SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu za google pixel za bei rahisi zenye utendaji mzuri (2025)

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

May 10, 2025

Simu mpya za Google Pixel hupatikana kwa bei kubwa ambayo kwa Tanzania ni wachache wanayomudu

Simu za google pixel hutengeneza simu za madaraja ya juu kama uonavyo iPhone

Hivyo katika hiii orodha ya simu za bei rahisi za google pixel utakutana na simu used na sio mpya

Na used zenyewe ni matoelo ya zamani japo mengi yana ubora wa kushindana kwa nyakati za sasa

Simu zote zilizopo hapa zinauzwa chini ya laki tano

Fuatalia uone ipi ina sifa zitakazokidhi mahitaji yako kwa wakati huu na ujao

Google Pixel 4

Google Pixel 4 bei yake ni laki nne(400,000) na ilitoka rasmi mwaka 2019 ikiwa na Android 10

Toleo la mwisho Android simu itakayopokea ni Android 13

Ina kamera mbili zinazoweza piga video za 4K  na zinatumia ulengaji wa dual pixel pdaf

pixel4

Utendaji wake sio mkubwa kwa viwango vya sasa kwani inatumia processor ya Snapdragon 855

Changamoto utaipata upande wa betri kwani ina betri dogo

Ukubwa wa betri ni mAh 2800 na haizidi masaa 10 ukiwa unatumia simu muda wote mpaka chaji kuisha

Google Pixel 4a

Bei ya Google Pixel 4a ni shilingi 400,000 kama ilivyo kwa mtangulizi

Ilitoka mwaka 2020

Na yenyewe inapokea mpaka toleo la Android 13

pixel4a

Betri yake sio kubwa kwani ina mAh 3140 na kasi ya chaji yake ni wati 18

Inakuja na kamera moja na inaweza kurekodi video za 4K

Utendaji wake ni wa wastani sio mkubwa ukilinganisha na matoleo ya kati ya miaka hii

Google Pixel 5a

Bei ya Google Pixel 5a ni shilingi 500,000(laki tano) ni simu za awali za pixel kuwa na 5G

Utendaji ni wastani japo inaweza kufungua vitu vingi

Na simu inayokuja na mfumo wa eSIM

pixel5a

Ina kamera mbili na inaweza kurekodi video za 4K kwa kiwango cha 60fps

Betri yake ni kubwa kiasi ambayo ni 4680mAh

Ni sehemu yenye waterproof ya Ip67 ila hakuna uhakika kama waterproof itaendelea kuwepo kama simu iliwahi kufunguliwa

Google Pixel 3 XL

Google Pixel 3 XL ina miaka takribani minane tangu ilipotoka

Toleo la android la mwisho simu kupokea ni Android 12

Ina kamera moja tu inayoweza pia kurekodi za 4K

Ina utendaji wa wastani kwa sababu ya kutumia chip ya Snapdragon 845

Betri yake ina ukubwa mAh 3430 hivyo sio betri kubwa

Google Pixel XL unaweza ipata kwa shilingi 360,000

Google Pixel 3a

Google Pixel 3a ilitoka mwaka 2019 na inauzwa kwa kiasi cha shilingi 280,000

Ni simu inayokuja na RAM ya GB 4 na utendaji wake sio mkubwa kihivyo

Hii simu inapokea mpaka Android 12 hivyo android za mbeleni hutopata

Betri yake na yenyewe sio kubwa ina mAh 3000

Simu ina kamera moja tu na inaweza kurekodi video za 4K

Inasapoti laini za eSIM

Google Pixel 3

Google Pixel 3 inauzwa kiasi cha shilingi 300,000

Na ilitoka mwaka 2018 hivyo ina miaka saba tangu itoke

Hii simu ina kamera moja ila ina uwezo kuvutia

pixel3

Kwani inaweza kurekodi video za full hd kwa kiwango cha fps 120

Ila betri yake ni dogo kwani mAh 2915

Na yenyewe ina waterproof ya IP68

Google Pixel 6a

Iwapo matoleo ya awali hayajakuridhisha basi Google Pixel 6a ni mbadala sahihi zaidi

Inauzwa shilingi laki tano (500,000)

Simu inakuja na kamera mbili huku kamera mbili na zinaweza kurekodi video za 4k kwa kiwango cha 60fps

pixel6a

Utendaji wake ni mkubwa kwani inatumia chip ya Google Tensor

Betri yake ni kubwa kiasi kwani ina mAh 4410mAh

Kasi ya chaji yake ni wati 18

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

bei ndogo

Simu za laki tatu zenye ubora wa kuridhisha kwa 2025

Iwapo unapanga kununua simu chini ya laki tatu au zisizozidi laki nne usitarajie kupata simu yenye ubora mkubwa Kwa maana usitarajie kamera kali na utendaji mkubwa Ila kwenye hii post […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

huawei mate

Simu Bora 15 Duniani 2024 (na zitakazotamba 2025)

Kwa mwaka 2024, soko la simu janja yaani smartphone duniani lilitawaliwa na makampuni ya Apple, Samsung, Xiaomi, Vivo na Oppo Kwa hapa Afrika kampuni ya Samsung inaongoza kwa mauzo ikifuatiwa […]

samsung a06

[VIDEO]-ubora wa picha na kiutendaji wa Samsung Galaxy A06

Hii ni video inayokupa nafasi kushuhudia sifa za ziada za samsung galaxy a06 hasa upande wa kamera Kama hujui, Galaxy A06 NI simu mpya ya daraja la chini ambayo imetoka […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company