SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na sifa zake muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

February 23, 2025

Hii ni post inayoenda kukuonyesha kinaga ubaga juu ya ubora mkubwa wa simu mpya ya Samsung Galaxy S25 Ultra

Samsung Galaxy S25 Ultra imeingia rasmi sokoni mnamo mwezi februari 2025

Ni simu ya daraja la juu ambayo inaambatana na sifa kubwa katika kila kipengele

Kabla ya kuitazama kiundani ni vizuri ukaifahamu bei yake

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra GB 256

Kwa Tanzania bei yake ni shilingi milioni 3.5 (yaani milioni tatu na nusu)

samsungs25ultra

Wakati ukiinunua utakuta hakuna chaji

Kwa maana kama hauna chaji itakulazimu ununue nyingine

Bei yake haipo sawa kwa zile zenye memori kubwa yaani GB 512 na 1TB

Hivyo bajeti yako itategemea na kiasi cha memori unachohitaji

Sifa za Samsung Galaxy S25 Ultra

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 8 Elite 
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×4.47 GHz Oryon V2 Phoenix L
  • Core Za kawaida(6) – 6×3.53 GHz Oryon V2 Phoenix M
  • GPU-Adreno 830
Display(Kioo) Dynamic LTPO AMOLED 2X, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 15
  • One UI 7
Memori UFS 4, 256GB,512GB,1TB na RAM 12GB,16GB
Kamera Kamera nne

  1. 200MP,multi-directional PDAF(wide)
  2. 10MP(telephoto)
  3. 50MP(periscope telephoto)
  4. 50MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.9inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 3,500,000/=

Uwezo wa network

Samsung Galaxy S25 Ultra inasapoti aina zote za network

Upande wa 5G inaweza kutumika hata ile inayotumia mmWave ambayo huwa na kazi zaidi

Kwenye 4G inakuja na LTE Cat 24

LTE Cat 24 inasapoti spidi ya kudownload hadi 10000Mbps na kuupload hadi 3500Mbps

Spidi ni kama mtandao wa simu una miundombinu na mazingira inayosapoti kasi ya aina hii

Pia Galaxy S24 Ultra inasapoti mtandao wa eSIM

Kwa maana hautokuwa na ulazima wa kununua laini za plastiki

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy S25 Ultra

Kioo cha hii simu kina kina kikubwa cha rangi

Kwani ni cha Dynamic LTPO Amoled kikiambatana na teknolojia ya HDR10+

HDR10+ ndio inayohusika kuongeza kina cha rangi kwenye kioo

Hivyo vitu vinaonekana kwa uangavu mzuri na rangi sahihi kwa kiwango kikubwa

Refresh rate yake inafika 120Hz kitu kinachofanya skrini kuwa fasata na murua unapotachi

Kioo cha Dynamic LPTO kinadhibiti matumizi ya refresh rate kubwa pale ambazpo haihitajiki

Kwani refresh rate kubwa ikiwa inatumika muda wote chaji ya betri hupungua

Nguvu ya processor Snapdragon 8 Elite

Kwa sasa Snapdragon 8 Elite inaongoza kuwa na nguvu kubwa kiutendaji kuliko processor zingine za simu

Pia ina ufanisi madhubuti wa matumizi madogo ya umeme hata kwa kazi kubwa

Ndio maana Samsung Galaxy S25 Ultra inakaa na chaji muda mrefu hata ukiwa unacheza gemu muda wote

Kwa vipimo vya app ya Geekbench, Snapdragon 8 Elite inaweza kufungua kurasa 229 kwa sekunde bila kukwama kwama

Na ina alama 3155 kwenye core moja yenye nguvu

Kumbuka hii processor ina core nane na core mbili hutumika kwa ajili ya kufanya kazi zinazohitaji nguvu kubwa

Uwezo wa betri na chaji

Ukubwa wa betri ya Galaxy S25 Ultra ni 5000mAh

Na simu inaweza kukaa na chaji kwa siku nzima katika matumizi ya kawaida

Ukiwa unacheza gemu wakati wote betri inadumu kwa masaa 11

Ni masaa mengi kwa sababu simu nyingi zilizopo sokoni hudumu kwa muda wa masaa 7

Inakubali chaji inayopeleka umeme mwingi hadi wati 45

Na pia inaweza kuchajiwa kwa njia ya wireless(bila kutumia waya)

Sema njia hii inapeleka umeme kidogo wa wati 15 tu

Hata hiyo simu haiji na chaji bali wewe ndio utalazimika kutumia ya zamani au kununua

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy S25 Ultra

Kama unataka simu yenye waterproof ya kuzuia maji hata kwa kina kirefu Samsung toleo jipya inahusika

Ina waterproof aina ya IP68 inayoweza kuzuia maji yasiingie kwenye simu hata ikizama kwenye kina cha mita 1,5 kwa nusu saa

