SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Tecno Spark 40 na bei zake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

August 4, 2025

Unajua kuwa mwaka 2025, Tecno imezindua simu tatu mpya katika familia ya Spark 40?

Simu hizo ni:
📱 Tecno Spark 40
📱 Tecno Spark 40 Pro
📱 Tecno Spark 40 Pro+

Bei zke zinaanzia Tsh 260,000 hadi kufikia takribani Tsh 500,000.
Kila toleo lina sifa tofauti zinazolifanya lifae kwa matumizi maalum. Hii ina maana kuna Spark inayokufaa kulingana na bajeti na mahitaji yako.

Ni muhimu kuelewa vizuri kila moja ili ujue ipi inakufaa zaidi.
Twende tukazichambue moja baada ya nyingine

Tecno Spark 40

Bei ya Tecno Spark 40 ni shilingi laki mbili na sitini (260,000)

Hii ikiwa na ukubwa wa ram ya GB 4 na memori ya GB 128

Utendaji wake unafaa zaidi kwa matumizi ya kawaida ya kila siku

1-tecnospark40

Kwa sababu prosesa yake ya Helio G81 ina nguvu ya wastani

Hii simu ina kamera moja yenye ukubwa megapixel 50

Inasapoti chaji ya wati 45 na betri yake ina ukubwa wa mAh 5200

Tecno Spark 40 Pro

Tecno Spark 40 Pro bei yake ni shilingi laki nne na ishirini (420,000)

Utendaji wake unakidhi kucheza baadhi ya gemu ila kwa settings za chini

Kwa sababu inatumia prosesa yenye nguvu ya wastani ambayo ni Mediatek Helio G100 Ultimate

1-tecnospark40pro

Inakuja na kioo kizuri cha amoled chenye refresh rate inayofika hadi 144Hz

Upande wa betri ina 5200mAh na chaji inayopeleka umeme hadi wati 45

Ina kamera ya ukubwa wa 50MP inayoweza kurekodi video za ubora wa 1440p

Tecno Spark 40 Pro+

Tecno Spark 40 Pro+ inauzwa shilingi laki tano

Hii ni bei ya Spark 40 Pro+ ya GB 128 na RAM GB 8

Spark 40 Pro+ inasapoti kuchajiwa kwa njia ya wireless kwa umeme wa wati 30

Ni simu yenye cheti cha IP67 chenye kuashiria uwezo wa simu kuzuia maji ya kina cha mita 1.5

Ukiondoa vitu hivi viwili sifa zingine zote zinafanana Tecno Spark 40 Pro

Maoni 6 kuhusu “Simu mpya za Tecno Spark 40 na bei zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

spark 40 pro

Bei ya Tecno Spark 40 Pro na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 40 Pro imewasili! Mwezi Julai 2025, Tecno imezindua rasmi toleo jipya lenye nguvu na muonekano wa kisasa zaidi. Spark 40 Pro inakuja na maboresho makubwa katika maeneo manne […]

infinix hot 60

Simu mpya za Infinix Hot 60 na bei zake

Infinix Hot 60 ni matoleo ya daraja kati yaliyoingia rasmi sokoni mnamo mwezi Julai 2025 Bei zake sio kubwa ni za wastani huku ukiwa na uhakika wa kupata mifumo mingi […]

camon 40

Bei ya Tecno Camon 40 na sifa zake muhimu

Simu za madaraja zinazotoka miaka ya karibuni zinashawishi kuachana na kununua simu za gharama kubwa Maana matoleo mapya yamekuwa na ubora wenye tofauti ndogo  na simu za bei kubwa Tofauti […]

Bei ya Infinix Note 50 na Sifa zake muhimu

Infinix wametoa matoleo mapya na yameshaanza kupatikana Tanzania Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 50 ambayo ina maboresho upande wa software, kioo na uimara wa simu kiujumla Kwa sifa […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company