Simu ya Sony iliyotoka mwaka huu 2025 ni Sony Xperia 1 VII
Bei yake unaijua ni shilingi ngapi? ni milioni nne na laki tano huko duniani
Ni bei kubwa sana na simu nyingi za sony zinauzwa kwa bei za viwango hivyo
Kwenye hii post utazioana simu za sony xperia za bei rahisi ambazo wengi wanaweza kuzimudu
Hata hivyo simu zote ni za zamani hivyo utapata ikiwa imeshatumika (sawa na kubeti)
Hizi ndizo simu zenyewe za sony
Sony Xperia 5
Bei ya Sony Xperia 5 ni shilingi 320,000 (laki tatu)
Utendaji wake ni wa wastani na baadhi ya simu mpya za matoleo ya kati zinapittwa na xperia 5
Simu hii ina kamera tatu na zinatoa picha nzuri na inaweza kurekodi video za 4K
Ni nadra kupata simu ya laki tatu yenye kamera ya 4K kwa sasa, ila hii ni ilitoka 2019
Upande wa software, simu inapata mpaka toleo la android 11 wakati kwa sasa kuna android 14
Kikubwa zaidi kuhusu hii simu ina kioo cha oled, na waterproof aina ya IP68
Sony Xperia L4
Sony Xperia L4 inauzwa shilingi 300,000 kwa ya GB 64
Ilitoka rasmi mwaka 2020
Haina utendaji mkubwa ukilinganisha na simu Sony Xperia 5
Kwa sababu processor yake ya Helio P22 haiwezi kusukuma vitu vingi vikubwa
Ndio maana hata kamera zake zinaweza kurekodi video za full hd kwa kiwango cha 30fps
Betri yake sio kubwa sana ina mAh 3580, kwa sasa betri nyingi zina ukubwa wa mAh 5000
Simu haina uwezo wa kupata android nyingine mbali na ile inayokuja nayo ambayo ni Android 9 (Pie)
Sony Xperia 5 II
Sony Xperia 5 II ni simu ya mwaka 2020, ila ina vitu vingi ambavyo vyenye hadhi hata kwa sasa
Cha ajabu, bei yake ni shilingi laki tatu na themanini (350,000)
Sifa zake nzuri ni hizi, kioo chake ni cha oled chenye refresh rate ya 120hz
Kamera zinapiga picha zenye muonekano mzuri hata kwenye mazingira yenye mwanga hafifu
Na zinaweza kurekodi video za 4K kwa kiwango cha 120fps
Hiki ni kitu kisichopatikana hata kwa simu za madaraja ya kati kama Samsung Galaxy A36
Changamoto ni kuwa inapokea toleo la android 12 pekee
Na betri yake ina mAh 4000 ambayo ni ndogo kwa viwango vya sasa
Sony Xperia 10 III Lite
Sony Xperia 10 III Lite ni simu ya mwaka 2021, ina miaka minne tangu itoke
Bei yake kwa Tanzania inapatikana kwa kiasi cha shilingi laki nne (400,000)
Ni simu ya kamera tatu yenye utendaji wa wastani
Kwani inatumia chip ya Snapdragon 695 5G
Tukirudi upande wa kamera, kamera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa kiwango cha 30fps
Betri yake ni kubwa kidogo ina mAh 4500
Inaweza kupata hadi Android 13
Sony Xperia 1 III
Kwenye hii orodha ya sony za bei rahisi hii ndio ina bei kubwa
Lakini ndio sony experia yenye uwezo mkubwa na ilitoka 2021
Utendaji mkubwa unachabgiwa na utumiaji wa processor ya Snapdragon 888 5G
Sony Xperia 1 III inauzwa shilingi laki saba (700,000) na imekamilika kila idara
Mfano upande wa kamera, kuna kamera tatu aina ya wide, telephoto na ultrawide
Kamera zote zina mfumo wa ulengaji wa kiutomaki wa dual pixel pdaf
Kutokana na nguvu kubwa kamera yake inaweza kurekodi video za 4k kwa kiwango cha 120fps
Chaji yake ina ukubwa wa mAh 4500 na chaji ya wati 30, na kioo chake ni cha oled
Ila hii Sony Xperia 1 III inapata mwisho toleo la Android 13
Sony Xperia XZ3
Bei ya Sony Xperia XZ3 ni shilingi laki mbili na nusu (250,000)
Ni simu ya kitambo sana tangu mwaka 2018, yaani ina miaka saba (7) tangu itoke
Na kwa bahati mbaya haipokei sapoti yoyote toka kwa sony
Ila sasa ni simu yenye kioo cha Oled na utendaji wa wastani
Ni simu yenye kamera moja yenye uwezo wa kurekodi video za 4K kwa kiwango cha fremu 30fps
Betri yake sio kubwa ina mAh 3300
Hitimisho
Sifa za sony zilizoorodheshwa zinazifanya kuwa simu shindani hata kwa wakati uliopo
Ukitazama simu zinazouzwa chini ya laki tano zina sifa chache sana nzuri ukilinganisha na hizi sony
Kwa kuwa ni simu za zamani kuna uwezekano ukaipata ikawa ina baadhi ya changamoto hasa za betri
Kikubwa ni kuwa makini wakati ukinunua popote pale duniani