SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Xiaomi(Redmi) 2025 na bei zake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

March 1, 2025

Hii ni orodha ya simu mpya za redmi na Xiaomi ambazo zimetoka mwanzoni mwa 2025 na mwishoni mwa 2024

Simu zilizoorodheshwa zipo za bei kubwa na bei ndogo

Hivyo basi utafahamu bei zake na sifa pamoja na ubora mkubwa kwenye kila simu iliyopo

Utaona simu ya Xiaomi iliyopo kwenye ligi moja na iPhone na Samsung

Tuzione sasa.

Xiaomi Redmi Note 14 Pro+ 5G

Bei ya Xiaomi Redmi Note 14 Pro+ 5G ni shiling milioni 1.1 ya ukubwa wa GB 256 na RAM GB 8

Utendaji wake unaweza kuhimili kucheza magemu tofauti bila shida

1-redminote14proplus

Kwani inatumia processor ya Snapdragon 7s Gen yenye ufanisi wa matumizi mazuri ya umeme

Ni simu yenye kamera tatu na kamera kubwa ina 200MP

Betri yake ina ukubwa wa 5110mAh na nguvu ya kuchaji ni kubwa ambayo ni 120W

Xiaomi Redmi Note 14 Pro 4G

Bei ya Xiaomi Redmi Note 14 Pro ni shilingi laki saba (700,000) ya ukubwa wa GB 256 na RAM GB 8

Na hii pia ina kamera tatu kubwa ikiwa na megapixel 200

redminote14pro4g

Inakuja na mfumo endeshi wa Android 14 na haitopata toleo lingine

Betri yake ni kubwa sana ambayo ni 5500mAh ila chaji yake kasi ni 45mAh

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu inatumia processor Mediatek Helio G100 Ultra

Xiaomi Redmi Note 14 5G

Bei ya Redmi Note 14 5G ya GB 256 na RAM GB 8 ni shilingi laki saba

Boresho kubwa kwenye hii simu ni uwepo wa mtandao wa 5G

Kwenye kamera yapo yaliyopunguzwa, kamera kubwa ina 108MP

3-redminote145g

Hii simu itapokea matoleo mapya ya android kwa miaka miwili

Betri yake ina ukubwa wa 5110mAh na chaji inapeleka kasi ya wati 45

Xiaomi Remi Note 14 4G

Bei ya Redmi Note 14 4G ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 6 ni shilingi laki tano (500,000)

Haina utendaji mkubwa ila utendaji wake ni wa wastani

Inatumia chip ya mediatek helio G99 Ultra

redminote144g

Mfumo wake wa kamera ni wakawaida hauna vitu vingi ila kamera kubwa ina 108MP

Hii simu inakuja na Android 14 na itapata matoleo mengine mara nne

Xiaomi Redmi 14C 5G

Bei ya Xiaomi Redmi 14C 5G ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 4 ni laki tatu na elfu hamsini (350,000)

Ni simu ya daraja la chini ila utendaji wake ni mzuri ukilinganisha na bei

Kwani inatumia processor ya Snapdragon 4 Gen 2

redmi14c5g

Simu itapokea matoleo mapya mawili ya Android

Upande wa kamera kuna kamera moja tu yenye megapixel 50

Betri yake ina mAh 5160 na spidi ya chaji ni wati 18(sio kubwa)

Xiaomi 15 Ultra

Xiaomi 15 Ultra bei yake ni shilingi milioni mbili na kaki tano (2,500,000)

Hii ndio simu yenye ufunano na matoleo ya iphone 16 ama Samsung Galaxy S25

Ina jumla ya kamera nne na kamera kubwa ina megapixel 200 huku zingine zikiwa na megapixel 50

xiaomi15ultra

Betri yake ni kubwa na ina mAh 6000 na chaji ya kasi ya 90W

Ina nguvu kubwa ya kiutendaji kwa sababu ina processor ya Snapdragon 8 Elite

Simu inakuja na Android 15 na itapata matoleo mapya ya android mara nne tu.

Xiaomi Poco X7 Pro

Bei ya Xiaomi Poco X7 Pro ni milioni moja na laki moja yenye GB 256 na RAM ya GB 8

Ina kamera mbili tu huku kamera kubwa ikiwa na 50MP

Inatumia processor ya Dimensity 8400 Ultra hivyo utendaji wake ni mzuri

pocox7pro

Inakuja na mfumo endeshi wa Android 15 na hakuna taarifa kama itapata toleo jipya

