SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Google Pixel 9 na Sifa zake muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

August 18, 2024

Google Pixel 9 ni simu mpya kabisa ya pixel kwa mwaka 2024

Ni simu kali sana upande wa utendaji, kamera na software hasa katika matumizi ya AI(akili mnemba)

Maboresho makubwa yamekuja na bei kubwa pia ukilinganisha na pixel za miaka ya nyuma wakati wa uzinduzi

Kwani bei ya Google Pixel 9 ya GB 128 inauzwa kwa zaidi ya shilingi milioni mbili na laki mbili kwa bei rasmi kutoka google

Hivyo basi kwa Tanzania bei yake inaweza kuzidi milioni 2.5

Swali la kujiuliza, kuna vitu gani hasa vinavyopelekea pixel 9 kuuzwa  bei kubwa

Hii posti inajibu hilo kwenye upande wa sifa za simu hii.

Sifa za Google Pixel 9

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Google Tensor G4
  • Core Zenye nguvu ya ziada(1) – 1×3.1 GHz Cortex-X4
  • Core Zenye nguvu(3)-3×2.6 GHz Cortex-A720
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.92 GHz Cortex-A520
  • GPU-Mali-G715 MC7
Display(Kioo) OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
Memori UFS , 256GB,128GB na RAM 12GB
Kamera Kamera mbili

  1. 50MP,dual pixel PDAF(wide)
  2. 48MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.3inchi
Chaji na Betri
  • 4700mAh-Li-Po
  • Chaji-27W
Bei ya simu(TSH) 2,500,000+/=

Uwezo wa network

Google Pixel 9 ni simu ya 5G inayosapoti laini aina za eSIM

Kwa sasa kampuni zinazosapoti eSIM kwa Tanzania ni Airtel, Vodacom na TTCL

Simu inasapoti aina zote  za 5G ikiwemo mmWave ambayo ndio yenye kasi kubwa zaidi

Pia 4G inasapoti masafa mengi hivyo hata kwa hapa Tanzania simu inaweza kutumika bila tatizo

Ubora wa kioo cha Google Pixel 9

Google Pixel 9 inakuja na kioo cha OLED chenye resolution ya 1080 x 2424 pixels

Ni resolution kubwa ambayo, na pia skrini yake inaongezewa ubora na uwepo HDR10+

HDR10+ inaongezea skrini kina cha rangi

Hivyo vitu vingi vinakuwa na muonekano mzuri wenye usahihi mkubwa wa rangi

Kwa wapenzi wa gemu watafurahia kutumia hii simu kwa sababu skrini ina kiwango cha refresh rate 120hz

Kiwango kikubwa cha refresh rate kinaifanya skrini ku-sense kwa haraka na smooth wakati unapoperuzi

Kiujumla kioo cha google pixel 9 kina ubora mkubwa na pia ni cha gharama

Nguvu ya processor Google Tensor G4

Simu inatumia processor ya Google Tensor G4 ambayo ni mpya

Pamoja na upya wa hii chip, kiutendaji inaachwa na chip za mwaka jana snapdragon 8 gen 4 na hata Apple A17 Pro

Ikumbukwe kuwa Tensor G4 imetengenezwa kwa ushirikiano na kampuni ya Samsung

Naweza sema Google Tensor G4 ni Exynos 2400 ya Samsung

Mbali na hayo, hii processor ina nguvu ya kufanya vitu vingi bila tatizo

Hii inatokana na core yenye nguvu kubwa sana kuundwa kwa muundo wa Cortex X4

Kiutendaji Cortex X4 imeongezeka kwa asilimia 15 ukilinganisha na muundo wa Cortex X3

Uwezo wa betri na chaji

Hii simu unaweza kuichaji kwa kutumia waya au bila waya kwa maana “wireless”

Na kiwango cha umeme kinachoweza kuingia ni wati 27

Kimakadirio, betri yake inaweza kuchukua takribani dakika 85 mpaka kujaa kwa 100%

Kitu kimoja cha kuangalia.

Ukubwa wa betri, betri ina kiwango cha 4700mAh

Japo ipo chini kidogo ya viwango vya betri nyingi ila kiwango hiki kinaweza kukaa na chaji hata kwa angalau masaa 11 ukiwa kwenye intaneti muda wote

Aina ya chaji ya hii simu ni usb type c

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo mawili tu upande wa memori ambayo yana ukubwa GB 128 na GB 256

RAM za simu ukubwa wake ni GB 12

Hii simu ina mifumo ya AI mingi ambayo kiujumla inahitaji memori kubwa

Ndio maaana inaambatana na RAM kubwa kwa ufanisi mzuri wa AI

Pia muundo wake wa memori ni wa UFS ambao kasi ya kusafirisha data ni kubwa

Uimara wa bodi ya Google Pixel 9

Bodi ya Google Pixel 9 imeundwa na bodi yenye waterproof aina ya IP68

Hii inamaanisha iwapo simu itazama kwenye kina cha mita 1.5 kwa muda wa nusu, maji hayataingia

