SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

iPhone za bei rahisi za kumiliki kwa sasa(2024-2027)

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

June 29, 2024

Katika pitapita zangu na kuchunguza simu bora za bei ndogo na ya chini nimekuja kugundua kitu cha kustahajabisha kidogo

Wapenzi wa iPhone wenye bajeti ndogo wananunua iphone used hazipokei maboresho ya mfumo endeshi mpya wa IOS

Aina hii ya simu haipokei Whatsapp mpya na zingine kuanzia mwakani hazitokuwa zinapokea whatsapp mpya

Basi hii posti inaorodhesha simu za iphone za bei rahisi zinazofaa kununuliwa kwa mwaka 2024 kwenda mbele

Iwapo unataka kumiliki yenye kupokea iOS mpya basi fuatilia hapa

Usiishie hapo, fuatilia posti yote uone vitu vya muhimu vilivyopo kwenye hizi simu.

Apple iPhone 8

iPhone 8 ni simu ya mwaka 2017 ambayo bei yake ni shilingi 300,000 ya GB 64

Utendaji wa iPhone 8 unazipiku simu nyingi mpya za madaraja ya chini na ya kati

Kwani processor yake ya Apple A11 Bionic ina alama 935 kwenye ya Geekbench, alama ambazo hazifikiwi na chip ya Helio G99 iliyotumika kwenye simu za tekno spark za 2023.

iphone 8

Inapokea mfumo endeshi mwisho wa iOS 16.7.5, kumbuka iOS mpya ni iOS 18

Hata hivyo kiasi iOS 16 inakupa uhakika wa kuendelea kupata maboresho ya apps kwa miaka mingi

Betri yake sio kubwa kwani ina mAh 1821, ukaaji wa chaji sio wa kuridhisha pia chunguza kipengele hiki unaponunua kwa mtu

Kitengo cha kamera simu inaweza kurekodi video za 4K

Ila ubora wa picha sio mkubwa kivile.

Unapoikuza picha kuna chengachenga zinaonekana kwa wazi halafu kuna mwangaza mwingi(overexposure)

Hata hivyo kwa viwango vya simu za daraja la kati za sasa simu inapiga picha nzuri

Apple iPhone 8 Plus

Simu ya iPhone 8 Plus ilitoka mwaka 2017 kama iliyvo mtangulizi wake

Kwa sasa bei ya iPhone 8 Plus ya GB 64 ni shilingi 350,000

Na yenyewe inatumia chip ya Apple A11 Bionic hivyo utendaji ni mzuri pia

Yaani inaweza kusukuma gemu nyingi pasipo kukwama kwama

iphone 8 plus

Pia inapokea mpaka toleo la iOS 16.7.5

Ina kamera moja tu na ina OIS pia inatumia PDAF

Ubora wa picha pia ni wa kawaida, picha ni nzuri ila kuna changamoto zilezile za iphone 8

Apple iPhone X

iPhone X ilitoka rasmi mwezi novemba 2017 ikiwa ni boresho la matoleo ya iphone 8

Vitu vilivyoboreshwa ni skrini(kioo) , betri na kamera kama utakavyoona

Bei ya iPhone X ni laki sita ya GB 64 na unaweza ipata chini ya hapo

Inapokea hadi toleo la iOS 16 na haipokei toleo jipya la iOS 18

iphone x

Kumbuka iOS 16 inatosha sana kuipa simu thamani kwa miaka ijayo

Betri yake ni kubwa kidogo, ina mAh 2716

Simu za zamani afya ya betri hupungua kadri muda unavyoenda

Kuna maboresho makubwa sana kwenye kamera

Kwani kwa mara ya kwanza apple walianza kutumia ulengaji wa dual pixel kwenye kamera kuu

Hata hivyo ubora wa picha hauna tofauti kubwa na iPhone 8 au iPhone 8 Plus

Apple iPhone XR

Simu ya iPhone XR ni toleo la iPhone la mwaka 2018

Bei ya iPhone XR ni shilingi laki saba ila kwa mtu unaweza ipata hata kwa laki tano

Kwenye utendaji iPhone XR inaitoa inachuana na Samsung Galaxy A55

Hii inatokana na iPhone XR kutumia processor ya Apple A12 Bionic yenye alama 1290 kwenye Geekbench

iphone xr

Kwa maana iphone xr inaendana kiubora na matoleo yaliyotoka kati ya 2023 hadi 2024 ya daraja la kati

iPhone XR inapokea mpaka toleo jipya kabisa la iOS 18,thamani yake bado inaridhisha

Betri yake ni kubwa ya kukaa na chaji muda mrefu kwani ina mAh 2900

Ina kamera moja upande wa ubora maboresho yapo hasa kiwango cha noise ni kidogo

Apple iPhone XS

iPhone XS iitoka mnamo mwaka 2018

Bei yake ni shilingi laki sita ila kwa bei ya mkononi unaweza ipata kwa chini ya hapo

Utendaji una nguvu ya kufanya vitu kwa ufanisi kutokana na kutumia chip ya Apple A12 Bionic