Betri yake ni kubwa (mah 6000) na chaji yake inasapoti wati 90

Xiaomi 17

Bei ya Xiaomi 17 kwa Tanzania ni shilingi milioni 1.8

Imetoka rasmi mnamo mwezi septemba, 2025

Ina jumla ya kamera zipatazo tatu zote zikiwa na megapixel 50

xiaomi 17

Betri yake ni kubwa sana kwani ina mAh 7000mAh

Chaji yake inasapoti umeme mpaka wa wati 100, hivyo ni fast chaji

Inakuja na mfumo endeshi wa Android 16 ikiwa na HyperOs 3

Xiaomi 17 pro

Bei ya Xiaomi 17 Pro kwa hapa Tanzania ni shilingi milioni 2

Utendaji wake ni mkubwa kwa sababu inatumia prosesa ya Snapdragon 8 Elite Gen 5

Betri yake sio kubwa kama ilivyo kwa Xiaomi 17 kwani ina mAh 6300

xiaomi 17 pro

Na yenyewe chaji yake inapeleka umeme hadi wa wati 100

Pia jumla ya kamera zake zipo tatu na zina megapixel 50

Inatumia mfumo endeshi wa Android 16 na HyperOs 3

Xiaomi 17 Pro Max

Bei ya Xiaomi 17 Pro Max kwa Tanzania ni shilingi milioni 2.2

Haina tofauti kisifa na Xiaomi 17 Pro ila kuna nyongeza ya vitu kadhaa

Kwanza, urefu wake ni mkubwa kutokana na kimo cha inchi 6.9

xiaomi 17 pro max

Betri yake kubwa sana ina ujazo wa mAh 7500

Mengineyo hayana tofauti kwa sehemu kubwa

Redmi note 15

Bei ya Redmi Note 15 toleo la China kwa hapa Tanzania ni shilingi 580,00

Toleo la duniani bado halijatoka inawzekana mpaka mwakani 2026

Utendaji wake unaweza kusukuma kila aina ya app kwa sababu inatumia processor ya Snapdragon 6 Gen 3

redmi note 15

Ina kamera mbili za wide na depth, moja tu ina 50mp

Betri yake ni kubwa ina mAh 5800

Pia inakuja na toleo la android 15 na hyperos 2

Redmi Note 15 Pro

Redmi Note 15 Pro kwa hapa Tanzania unaweza ipata kwa shilingi 750,000

Ina betri yenye ukubwa wa mAh 7000

Jumla ya kamera inazokuja nazo ni mbili ambazo ni wide na ultrawide

redmi note 15 pro

Utendaji wake ni mzuri pia kutokana na kutumia prosesa Mediatek Dimensity 7400

Chaji yake inaweza kupeleka mpaka umeme wa wati 45

Redmi Note 15 Pro+

Bei ya Redmi Note 15 Pro+ kwa Tanzania inauzwa shilingi 970,000

Hii ni redmi yenye nguvu zaidi kwa sababu inatumia processor ya Snapdragon 7s Gen 4

Simu inakuja na kamera tatu aina ya wide, ultrawide na telephoto

redmi note 15 pro plus

Betri yake ina ujazo wa mAh 7000

Chaji yake inasapoti na kupeleka umeme wa wati 90

Na yenyewe inatumia Android 15 ikiwa na HyperOs 2

Redmi 15

Bei ya Redmi 15 kwa Tanzania ni shilingi laki tano na nusu

Ni simu ya daraja la kati inayokubali mtandao wa 5G

Na yenyewe betri lake lina ukubwa wa 7000mAh

redmi 15 5g

Chaji yake inasapoti umeme wa wati 33, hivyo kwa ukubwa wa betri simu inaweza chukua muda kidogo

Upande wa software inakuja na Android 15

Redmi 15c

Redmi 15C bei yake ni shilingi 350,000 kwa ya GB 256

Hii ni simu bajeti inayolenga zaidi mtumiaji wa kawaida

Ina kamera mbili huku moja ikiwa na megapixel ya 50

Inakuja na android 15 na hyperos 2

redmi 15c

Betri yake ina ukubwa wa mAh 6000

Utendaji wa simu ya Redmi 15C ni wa wastani unaotokana na uwepo wa prosesa ya kawaida

 

Maoni 3 kuhusu “Simu mpya za Xiaomi(Redmi) 2025 na bei zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 17 thumbs

Bei ya Xiaomi 17 na Sifa Zake Muhimu

Xiaomi 17 ni bonge moja la simu kwa kutazama sifa zake zote Bei yake kwa hapa Tanzania ni shilingi milioni 2.3 yenye ukubwa wa GB 256 na RAM ya GB […]

infinix hot 60 pro thum

Bei ya Infinix Hot 60 Pro na sifa zake muhimu

Je unajua kuwa simu ya Infinix Hot 60 Pro inaiacha mbali Samsung Galaxy A16? Wakati huo Infinix Hot 60 Pro bei yake iko chini ukilanganisha Samsung Kwenye hii post utafahamu […]

bei ndogo

Simu za laki tatu zenye ubora wa kuridhisha kwa 2025

Iwapo unapanga kununua simu chini ya laki tatu au zisizozidi laki nne usitarajie kupata simu yenye ubora mkubwa Kwa maana usitarajie kamera kali na utendaji mkubwa Ila kwenye hii post […]

infinix note 50 thumb

Ubora wa simu mpya za Infinix Note 50

Katika baadhi ya nchi, Infinix walitoa toleo jipya la Infinix Note 50 Matoleo hayo ni Infinix Note 50 4G Infinix Note 50s Infinix Note 50 Pro 4G Infinix Note 50 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company