SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Xiaomi(Redmi) 2025 na bei zake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

March 1, 2025

Hii ni orodha ya simu mpya za redmi na Xiaomi ambazo zimetoka mwanzoni mwa 2025 na mwishoni mwa 2024

Simu zilizoorodheshwa zipo za bei kubwa na bei ndogo

Hivyo basi utafahamu bei zake na sifa pamoja na ubora mkubwa kwenye kila simu iliyopo

Utaona simu ya Xiaomi iliyopo kwenye ligi moja na iPhone na Samsung

Tuzione sasa.

Xiaomi Redmi Note 14 Pro+ 5G

Bei ya Xiaomi Redmi Note 14 Pro+ 5G ni shiling milioni 1.1 ya ukubwa wa GB 256 na RAM GB 8

Utendaji wake unaweza kuhimili kucheza magemu tofauti bila shida

1-redminote14proplus

Kwani inatumia processor ya Snapdragon 7s Gen yenye ufanisi wa matumizi mazuri ya umeme

Ni simu yenye kamera tatu na kamera kubwa ina 200MP

Betri yake ina ukubwa wa 5110mAh na nguvu ya kuchaji ni kubwa ambayo ni 120W

Xiaomi Redmi Note 14 Pro 4G

Bei ya Xiaomi Redmi Note 14 Pro ni shilingi laki saba (700,000) ya ukubwa wa GB 256 na RAM GB 8

Na hii pia ina kamera tatu kubwa ikiwa na megapixel 200

redminote14pro4g

Inakuja na mfumo endeshi wa Android 14 na haitopata toleo lingine

Betri yake ni kubwa sana ambayo ni 5500mAh ila chaji yake kasi ni 45mAh

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu inatumia processor Mediatek Helio G100 Ultra

Xiaomi Redmi Note 14 5G

Bei ya Redmi Note 14 5G ya GB 256 na RAM GB 8 ni shilingi laki saba

Boresho kubwa kwenye hii simu ni uwepo wa mtandao wa 5G

Kwenye kamera yapo yaliyopunguzwa, kamera kubwa ina 108MP

3-redminote145g

Hii simu itapokea matoleo mapya ya android kwa miaka miwili

Betri yake ina ukubwa wa 5110mAh na chaji inapeleka kasi ya wati 45

Xiaomi Remi Note 14 4G

Bei ya Redmi Note 14 4G ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 6 ni shilingi laki tano (500,000)

Haina utendaji mkubwa ila utendaji wake ni wa wastani

Inatumia chip ya mediatek helio G99 Ultra

redminote144g

Mfumo wake wa kamera ni wakawaida hauna vitu vingi ila kamera kubwa ina 108MP

Hii simu inakuja na Android 14 na itapata matoleo mengine mara nne

Xiaomi Redmi 14C 5G

Bei ya Xiaomi Redmi 14C 5G ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 4 ni laki tatu na elfu hamsini (350,000)

Ni simu ya daraja la chini ila utendaji wake ni mzuri ukilinganisha na bei

Kwani inatumia processor ya Snapdragon 4 Gen 2

redmi14c5g

Simu itapokea matoleo mapya mawili ya Android

Upande wa kamera kuna kamera moja tu yenye megapixel 50

Betri yake ina mAh 5160 na spidi ya chaji ni wati 18(sio kubwa)

Xiaomi 15 Ultra

Xiaomi 15 Ultra bei yake ni shilingi milioni mbili na kaki tano (2,500,000)

Hii ndio simu yenye ufunano na matoleo ya iphone 16 ama Samsung Galaxy S25

Ina jumla ya kamera nne na kamera kubwa ina megapixel 200 huku zingine zikiwa na megapixel 50

xiaomi15ultra

Betri yake ni kubwa na ina mAh 6000 na chaji ya kasi ya 90W

Ina nguvu kubwa ya kiutendaji kwa sababu ina processor ya Snapdragon 8 Elite

Simu inakuja na Android 15 na itapata matoleo mapya ya android mara nne tu.

Xiaomi Poco X7 Pro

Bei ya Xiaomi Poco X7 Pro ni milioni moja na laki moja yenye GB 256 na RAM ya GB 8

Ina kamera mbili tu huku kamera kubwa ikiwa na 50MP

Inatumia processor ya Dimensity 8400 Ultra hivyo utendaji wake ni mzuri

pocox7pro

Inakuja na mfumo endeshi wa Android 15 na hakuna taarifa kama itapata toleo jipya

Betri yake ni kubwa (mah 6000) na chaji yake inasapoti wati 90

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsungs25thumb

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na sifa zake muhimu

Hii ni post inayoenda kukuonyesha kinaga ubaga juu ya ubora mkubwa wa simu mpya ya Samsung Galaxy S25 Ultra Samsung Galaxy S25 Ultra imeingia rasmi sokoni mnamo mwezi februari 2025 […]

samsungfoldspecial

Simu mpya za Samsung 2025 na bei zake

Mwezi wa Januari kampuni ya Samsung ilitangaza ujio wa matoleo matatu mapya ya Samsung Galaxy S25 Matoleo ya Samsung Galaxy S25 ni ya daraja la juu hivyo  ubora na bei […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

huawei mate

Simu Bora 15 Duniani 2024 (na zitakazotamba 2025)

Kwa mwaka 2024, soko la simu janja yaani smartphone duniani lilitawaliwa na makampuni ya Apple, Samsung, Xiaomi, Vivo na Oppo Kwa hapa Afrika kampuni ya Samsung inaongoza kwa mauzo ikifuatiwa […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company