SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Infinix Note 40 Pro na Sifa zake muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

September 3, 2024

Unataka simu nzuri ya Infinix?

Ni infinix note 40 pro iliyotoka mwaka 2024 mwanzoni mwa mwaka

Ila sasa bei yake ni shilingi milioni moja na laki moja ikiwa na ukubwa wa GB 256

infinix note 40 pro showcase

Ubora mkubwa wa Infinix Note 40 Pro upo kwenye skrini, utendaji, betri pamoja na chaji

Tupitie kipengele kimoja baada ya kingine uone ubora mkubwa wa infinix note 40 pro

Sifa za Infinix Note 40 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Dimensity 7020
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.2GHz Cortex A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0GHz Cortex A55
  • GPU-IMG BXM-8-256
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
  • XOS 14
Memori  256GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 2MP
  3. 2MP
Muundo Urefu-6.78inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 1,100,000/=

Uwezo wa network

Kwanza hii simu inatumia laini za kawaida yaani haitumii muundo wa laini za eSIM

Inasapoti mtandao wa 5G hivyo kama upo kwenye maeneo ya 5G utakuwa unapata kasi kubwa ya kupakua vitu

Uzuri ni kwamba inasapoti 5G za aina zote yaani SA na NSA

Kama mtandao una miundombinu ya SA 5G utapata 5G ya ukweli na yenye kasi

Kwa hapa Tanzania NSA ndio inayotumika zaidi kutokana na SA kuwa na gharama kubwa na ni teknolojia mpya inayohitaji vifaa vipya kabisa

Upande wa 4G, kasi yake inafika ziaidi Mbps 2000

Lakini kuipata spidi hii inategemea sana na uwezo wa mtandao husika ambapo kwa Tanzania ni changamoto

Ubora wa kioo cha Infinix Note 40 Pro

Kioo cha Infinix Note 40 Pro ni angavu sana kwani kina nits 1300

Kinaruhusu kutumika kwenye mazingira yoyote na vitu vikaonekana kwa uzuri

Ni cha aina ya amoled chenye refresh rate ya 120Hz

infinix note 40 pro display

Refresh rate kubwa hufanya kioo kuwa fasta na chepesi

Na amoled utajiri wa rangi ni mkubwa na rangi za vitu huonekana kwa usahihi ukilinganisha na  vioo vya LCD

Nguvu ya processor Mediatek Dimensity 7020

Kwanza Infinix Note 40 Pro ina ufanisi mzuri wa matumizi ya betri kwa sababu ya aina ya processor iliyotumika

Processor hiyo mediatek dimensity 7020

Dimensity 7020 ina core mbili zilizoundwa kufanya kazi kubwa lakini kwa matumizi madogo ya umeme

Sehemu(core) hizo ni Cortex A78, na core sita zilizobaki ni aina ya Cortex A55 kwa ajili ya kazi zisizohitaji nguvu kubwa kama kutuma meseji kupiga simu nk.

infinix note 40 pro chip

Kwenye app za kupima uwezo wa procesor, dimensity 7020 ina alama za kuridhisha

Katika vipimo vya antutu, chip ina alama 470,000

Na geekbench, chip ina alama 884, simu za madaraja ya chini huwa na alama za chini zaidi

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Infinix Note 40 Pro ina ukubwa wa mAh 5000

Hivyo ukaaji wa chaji ni wa kuridhisha

Simu inaweza kuchajiwa kwa njia mbili

Na zote zinaweza kujaza betri hii kubwa kwa haraka ndani ya muda mfupi

infinix note 40 pro chaji

Yaani simu inaweza chaji kwa njia ya waya au bila waya(wireless)

Chaji ina kasi ya kupeleka umeme wa wati 45 ambayo inaweza kujaza betri kwa 100 ndani ya dakika 70

Na wireless kasi yake ni  wati 20

Hii ni tofauti na simu nyingi ambapo wireless chaji huwa na kasi ndogo

Ukubwa na aina ya memori

Hii simu inatumia memori za muundo wa UFS ambao huwa na kasi kubwa sana ya kusafirisha data

Na kuna toleo la aina moja tu upande wa memori

Ambapo utapata yenye ukubwa wa GB 256

Na ram ya GB 8

Huu ukubwa unafaa na kutosheleza kuhifadhi mafaili mengi

Uimara wa bodi ya Infinix Note 40 Pro

Infinix wameendelea kuboresha simu wanazoziingiza sokoni

Kwa matoleo mengi ya nyuma infinix hazikuwa na viwango vya IP

Viwango vya IP huashiria uwezo wa simu kuzuia maji

Ila toleo la Infinix Note 40 Pro linabainisha kuwa na waterproof ya IP53

IP53 inaashiria uwezo wa simu kuzuia maji ya kiwango cha kunyunyuluzika

Tofauti na IP67/IP68 ambavyo vinabainisha simu kutopitisha maji hata ikizama kwenye kina cha mita 1.5 kwa muda wa nusu saa

