SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora wa simu mpya za 5G Samsung Galaxy A26 na A36

Simu Mpya

Sihaba Mikole

April 19, 2025

Mpaka kufikia 2025, kampuni za simujanja zimetoa matoleo mengi ya daraja la kati

Wanaotaka kununua simu za daraja la kati wana machaguo mengi ya kuchagua

Moja ya simu mpya za madaraja hayo ni Samsung Galaxy A26 na Samsung Galaxy A36

Ni simu zilizotoka mwezi machi 2025 na bei zake ni 650,000 na 850,000

Hapa, kwa ufupi, tutaangalia ubora katika vipengele vya

  • Kamera
  • Software
  • Ukaaji wa chaji
  • Utendaji

Samsung Galaxy A26

Simu inakuja katika matoleo manne ikiwa na mgawanyiko wa ukubwa GB 128 na GB 256

Upande wa RAM unaweza kuta ya GB 6, 4 AU 8

samsung galaxy a26

Urefu na upana ni inchi 6.7 na simu ya 5G

Software

Samsung Galaxy A26 inatumia mfumo endeshi wa Android 15 na One UI 7

Itakuwa inapokea matoleo mapya ya Android kwa kipindi cha miaka 6

Ni mageuzi makubwa maana zamani Samsung walikuwa wanatoa update miaka michache

Hivyo mfumo endeshi mpya unampa nafasi mtumiaji kupata vitu vipya

Na kuipa simu thamani muda mrefu hata pale utakapotaka kuuza

Kamera

Simu ina kamera tatu ambazo ni aina ya wide, ultrawide na macro

Kamera kubwa ina megapixel 50 ikiwa na OIS

Inaweza kurekodi video za 4K ambazo huwa na mng’ao mkubwa wa picha

Ila kamera ya mbele ukubwa wake ni megapixel 13 tu

Na inaweza kurekodi video za full hd pekee

Ukaaji wa chaji

Betri ya Samsung Galaxy A26 ina ukubwa wa mAh 5000

Na katika matumizi ya kawaida simu inaweza kukaa na chaji kwa msaaa karibu 11

Kwenye uchezaji magemu mara kwa mara inaweza kustahimili kukaa na chaji masaa karibu nane

Kwa maana hiyo wastani wa ukaaji wa chaji sio mbaya

Utendaji

Nguvu ya utendaji ni ya wastani na inaweza kufanya mambo pasipo tatizo

Hii inatokana simu kutumia processor ya Exynos 1380

Ambapo core yenye nguvu sana zimeundwa kwa muundo wa Cortex A78

Na zipo core mbili kwa ajili ya kazi zinazohitaji nguvu kubwa

Samsung Galaxy A36

Samsung Galaxy A36 inakuja na ukubwa wa GB 128 au GB 256

Na upande wa RAM zipo za matoleo ya GB 6, 8 na 12

Kwa picha ya haraka Galaxy A36 ubora wake uko mbele ya Galaxy A26

samsung galaxy a36

Software

Inatumia Android 15 na itapata maboresho ya Android mpya kwa miaka sita(6)

Yaani utapata hadi Android 21

Kwa maana kwa changamoto zitakazohusiana na mfumo endeshi, simu itapata marekebisho

Kamera

Upande wa kamera, kuna kamera tatu za wide, ultrawide na macro

Hapa hakuna tofauti na Samsung Galaxy A26

Na pia inarekodi video za 4K kwa kiwango cha 30fps

Na kamera ya mbele ya self ina megapixel 12 inayoweza kurekodi video za full hd pekee

Ukaaji wa chaji

Katika matumizi ya kawaida BETRI yake ya ukubwa wa 5000mAh inaweza kukaa na chaji mpaka masaa 12

Kwenye kucheza gemu simu inachukua masaa saba mapaka chaji kuisha ukiwa unarekodi muda wote

Na inasapoti chaji ya wati mpaka 25

Hivyo kuwahi kujaa kwa muda mfupi ni swala la kawaida

Utendaji

Hii simu inatumia processor ya Snapdragon 6 Gen 3

Kimuundo inaendana na Exynos 1380 maana zote zinatumia muundo wa Cortex A78

Lakini utendaji wa Snapdragon ni mkubwa kwa kiasi fulani

Na hivyo inaweza kufanya vitu na kwa matumizi ya umeme kidogo

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company