanzania ni shilingi milioni 1.8
Imetoka rasmi mnamo mwezi septemba, 2025
Ina jumla ya kamera zipatazo tatu zote zikiwa na megapixel 50
Betri yake ni kubwa sana kwani ina mAh 7000mAh
Chaji yake inasapoti umeme mpaka wa wati 100, hivyo ni fast chaji
Inakuja na mfumo endeshi wa Android 16 ikiwa na HyperOs 3
Xiaomi 17 pro
Bei ya Xiaomi 17 Pro kwa hapa Tanzania ni shilingi milioni 2
Utendaji wake ni mkubwa kwa sababu inatumia prosesa ya Snapdragon 8 Elite Gen 5
Betri yake sio kubwa kama ilivyo kwa Xiaomi 17 kwani ina mAh 6300
Na yenyewe chaji yake inapeleka umeme hadi wa wati 100
Pia jumla ya kamera zake zipo tatu na zina megapixel 50
Inatumia mfumo endeshi wa Android 16 na HyperOs 3
Xiaomi 17 Pro Max
Bei ya Xiaomi 17 Pro Max kwa Tanzania ni shilingi milioni 2.2
Haina tofauti kisifa na Xiaomi 17 Pro ila kuna nyongeza ya vitu kadhaa
Kwanza, urefu wake ni mkubwa kutokana na kimo cha inchi 6.9
Betri yake kubwa sana ina ujazo wa mAh 7500
Mengineyo hayana tofauti kwa sehemu kubwa
Redmi note 15
Bei ya Redmi Note 15 toleo la China kwa hapa Tanzania ni shilingi 580,00
Toleo la duniani bado halijatoka inawzekana mpaka mwakani 2026
Utendaji wake unaweza kusukuma kila aina ya app kwa sababu inatumia processor ya Snapdragon 6 Gen 3
Ina kamera mbili za wide na depth, moja tu ina 50mp
Betri yake ni kubwa ina mAh 5800
Pia inakuja na toleo la android 15 na hyperos 2
Redmi Note 15 Pro
Redmi Note 15 Pro kwa hapa Tanzania unaweza ipata kwa shilingi 750,000
Ina betri yenye ukubwa wa mAh 7000
Jumla ya kamera inazokuja nazo ni mbili ambazo ni wide na ultrawide
Utendaji wake ni mzuri pia kutokana na kutumia prosesa Mediatek Dimensity 7400
Chaji yake inaweza kupeleka mpaka umeme wa wati 45
Redmi Note 15 Pro+
Bei ya Redmi Note 15 Pro+ kwa Tanzania inauzwa shilingi 970,000
Hii ni redmi yenye nguvu zaidi kwa sababu inatumia processor ya Snapdragon 7s Gen 4
Simu inakuja na kamera tatu aina ya wide, ultrawide na telephoto
Betri yake ina ujazo wa mAh 7000
Chaji yake inasapoti na kupeleka umeme wa wati 90
Na yenyewe inatumia Android 15 ikiwa na HyperOs 2
Redmi 15
Bei ya Redmi 15 kwa Tanzania ni shilingi laki tano na nusu
Ni simu ya daraja la kati inayokubali mtandao wa 5G
Na yenyewe betri lake lina ukubwa wa 7000mAh
Chaji yake inasapoti umeme wa wati 33, hivyo kwa ukubwa wa betri simu inaweza chukua muda kidogo
Upande wa software inakuja na Android 15
Redmi 15c
Redmi 15C bei yake ni shilingi 350,000 kwa ya GB 256
Hii ni simu bajeti inayolenga zaidi mtumiaji wa kawaida
Ina kamera mbili huku moja ikiwa na megapixel ya 50
Inakuja na android 15 na hyperos 2
Betri yake ina ukubwa wa mAh 6000
Utendaji wa simu ya Redmi 15C ni wa wastani unaotokana na uwepo wa prosesa ya kawaida
Maoni 3 kuhusu “Simu mpya za Xiaomi(Redmi) 2025 na bei zake”
Mpanue wigo wa biashara kuwe na agent kila wilaya mtauza mno
Siom gan? wanaweza kutumia wenye uwezo wa chini
simu yoyote unaweza kutumia kulingana na bajeti yako