SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za iPhone 17 na bei zake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

September 16, 2025

Kuna simu mpya za matoleo ya iPhone 17 ambayo apple wameyazinduwa septemba 2025

Kuna kipya lakini si kikubwa sana

Ila kinaweza kukuvuta kuinunua moja iphone za mwaka 2025

Kama una hamu ya upekee wa hizi iphone 17 ukilinganisha na toleo la iphone 16 basi pitia sifa za kila iphone

Hapa kuna sifa muhimu za iphone mpya za matoleo ya:

  1. Apple iPhone 17
  2. Apple iPhone 17 Pro
  3. Apple iPhone 17 Pro Max
  4. Apple iPhone Air

Apple iPhone 17

Bei ya iPhone 17 kwa Tanzania ni shilingi milioni 3

Ni simu ya kimo cha inchi 6.3 kimo cha wastani

Upande wa mifumo ya memori inakuja na RAM ya GB 8 na ukubwa wa memori GB 256 au 512

Inatumia mfumo endeshi mpya wa iOS 26

iphone 17

Betri yake ni ndogo kwani ukubwa wake ni mAh 3692

Kasi chaji yake ni ya wastani, inapeleka umeme unaofika hadi wati 25

Inakuja na kamera mbili za lenzi upana wa kawaida na lenzi ya upana mkubwa mkubwa sana zote zina 48MP

Apple iPhone 17 Pro

Bei ya iPhone 17 Pro ni shilingi milioni 4 kwa Tanzania

Na yenyewe kimo chake ni inchi 6.3

Ila utendaji wake ni mkubwa zaidi ya Apple iPhone 17

Kwani inatumia chip aina ya Apple 19 Pro

Ukubwa wa betri ni wa wastani kwani ina mAh 3988

iphone 17 pro

Wakati kiwango cha juu cha kuchaji ni wati 25 ambayo sio kikubwa sana

RAM ina ukubwa wa GB 12, huku kamera zikiwa tatu zenye 48MP

Kamera iliyoongezeka ni ya lenzi ya periscope telephoto kwa ajili ya kupiga vitu vilivyo mbali sana na kamera

Apple iPhone 17 Pro Max

Bei ya iPhone 17 Pro Max kwa Tanzania ni shilingi ni milioni 4.5

Ni apple yenye ndefu zaidi kwa sababu kimo chake ni inchi 6.9

Pia ina betri kubwa, kwa matoleo ya USA ni mah 5088, na kwingineko ni mah 4832

Na yenyewe inakuja na kamera tatu kama ilivyo Pro

iphone 17 pro max

Utendaji wake ni mkubwa, inatumia chip ya Apple 19 Pro

RAM yake ina ukubwa wa 12GB ukubwa wa memori unaanzia GB 256 hadi 1TB

Kiujumla kilichoongezeka kwenye pro max ni betri na urefu wa simu

Apple iPhone Air

Bei ya iPhone Air ni shilingi milioni 3.7

iPhone Air haina tofauti sana iPhobe 17 Pro

Utofauti wake ni wembamba

Hii ni iphone nyembamba zaidi kama ilivyo kwa samsung galaxy 25 edge

Pia ina betri dogo lenye ukubwa wa mAh 3149

Kwa bahati mbaya ama nzuri toleo hili linatumia laini za eSIM pekee

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company