Ina bodi ya titanium ambayo huwa ni imara na ngumu

Na inatumia vioo vya Corning Gorilla Armor 2

Hata hivyo umakini ni muhimu kwa sababu kioo ni kioo tu huvunjika

Ubora wa kamera

Katika kamera nne ilizo nazo zote zinatoa picha nzuri

Na zenye utofautishaji mkubwa wa rangi

Dynamic range ya simu ni kubwa hata kwa wakati wa mchana kamera inahimiri mwanga mwingi na kutoa picha kwa rangi zake

Hata ukiikuza picha baada ya kupiga vitu vinaonekana kwa uzuri

Nyakati za usiku picha zinatokea vizuri japo kama giza ni kubwa kwa kiwango cha noise kinaweza kuonekana

Upande wa video kamera yake inaweza kurekodi video hadi za 8K na 4K kwa kiwango cha 120fps

Ubora wa Software

Kwa sasa ubora mkubwa wa software unaoneshwa zaidi kwenye matumizi ya AI

Kabla, hii simu inakuja na Android 15 na itakuwa inapokea toleo jipya la android kwa miaka 7 mfulululizo

Yaani itapata hadi android 22

Kwenye AI simu inasapoti kitu kinaitwa natural language understanding hata kwenye settings

Kwa mfano mwanga wa kioo ni mkubwa na hujui settings za kupunguza mwanga

Kwenye setting unaweza kuiambia simu kwamba macho yangu yanauma kwa sababu ya mwanga

Basi muda si mrefu itakuletea page ya kupunguza mwanga yenyewe, yaani imeelewa unachotaka kufanya

Pia katika picha unaweza kuongeza ama kuondoa kitu na picha ikaonekana halisi

Yaani kwenye Galaxy AI kuna mengi sana ya Artificial Intelligence

Washindani wa Samsung Galaxy S25 Ultra

Kwa upande wa apple kuna toleo jipya la iPhone 16e

iPhone 16e hata hivyo ni toleo dogo haliwezi kuwa mshindani sahihi

Mshindani sahihi ni iPhone 16 Pro Max, Xiaomi 15 Pro, OnePlus Ace 5 Pro na hata Samsung Galaxy S24 Ultra

Simu tajwa upande wa hardware zinaendana kisifa katika maeneo mengi

Kwa mfano simu za Xiaomi 15 Pro na OnePlus Ace 5 Pro zinatumia processor iliyotumika kwenye Samsung Galaxy S25 Ultra

Hii inamaanisha hizo simu hazina tofauti kubwa kiutendaji

Na mbaya zaidi simu za China huuzwa kwa bei ya chini zaidi

Uwepo wa simu za China sokoni kumeiondoa Samsung katika nafasi ya kampuni zinazoongoza kimauzo

Neno la mwisho

Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na ubora wake himilivu kwa watu wenye bajeti kubwa

Uimara na matumizi makubwa ya AI na sapoti ya software kwa muda mrefu unaipa simu thamani kubwa

Kwa mtumiaji hatolazimika kubadilisha simu mara kwa mara kupata vitu vipya maana simu inajitosheleza

Na itakuwa inapokea vitu vipya kwa muda mrefu

Ila bei yake pia inaweza ikawa ni changamoto pale itakapokutana na simu za China

Makampuni kama Xiaomi, Vivo, Oppo, Huawei na mengineyo hayapo nyuma katika utowaji wa simu kali

Ila kitendo cha kutoa update za software kwa muda mrefu kimeiweka toleo jipya la samsung katika nafasi nzuri

Maoni 2 kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy S25 Ultra na sifa zake muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi15ultra

Simu mpya za Xiaomi(Redmi) 2025 na bei zake

Hii ni orodha ya simu mpya za redmi na Xiaomi ambazo zimetoka mwanzoni mwa 2025 na mwishoni mwa 2024 Simu zilizoorodheshwa zipo za bei kubwa na bei ndogo Hivyo basi […]

samsungfoldspecial

Simu mpya za Samsung 2025 na bei zake

Mwezi wa Januari kampuni ya Samsung ilitangaza ujio wa matoleo matatu mapya ya Samsung Galaxy S25 Matoleo ya Samsung Galaxy S25 ni ya daraja la juu hivyo  ubora na bei […]

iphone 16 pro

Kampuni bora za Simu duniani (2024/2025)

Pamoja na uwepo wa makampuni zaidi ya 100 ya kutengeneza simu bado kampuni zilezile zimeendelea kushika soko kwa sehemu kubwa duniani, kampuni hizo ni apple, samsung na xiaomi na nyinginezo. […]

huawei mate

Simu Bora 15 Duniani 2024 (na zitakazotamba 2025)

Kwa mwaka 2024, soko la simu janja yaani smartphone duniani lilitawaliwa na makampuni ya Apple, Samsung, Xiaomi, Vivo na Oppo Kwa hapa Afrika kampuni ya Samsung inaongoza kwa mauzo ikifuatiwa […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company