Labda matoleo yatakayofuata yatakuja na waterproof imara zaidi

Ubora wa kamera

Kama umesoma mwanzo mwisho utaona infinix note 40 pro ubora wake ni mkubw maeneo mengi

Ila kwenye kamera kuna vitu vinakosekana ukilinganisha na bei yake

Kwanza ina kamera tatu huku kamera mbili zina megapixel 2 tu

Na pia kamera mbili hazijurikani ni za aina gani bali kamera moja ya megapixel 108 ina lenzi ya wide

infinix note 40 pro camera

Hii ndio kasoro kubwa ninayoiona

Kamera kuu upigaji mzuri hasa kwenye mazingira yenye mwanga wa kutosha

Ila haiwezi kurekodi video zenye resolution za 4K

Hii inasababishwa na uwezo wa processor kuwa mdogo kwenye kuchakata video za resolution kubwa

Ubora wa Software

Infinix Note 40 Pro inatumia mfumo endeshi wa Android 14 na XOS 14

Kuna vitu vingi vimeongezwa kwenye XOS 14

Kimoja wapo kizuri ni uwezo wa kutumia app mbili kwa wakati mmoja

Yaani unaweza ukaigawanya skrini katika mbili, ya juu na ya chini

Sehemu ya juu ukawa unaangalia youtube, na sehemu ya chini ukawa unasoma whatsapp

Hii inaitwa dual app

Washindani wa Infinix Note 40 Pro

Mshindani wa kwanza ni toleo la Samsung Galaxy A54 na pia Samsung Galaxy A55

Samsung Galaxy A55 ina ubora mwingi unaoizidi Infinix kwenye kila eneo

Pia kamera za samsung zipo tatu zinazoweza kurekodi video za 4K

Moja ya kamera zake ni ya ultrawide

Pia A55 ina skrini ya hdr10+ na waterproof ya IP67

sasmunga55

Waki huo bei ya Samsung Galaxy A55 ni chini ya milioni moja

Simu mbadala nyingine ni Redmi Note 13 Pro

Redmi Note 13 Pro ina kioo kizuri chenye dolby vision, utendaji wenye nguvu kuliko infinix

Na Redmi Note 13 Pro inauzwa kwa bei ya chini ya laki nane

redminote13pro

Na simu kali nyingine ambayo infinix note 40 pro haifui dafu ni OPPO Reno11 Pro

Bei ya OPPO Reno11 Pro inaendana na hii infinix

Kiujumla kwa aina ya bei, simu hii ya infinix inajiingiza katika kundi lenye simu nyingi kali

Neno la Mwisho

Bei ya Infinix Note 40 Pro inaashiria wazi kuna ubora mkubwa ukilinganisha na simu za matoleo ya Smart au Hot

Pamoja na hayo maboresho, kuna baadhi ya maeneo simu ilihitaji kuwa na maboresho zaidi ili kuendana na ushindani na simu zingine za namna hiyo.

Hata hivyo kwa mtumiaji na pia kwa asiependa infinix ataona utofauti mkubwa na matoleo ya nyuma ya infinix

Ni matumaini hii simu itakuwa inapokeo maboreshi ya mfumo mpya wa Android kwa miaka kadhaa

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix note 40 pro thumb

[VIDEO]-Ubora wa Kamera, uimara wa kuzuia maji, sifa na bei ya Infinix Note 40 Pro

Tazama uwezo wa Infinix note 40 pro katika kuzuia majia na pia ubora katika vipengele vingine vya hii simu na sifa zake zote muhimu

tecno camon 30 thumb

Bei ya Tecno Camon 30 Pro na Sifa Muhimu

Simu ya Tecno Camon 30 Pro ilitangazwa mwezi februari ila imetoka rasmi mwezi wa nne 2024 Ni simu ya daraja la kati(midrange) hivyo bei yake sio sawa na Tecno matoleo […]

infinix thumbnail

Simu mpya za Infinix (Matoleo ya 2024)

Tangu kuanza kwa mwaka 2024 kampuni ya Infinix zimeingiza sokoni takribani simu nane Katika mrorongo wa simu mpya za infinix na tecno yapo matoleo ya daraja la chini na daraja […]

tecno camon 30 premier thumbnail

Bei ya Tecno Camon 30 Premier 5G na Sifa zake muhimu

Kwenye matoleo bora ya simu kutoka Tecno, matoleo ya Tecno Camon huja na ubora katika vipengele vingi Hata bei za matoleo ya Camon huzizidi bei za Tecno Spark na Tecno […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company