SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Samsung na bei zake (2026)

Brand

Sihaba Mikole

March 10, 2026

Simu mpya za Samsung  kwa mwaka 2026 zina maboresho makubwa kwa simu za madaraja yote

Maboresho makubwa zaidi yammefanyika kwenye utendaji

Hivyo hii hapa ni orodha ya baadhi ya simu za Samsung zinazopatikana hapa Tanzania

Kila siku utajua ubora wake na bei yake hapa nchini

Samsung Galaxy S26 Ultra

Bei ya Samsung Galaxy S26 Ultra ni shilingi milioni 3.8 hasa kwa dar es salaam

Samsung hii inakuja na prosesa mpya aina ya Snapdragon 8 Elite Gen 5

Snapdragon 8 Elite Gen 5 ina pafomansi kubwa kwenye kila idara

Na ufanisi wake wa kukaa chaji ni mkubwa

Boreshwa la ajabu zaidi ni upande wa skrini

Skrini ya samsung galaxy s26 ultra ina uwezo wa kuzuia mtu wa pembeni asione kile unachokiangalia

Inadumisha faragha

Samsung Galaxy 26+

Bei ya Samsung Galaxy S26+ ni shilingi milion 3.2

Ina sifa zote kama za Samsung Galaxy S26 Ultra

Isipokuwa Galaxy S26+ ina kimo cha inchi 6.7

Pia chaji yake kasi ya juu ya kupeleka umeme ni wati 45

Samsung Galaxy S26

Bei ya Samsung Galaxy S26 ni shilingi milioni 2.8

Upande wa betri inatumia betri dogo zaidi kuliko samsung zingine

Ni simu yenye kimo kifupi cha inchi 6.3

Samsung Galaxy Z Trifold

Samsung Galaxy Z Trifold ndio samsung ya gharama zaidi kwa sasa

Bei ya Samsung Galaxy Z Trifold ni shilingi milioni 7.8

Hii simu ina skrini zipatazo tatu

Ukiikunjua skrini zote upana wake unafika inchi 10 sawa na Tablet za walimu

Betri lake lina ukubwa wa mAh 5600

Utendaji wake pia ni mkubwa

 

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company