SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Jinsi ya kujua iPhone original kirahisi

Miongozo

Sihaba Mikole

December 16, 2025

Unaiona hii picha ya simu mbili za toleo la Apple iPhone 14 Pro Max

Moja ya kati hizi iphone ni feki.

fake vs original ip14promax

Je kwa kutazama unaweza kuijua ipi ni iphone original kati ya hizi simu mbili?

Kama umeshindwa nitakuonyesha njia nyepesi kabisa za kuijua iphone halisi

Hizi njia zimegawanyika katika sehemu zifuatazo ambazo unaweza kuitumia moja wapo

Njia hizo inahusisha.

  1. Muonekano wa iphone
  2. Software za iphone
  3. Kutumia apps nje ya iphone
  4. Kutumia njia za online

Angalizo

Kabla hujaamua kununua iphone, jitahidi kufuatilia taarifa za hizo katika hasa kuhusu prosesa, memori, aina ya kamera, kioo, tabia za mfumo endeshi(iOS) na pia muundo halisi wa iphone origino

Ukielewa simu husika baada ya kufuatilia video mbalimbali na sifa za simu unaweza kuigundua iphone feki bila hata kuitazama kiundani

Hivyo kwa njia hizi chache utaigundua iphone feki mapema tu.

Muonekano wa iPhone

iPhone origino na feki mara nyingi hutofautiana katika muonekano hasa rangi ya bodi, muonekano wa skrini na pia hata kamera

iPhone feki rangi zake hazikolei kama ilivyo origino

Na muonekano wa logo ya apple vilevile haviendani

Kwa mfano picha ya juu mwanzoni, logo ya apple ya simu ya kwanza inang’aa kuliko  kuliko ya upande wa kulia ambayo imekolea weusi

Ya kushoto ni feki.

Pia tazama hii picha ya iphone 17 pro max feki na original

Ya kulia ni feki hata logo ya apple haionekani vizuri

Pia muonekano wa kamera wa iphone feki hufanana

Kamera zote lenzi zake huwa na ukubwa sawa tofauti na iphone orijino ya upande wa kulia picha ya kwanza na upande wa kushoto kwenye picha ya iphone 17 pro max

Muonekano wa skrini

Skrini inakupa utofauti wa wazi kati ya iphone orijino na feki

Itazame hii picha

fremu iphone

Na kisha tazama upande fremu  kushoto na kulia, juu na chini

Kwenye simu feki(kulia) kuna fremu ya rangi nyeusi pana inazunguka skrini

Hivyo skrini haikavi eneo lote hasa upande wa chini fremu ni pana

Wakati simu ya kulia(iphone orijino) skrini imekava kioo chote

Na upana wa fremu yenye rangi ni mwembamba na upo sawa kwenye pande zote

Software za iPhone

iPhone inatumia mfumo endeshi wa iOS na sio android

Hivyo apps za mfumo endeshi wa android hazifanyi kazi kwenye iPhone

Kwa mfano app ya kupakua apps mbalimbali kwenye iPhone huitwa App store

App store haipatikani kwenye android

Simu feki huweka mfano wa icon ya app store lakini huwa haifanyi kazi huwezi kuinstall app

google play store

Pia kwenye ya utiltity za simu feki utakuta app ya google play store

Kutumia apps za kutest simu

Moja ya njia nyingine rahisi zaid ya kugundua iphone feki ni kwa kutumia apps za kutest prosesa

Data za prosesa sio rahisi kuzichezea hasa spidi ya prosesa

App moja wapo nzuri kwa kazi hii ni CPU Z na geekbench

Ila inabidi ujue prosesa na spidi yake ya juu

Kwa mfano iphone 16 pro max prosesa yake ni Apple A18 Pro

Na spidi yake ya juu ni 4.05GHz na 2.42GHz na idadi ya core zipo sita

Taarifa hizi unaweza zipata kwenye gsmarena.com

CPU Z itakuonyesha taarifa zote na spidi inavyoenda kwa wakati kwa kila core(huandikwa cpu 0, cpu 1 nk)

Simu feki huwa kasi ya cpu haiwezi kuwa kubwa

Na huwa ndogo na huwa haibadiliki badiliki

Kwa hiyo spidi haiendani na cpu ilivyoainishwa basi jua hiyo simu feki

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company