Hali hii inakupa uhuru wa kutumia simu hata kwenye mazingira yenye unyevu unyevu

Kwenye ulinzi wa skrini, pixel 9 inakuja na vioo vya gorilla victus 2

Kampuni ya corning glass, inasema vioo vya gorilla victus 2 vinalenga kuzuia simu kupasuka pindi simu ikianguka katika uso wa ardhi ambao ni rahisi kioo kupasuka

Na pia ina uimara kwenye mikwaruzo

Kiujumla bodi ya simu ni nzuri ya kuweza kudumu kwa muda mrfu

Ila tu umakini unatakiwa katika mazingira yote

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera zipatazo mbili

Kamera zote zinatumia ulengaji wa dual pixel pdaf

Na kamera kubwa inaambatana na laser af, laser af mara nyingi hutumika zaidi nyakati za usiku

Kuhusu ubora wa picha, kamera kuu inapiga picha vizuri

Usahihi wa rangi ni mkubwa na dynamic range inafanya kazi kubwa sana katika utofautishaji wa rangi

Kwa kiasi kubwa kamera inapiga picha zenye muonekano halisi kwa sehemu kubwa

Upande wa video, kamera ya google pixel inaweza kurekodi mpaka video za 4K

Ubora wa Software

Google Pixel 9 inakuja na Android 14

Kitu kikubwa kinachopatikana kwenye software ni ongezeko la matumizi ya Artificial Intelligence

Hili unaweza kuliona kwa uwepo wa chatbot ya Gemini ambayo ni mshindani chatgpt

Pia kuna matumizi ya AI upande wa kamera

Kwa mfano mpo watu wawili na mnataka mpige picha ya pamoja mtakayotokea wote wawili

Camera ya pixel inakupa hiyo nafasi, kwa kuanza unapiga picha ya kwanza.

Halafu unatoka kwenye kamera kisha unaenda kupigwa picha wewe

Baada ya muda app inaunganisha picha zote mbili, na kuonekana kama ilipigwa kwa wakati mmoja

Washindani wa Google Pixel 9

Kwa kuwa Google Pixel 9 ni simu ya daraja la juu, washindani wake moja kwa moja watukuwa ni Samsung Galaxy S24, Apple iPhone 15

Pia Oppo matoleo ya find x, na baadhi ya simu za Xiaomi bila kusahau oneplus

Changamoto kubwa Google Pixel 9 anayoipata mbele ya washindani wake ni utendaji

Simu nyingi za Android za daraja la juu zinatumia processor ya Snapdragon 8 Gen 4

Tayari utendaji wa Snapdragon 8 Gen 4 ni mkubwa sana ukilinganisha na Google Tensor G4

Na bado kumekuwa na malalamiko juu ya kuzidi kwa joto unaosababishwa na chip ya tensor g4

Kwa bahati mbaya kuna mfanano wa bei na hizo simu

Neno la Mwisho

Bei ya Google Pixel 9 ni kubwa unapolinganisha kipato cha watanzania wengi

Pamoja na bei kuwa kubwa ubora wa simu pia ni kiwango katika maeneo mengi

Kuanzia kamera, uimara wa bodi, chaji na betri, na pia software na kamera ni balaa tupu

Kama unapenda kupiga sana picha google pixel ni toleo la kuipa kipaumbele

Iko vizuri zaidi katika kipengele hiko.

Wazo moja kuhusu “Bei ya Google Pixel 9 na Sifa zake muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

pixel 9 pro fold

Simu Mpya za Google Pixel 2024 na bei zake

Kuna matoleo yapatayo manne ya simu mpya za google ambayo yametoka mwaka 2024 Matoleo yote yanatofoautiana kwa kiasi fulani kwenye muundo na baadhi ya vitu kama utakavyoona Hivyo, bei zake […]

iphone thumbnail

iPhone za bei rahisi za kumiliki kwa sasa(2024-2027)

Katika pitapita zangu na kuchunguza simu bora za bei ndogo na ya chini nimekuja kugundua kitu cha kustahajabisha kidogo Wapenzi wa iPhone wenye bajeti ndogo wananunua iphone used hazipokei maboresho […]

[VIDEO]: Simu bora duniani na bei zake 2024

Huu ni muendelezo mwingine wa simu tano ambazo hazitumikii sana na watanzania. Lakini kiulimwengu ni kati ya simu bora duniani kwa mwaka 2024. Hizi ni simu zenye utendaji mkubwa kwenye […]

pixel 8a thumbnail

Bei ya Google Pixel 8a na Sifa zake Muhimu

Kwenye mlolongo wa matoleo ya Google Pixel 8, Google Pixel 8a ndio ina bei ndogo zaidi Bei ya Google Pixel 8a ya GB 128 ni shilingi za tanzania milioni moja […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company