Upande wa software, iPhone XS inaweza kupokea hadi iOS 18

iphone xs

Betri yake sio kubwa kama iPhone XR, ukubwa wake ni 2600mAh

Kamera yake inaweza kurekodi video za 4K

Hata hivyo ubora wa kamera ni mzuri ila sio wa kiwango kikubwa

Maana ukiikuza picha kuna chengachenga zinaonekana

Apple iPhone XS Max

Apple iPhone XS Max na yenyewe ilizinduliwa mwaka 2018, ni toleo bora kati ya matoleo ya iPhone X

Bei yake ni shilingi laki saba kwa hapa Tanzania

Processor inayotumia ni Apple A12 Bionic, nguvu yake ya utendaji ni kubwa

Inapokea hadi toleo la iOS 18 hivyo basi hata matoleo mapya ya app simu itakuwa inayapata kwa miaka mingi

iphone xs max

Betri ya iPhone XS Max na lenyewe sio kubwa kwani lina ukubwa wa 2600mAh

Ina kamera mbili zinazotumia ulengaji wa dual pixel pdaf na uwezo wa kurekodi video za 4K

Ubora wa picha ni mzuri japo noise zipo hata kwenye mwanga mwingi

Apple iPhone 11

Simu ya iPhone 11 ilitoka rasmi mwaka 2019, hili toleo lina ubora zaidi ukilinganisha na matoleo ya nyuma

Bei ya iphone 11 kwa mwaka 2024 ni shilingi laki nane yenye GB 128 na ikiwa ni used

iPhone 11 ina nguvu kubwa sana ya kuweza kufungua app ya aina yoyote bila kukwama

Hii inatokana na simu kutumia processor yenye nguvu, chip hiyo ni Apple A13 Bionic

iphone 11

Kuna app za kupima nguvu za processor ambazo ni Antuntu na Geekbench

Kwenye antuntu Apple A13 Bionic ina alama 870K, na geekbench inaonyesha chip inaweza kufungua kurasa 87 kwa sekunde bila kuganda

Hii ni namba kubwa, simu nyingi mpya za daraja la kati hazifikii kiwango hiki

Simu inapokea toleo jipya la iOS 18 na itapokea toleo litakalofuata

Ina betri yenye ukubwa wa 3110mAh

Kamera zake zinapiga picha nzuri na inajitahidi kuonyesha rangi kwa usahihi mkubwa

Apple iPhone 11 Pro

Apple iPhone 11 Pro na yenyewe ilitoka mwaka 2019 ikiwa na kamera tatu

Bei ya iPhone 11 Pro ni shilingi laki tisa na elfu ishirini

Utendaji wake una nguvu kwa sababu inakuja na chip ya Apple A13 Bionic

Kama ilivyo kwa iphone za mwaka 2018 kwenda mbele, iPhone 11 Pro inapokea toleo hadi la iOS 18

iphone 11 pro

Betri yake ina ukubwa wa 3046mAh

Kamera ya iphone 11 Pro inatoa picha nzuri hata katika ya mwanga hafifu

Moja ya kamera yake inatumia chip ya dual pixel pdaf na inaweza kurekodi za 4K kwa kiwango cha 60fps

Apple iPhone 11 Pro Max

Apple iPhone 11 Pro Max ni simu ya daraja la juu kwa mwaka 2019

Hivyo bei yake kwa wakati huo ilikuwa kubwa ila kwa sasa imeshuka

Bei yake pia inachagizwa na uwepo wa processor ya Apple A13 Bionic

Bei ya iphone 11 pro max ni milioni moja na laki tatu ila wapo wanaouza hadi laki tisa

iphone 11 pro max

Hii ikiwa na ukubwa wa GB 256

Ni iphone ya mwanzo kuja na betri kubwa

Betri yake ina ukubwa wa 3969mAh

Ubora wake wa kamera ni mkubwa ukizingatia moja lenzi yake ni ya optical lenzi

Hitimisho

Hizi ndizo iphone za kumiliki kwa sasa epuka kununua iphone ambayo haipokei maboresho ya iOS

Simu za iphone ni tofauti sana na simu za Android kutokana na kuwa na restrictions nyingi

Kwa kifupi acha kununua iphone inayoishia na mfumo endeshi wa iOS 12, UTANISHUKURU.

Maoni 4 kuhusu “iPhone za bei rahisi za kumiliki kwa sasa(2024-2027)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Google Pixel 9 na Sifa zake muhimu

Google Pixel 9 ni simu mpya kabisa ya pixel kwa mwaka 2024 Ni simu kali sana upande wa utendaji, kamera na software hasa katika matumizi ya AI(akili mnemba) Maboresho makubwa […]

thumbnail

[VIDEO]:Simu zote za iPhone za bei ndogo na zinazofaa

Kabla ya kununua iphone za bei rahisi ambazo mara nyingi huwa ni used, kitu cha kwanza cha kuangalia ni kama itakuwa inapata sapoti ya kupokea mfumo endeshi wa iOS Tofauti […]

[VIDEO]: Simu bora duniani na bei zake 2024

Huu ni muendelezo mwingine wa simu tano ambazo hazitumikii sana na watanzania. Lakini kiulimwengu ni kati ya simu bora duniani kwa mwaka 2024. Hizi ni simu zenye utendaji mkubwa kwenye […]

Simu bora duniani na bei zake 2024

Leo tuzungumzie kuhusu simu bora duniani na bei zake kwa mwaka 2024 Kuna matoleo mapya ya simu kali yenye ubora wa kiutendaji na wenye nguvu madhubuti katika maeneo mengi Ubora […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company