Infinix wametoa matoleo mapya na yameshaanza kupatikana Tanzania
Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 50 ambayo ina maboresho upande wa software, kioo na uimara wa simu kiujumla
Kwa sifa zake za ziada imepelekea bei yake kuongezeka kidogo ukilinganisha na Infinix Note 40 ya 2024
Na pia ina toleo la aina moja upande wa memori
Bei ya Infinix Note 50 ya GB 256
Kwa Tanzania Infinix Note 40 inauzwa shilingi laki sita na elfu sitini (660,000)
Hii ikiwa na RAM ya ukubwa wa GB 8
Hakuna aina nyingine ya RAM matoleo yote yana RAM ya GB 8
Pia mfumo wake wa memori ni aina ya UFS 2.2
Ni vizuri ukazielewa sifa za Infinix Note 40 kisha ukalinganisha na bei yake kujua kama zinashahabiana
Sifa za Infinix Note 50
Sehemu Za Simu | Sifa za Simu |
---|---|
Network | 2g, 3g, 4g |
Processor(SoC) |
|
Display(Kioo) | Amoled, Refresh rate:120Hz |
Softawre |
|
Memori | UFS 2.2,256GB na RAM 8GB |
Kamera | Kamera MBILI
|
Muundo | Urefu-6.78inchi |
Chaji na Betri |
|
Bei ya simu(TSH) | 660,000/= |
Uwezo wa network
Infinix Note 50 ni simu inayosapoti mtandao wa 4G haina 5G
Aina ya 4G inayosapti ni LTE Cat 13
LTE Cat 13 inaweza kupakua kitu kwa spidi inayofika 650Mbps
Ni kasi kubwa kama mtandao wa simu utakuwa una nguvu hiyo
Kwa wanaopenda eSIM, Note 50 haina huo mfumo bali inatumia laini za kawaida
Ubora wa kioo cha Infinix Note 50
Kioo cha hii simu ni cha aina ya Amoled
Refresh rate yake inaweza kufika hadi 144hz
Refresh rate kubwa hufanya simu kuwa na mwitikio na muonekano mzuri unapokuwa una-scroll na hata wakati wa kucheza gemu
Hata hivyo si mara zote utahitaji kutumia refresh rate kubwa
Uangavu wake kwenye kuonyesha vitu unafika nits zaidi ya 2000
Hivyo ukiwa maeneo ya juani bado utaweza kuona kwa uzuri
Nguvu ya processor ya Mediatek Helio G100 Ultimate
Chip ya Mediatek helio g100 ultimate ina nguvu ya wastani
Inaweza kufanya vitu vingi pasipo kukwama kwama
Kwenye geebench inaonyesha helio g100 ultimate inaweza kufungua kurasa zaidi ya 50 kwa sekunde
Haina tofauti kubwa sana na processor ya Snapdragon 4 gen 2 iliyotumika kwenye simu za Redmi Note 12R ya 2023
Hii chip ina sehemu mbili zilizotengwa kwa kufanya kazi zinazohitaji kazi kubwa
Sehemu zinatumia muundo wa Cortex A76
Uwezo wa betri na chaji
Betri ya Infinix Note 50 ina ukubwa wa mAh 5200
Ni betri kubwa inayoweza kukaa na chaji muda mrefu
Chaji yake inapeleka umeme wa wati 45
Hii inamaanisha chaji yake inawahi kujaa chaji ndani ya dakika 80 kutoka 0%
Hii simu inaweza kuchajiwa kwa njia ya wireless kwa kasi ya wati 30
Uimara wa bodi
Infinix Note 50 ina waterproof aina ya IP64
IP64 humaanisha simu inaweza kuzuia maji ya kiwango cha kunyululuzika na pia kuzuia vumbi
Ni tofauti na IP67 ambayo simu inaweza zama kwenye maji na ikanusurika
Lakini IP64 unaweza ukaitumia wakati mvua inanyesha na sio kuzama kina kirefu
Ubora wa kamera
Infinix Note 50 ina kamera mbili zenye megapixel 50 na 2
Kmaera kubwa inajitahidi kupiga picha vizuri
Kwenye mwanga wa kutosha muonekano wa vitu mzuri kiasi
Kitu kimoja kinachoweza kisifurahishe baadhi ni mkorezo mkubwa wa rangi
Lakini kuna mazingira uhalisia wa rangi unapungua hasa mwanga wa jua ukiwa mkubwa
Hata hivyo ni kamera nzuri yenye ubora wa wastani
Ubora wa Software
Infinix Note 50 inakuja na Android 15 na itapata matoleo mapya ya android kwa muda wa miaka miwili
Mfumo mwingine ambao utakupatia mifumo mingi ya AI(akili mnemba) ni XOS 15
Kuna mifumo ya AI ipatayo 10 kwneye hii simu
Baadhi ni circle to search, kufupisha taarifa ya kitu, kuondoa kelele wakati wa mawasiliano kwa njia ya simu
Simu nyingi za madaraja ya kati hutoa mifumo ya AI michache ila infinix inayo mingi
Washindani wa Infinix Note 50
Kuna Tecno Camon 40 ambayo bei yake ni sawa na hii infinix
Camon 40 na Infinix 50 ni kama simu moja maana zinafanana vitu vingi mno
Mshindani mwingine ni Samsung Galaxy A16 na Redmi Note 14 4G
Hizi zote zina utendaji unaofanana na bei zake sio kubwa
Kwa kifupi washindani ni wengi katika kipengele hiki cha matoleo ya daraja la kati
Neno la Mwisho
Kwa kuzingatia sapoti ya software ya miaka miwili, bei ya infinix note 50 ina haki kuwa hivyo
Kutoa update maana yake kuna watu wanafanya maboresho ya simu kwa kutazama changamto zinazojitokeza
Kwa hiyo kuna gharama pia ya kutoa update ndio maana simu za bei ndogo sana hazina update
Mbali na hayo ni vizuri infinix wakaanza kuwezesha video za 4k kwenye simu za matoleo ya Note