Hapa utaenda kufahamu bei halisi ya Tecno mpya ya 2025
Tecno hiyo ni Tecno Camon 40 Pro ambayo imezinduliwa mwezi wa tatu
Camon 40 Pro inafanana kiasi flani na Camon 30 Pro ila Camon 40 ina vitu vingi vya kuvutia
Nadhani maboresho yake yanaweza kunyamazisha wanaoidharau Tecno
Hivyo ndio vitu utakavyoenda kuvifahamu kiundani ukisoma posti yote
Kaa mkao wa kula
Bei ya Tecno Camon 40 Pro ya GB 256
Tecno Camon 40 Pro yenye GB 256 na RAM ya GB 8 inauzwa shilingi laki sita (600,000)
Kwa Tanzania, hii inaweza ikawa bei kubwa
Lakini ukifuatilia sifa zake zilizoorodheshwa hapa utagundua kuwa ni bei sahihi
Na pia ipo yenye RAM ya GB 12, inafaa zaidi kama unatumia simu kwa vitu kwa wakati mmoja
Hivyo hutowaza simu kukwama kwama
Sifa za Tecno Camon 40 Pro
Sehemu Za Simu | Sifa za Simu |
---|---|
Network | 2g, 3g, 4g and 5g |
Processor(SoC) |
|
Display(Kioo) | AMOLED, Refresh rate:144Hz |
Softawre |
|
Memori | 256GB na RAM 8GB,12GB |
Kamera | Kamera MBILI
|
Muundo | Urefu-6.78inchi |
Chaji na Betri |
|
Bei ya simu(TSH) | 600,000/= |
Uwezo wa network
Tecno Camon 40 Pro inasapoti mtandao wa 5G
Haina laini za eSIM hivyo utatumia laini za siku zote
Kasi yake ya kudownload inafika zaidi ya Mbps 3000
Ila mitandao mingi hapa haisapoti kasi hiyo
Masafa yake yanakubali mitandao yote ya simu hapa nchini
Ubora wa kioo cha Tecno Camon 40 Pro
Muonekano wake wa kioo ni muundo wa curve(muundo wa upinde) kushoto na kulia
Inatumia kioo cha AMOLED ambacho kina refresh rate ya 144Hz
Hii inafanya kuwa ni kioo kizuri sana kwenye kucheza magemu
Lakini kiwango cha refresh rate hii ni kama cha toleo lililopita
Kingine simu ina skrini protekta ya Gorilla glass 7i
Hiki ni kioo kimeundwa kuhimili mipasuka simu inapodondoka
Nguvu ya processor (Dimensity 7300)
Tecno Camon 40 Pro inatumia chip ya dimensity 7300
Ni chip ambayo imegawanyika katika sehemu mbili
Ambapo sehemu yenye nguvu kubwa ina muundo wa Cortex A78
Utendaji wake ni wa wastani unaoweza kusukuma vitu vingi pasipo na tatizo
Kwa bahati mbaya utendaji wake sio mkubwa kama chip ya Dimensity 8200
Dimensity 8200 ilitumika kwenye simu ya Tecno Camon 30 Pro
Uwezo wa betri na chaji
Simu inakuja na betri ya ukubwa wa 5200mAh
Na chaji yake inasapoti umeme wa wati 45
Chaji ya aina hii hujaza simu kwa haraka chini ya lisaa limoja na nusu
Ukiwa unacheza gemu muda wote pasipo kupumzika, simu inachukua kama masaa 8 kuisha chaji
Na kwa matumizi ya kawaida inachukua mpaka masaa 14
Kwa betri kubwa kama hii chaji yenye kasi ni muhimu kujaza betri kwa haraka
Uimara wa bodi ya Tecno Camon 40 Pro
Kwa mara ya kwanza Tecno wameto simu imara kuzuia maji yasiingie ndani ya simu kama ikizama kwenye maji mengi
Kwa sababu ina waterproof aina ya IP68
IP68 inamaanisha kuwa simu inaweza KUHIMILI kuzuia maji kwa muda wa nusu saa katika kina cha mita mbili
Ni kimo kama diaba la maji
Kwenye maduka ya tecno utaona jinsi simu inavyohimili kuzuia maji maana huonyesha wateja
Ubora wa kamera
Kamera zake zipiga vizuri hasa kwenye mwanga mwingi kwa picha ambazo nimeziona zilizopigwa na hii simu
Lakini usahihi wa rangi sio mkubwa sana
Maana kwa mtu mweusi ni kama kamera inaongeza mng’ao
Kwa wanaopenda effect za namna hii wanaweza kuona kuwa picha ni nzuri na ipo sawa
Kiujumla ina kamera mbili mojawapo ni ya ultrawide
Mifumo yake haina mambo mengi ya ziada kama dual pixel pdaf
Na inaweza kurekodi video za 4K kwa kiwango cha 60fps
Ubora wa Software
Kwenye software Tecno wamefanya maboresho makubwa mengi
Maboresho hayo yamejikita zaidi katika matumizi ya AI
Ukiwa na hii Tecno utaweza kutumia mfumo wa Circle to search
Yaani endapo umekutana na picha na katika picha kikawepo kitu ambacho hukijui ila unataka kujua taarifa zake
Mfumo unakurusu kuzungushia duara hiko kitu na kisha google inakupa taarifa
Pia ina mfumo wa kuondoa “background noise” wakati ukiwa unaongea na mtu kwenye simu
Yaani ukiwa kwenye mazingira ya kelele, simu itaondoa hizo kelele ili kuwasiliana kwa usikivu
Washindani wa Tecno Camon 40 Pro
Washindani wakubwa kwa kutazama simu ni Redmi Note 14 Pro na Samsung Galaxy A56
Redmi inatumia processor moja na Camon 14
Ila redmi inasapoti laini ya eSIM pia
Lakini pia ina kamera yenye megapixel 200
Na kioo chake kina teknolojia ya HDR10+ na Dolby Vision
Na samsung sifa zake unaweza kuziona hapa: Ubora wa samsung galaxy a56
Hizo simu mbili na zingine zinaweza iletea hii simu changamoto
Neno la mwisho
Tecno camon 40 pro ina maboresho mengi zaidi kwenye upande wa software
Ila ukilinganisha na Tecno Camon 30 Pro utaona utendaji wa camon 30 pro kuwa ni mkubwa
Pia kwenye idara yake ina washindani wengi wenye simu nzuri pia
Na boresho kubwa zaidi ni uwepo wa IP68 ambayo inafaa sana kwa ulinzi wa simu na maji