SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Spark 40 na Sifa zake muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

August 17, 2025

Simu mpya ya Tecno Spark 40 tayari imeingia sokoni

Kuna maboresho ila sina uhakika iwapo maboresho yake yanaweza mshawishi mtumiaji wa Spark 30 kutumia spark 40

Ukizingatia bei ya Tecno Spark 40 haitofautini sana na toleo lililopita

Wakati huo Spark 40 ikiwa imepunguzwa baadhi ya vitu

Kama una shauku ya kujua basi fuatilia posti yote

Bei ya Tecno Spark 40 ya GB 128

Spark 40 ya ukubwa huu inauzwa shilingi laki tatu na ishirini (320,000) kwa Tanzania

Hii ikiwa na ukubwa wa RAM ya GB 4

Tofauti na mwaka jana iliyokuwa na GB 8

Spark 40 ya gb 256 inaambatana na ram ya gb 8 ila bei yake ni 420,000

Kwa hiyo tathmini matumizi yako ufanye chaguo sahihi

Sifa za Tecno Spark 40

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G91
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.2 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) –  6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 15
  • HIOS 15
Memori 256GB,128GB na RAM 8GB,6GB,4GB
Kamera Kamera MOJA

  1. 50MP,PDAF(wide)
Muundo Urefu-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 5200mAh-Li-Po
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 320,000/=

Uwezo wa network

Tecno Spark 40 ni simy ya 4g haisapoti mtandao wa 5g

Na inatumia laini za kawaida kwa maana haina eSIM

Inatumia 4g aina ya lte cat 7 yenye kasi inayofika 300mbps

Ukiwa eneo lenye 4g+ unaweza kuifikia hii kasi

Hiyo itakusaidia kudownload kwa muda mfupi faili la gb kubwa

Hata hivyo inategemea mtandao unaotumia

Ubora wa kioo

Kioo Tecno Spark 40 ni cha ips lcd chenye refresh rate inayofika 120hz

Hii refresh rate inaifanya simu na mguso laini n wa haraka

Tofauti na spark 30 iliyokuwa na 90hz

Bahati mbaya ni kuwa kioo cha spark 40 kimenguwa resolution yaani ina 720p

Hivyo muonekano wa vitu haukolei sana na uangavu kidogo

Nguvu ya utendaji

Utendaji wa hii ni wa wastani kutokana na kutumia prosesa ya mediatek helio g91

Inafaa zaidi kwa matumizi ya kawaida kama whatsapp na hata kucheza gemu kwa settings za chini

Ukinunua yenye RAM ya gb 8 utendaji utaimalika kiasi fulani

Kwenye app ya geekbench hii chip ina alama 405

Ambayo kiuhalisia sio kubwa linapokuja swala la utendaji

Uwezo wa kamera

Hii simu ina kamera moja inayopiga picha na kurekodi video

Uubwa wake ni MP 50 na ina ulengaji aina PDAF

Ubora wa picha ni mzuri kwa maingira yenye mwanga mwingi

Na kamera inaweza kurekodi video za full hd

Software

Tecno Spark 40 inakuja na mfumo wa HIOS 15 ukiwa kwenye Android 15

HIOS 15 inakupa mifumo kadhaa ya AI kama vile circle to search, AI writing

Kwa maana utakuta kuna mifumo inayofupisha taarifa kuwa fupi

Hakuna taarifa kama itapokea toleo jipya la Android

Kwa sababu hata Tecno Spark 30 haijapokea Android 15

Neno la mwisho

Kama una simu ya tecno ya zamani sana, basi ukimiliki tecno spark 40 ni hatua kubwa

Ila kama una spark 30 toleo sahihi zaidi kumiliki ni Tecno Spark 40 Pro+

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company