SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Spark 30C na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

October 6, 2024

Tecno wameleta toleo jipya la simu ya madaraja ya chini yenye maboresho

Ina maboresho upande wa skrini(kioo) kuwa na refresh rate kubwa ambayo mara hupatikana kwenye simu za daraja la kati kwenda mbele

Pamoja na maboresho hayo, bado bei ya Tecno Spark 30C ni ndogo na ambayo wengi wanaweza kiumudu

Kwani bei yake rasmi kwa Tanzania ni shilingi laki mbili na elfu tisini (290,000)

Hii ikiwa na ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 4.

Tuzame kiundani zaidi ulewe ubora na changamoto za Tecno Spark 30C ili ufanye uamuzi sahihi

Sifa za Tecno Spark 30C

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G81
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0GHz Cortex A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz Cortex A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
Memori 256GB,128GB, na RAM 6GB,4GB
Kamera Kamera MOJA

  1. 50MP,PDAF(wide)
Muundo Urefu-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 290,000/=

Uwezo wa network

Tecno Spark 30C ni simu ya 4G inayosapoti laini mbili

Haishangazi kutokana na aina ya bei na aina ya wateja inayolenga

Kwa maana ukiwa na hii simu hautoweza kutumia 5G hata kama upo kwenye eneo linalosapoti 5G

Kwa bahati au nzuri 5G imeenea maeneo machache sana hapa Tanzania

Kwani hata wamiliki wa simu zenye 5G mara nyingi kama si mara zote hutumia mtandao wa 4G

Hata mambo yanaweza mabadilika kadri muda utakavyokuwa unasogea

Ubora wa kioo cha Tecno Spark 30C

Kioo cha hii simu kina refresh rate inayofika 120Hz

Lakini kioo kina resolution ya kawaida ambayo sio full hd

Refresh rate kubwa hufanya kioo kuwa chepesi na muonekano mzuri pale unapokuwa unaskrol ama kucheza gemu

Ila changamoto kubwa ya refresh rate kubwa ni kutumia umeme mwingi

Ni vizuri ukatambua sio nyakati zote utahitaji kutumia refresh rate kubwa

Ni vizuri ukaizima kama una matumizi ya kawaida

Nguvu ya processor Mediatek Helio G81

Nguvu ya processor sio kubwa kivile japo inakuwezesha kucheza baadhi ya gemu kama PUBG Mobile

Ila gemu kama Call of duty au assassin creed itakulazimu kupunguza ubora wa graphics vinginevyo simu inaweza kukwama kwama

Hii inasababishwa na processor ya mediatek helio g81 kuundwa na muundo wa Cortex A75 kwenye core zenye nguvu kubwa

Hata kwenye inayopima nguvu za processor za simu helio g81 ina alama kama 400 hivi

Ambapo ni ndogo

Lakini kumbuka simu inamlenga mtumiaji mwenye matumizi ya kawaida

Hivyo inakuwa haina haja ya kuweka teknolojia kubwa sana kwenye simu kwani itaongeza gharama na simu kuwa na bei kubwa

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya inapeleka umeme wa wati 18

Ni kasi ya wastani na simu inaweza kuchukua muda kidogo kujaa

Kikawaida cha wati 33 hujaza betri kwa muda wa dakika 80 yaani lisaa limoja na dakika ishiri

Wati 18 inaweza chukua hata masaa matatu kujaza betri kubwa ya mAh 5000

Kwa mtumiaji wa hii simu atanufaika pia na ukaaji wa chaji

Kwa sababu processor iliyopo imeboreshwa pia kwenye matumizi ya chaji

Kiwastani ukiwa kwenye intaneti muda wote simu inadumu na chaji kwa masaa karibu 12

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo ya aina mbili upande wa ukubwa wa memori

Unaweza ukapata ya GB 128 na GB 256

Na zote zimagawanyika katika matoleo ya aina mbili upande wa RAM

Unaweza ukapata mojawapo yenye RAM ya GB 4 ama GB 6

Kama ukiweza kuongezea pesa, chukua yenye RAM ya GB 6

RAM kubwa inakupa upana kufungua mafaili mengi kwa wakati mmoja bila kufanya simu kuwa nzito

Uimara wa bodi ya Tecno Spark 30C

Bodi yote ya Tecno Spark 30C ni ya plastiki

Tofauti ni simu za gharama kubwa ambazo zinaweka bodi za titanium

Katika mazingira yenye maji ya kunyunyulizika, maji hayatoingia ndani ya simu kama utakuwa umejisahau

Ila simu ukiizamisha kwenye kina kikubwa cha maji mengi basi itaharibika

Kwenye skrini simu haiji na protekta

Ni muhimu ukanunua protekta kuepuka na changamoto ya simu kupasuka

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera moja inayokuja na ukubwa wa megapixel 50

Kwa nyuma muonekano wake unashawishi kusema kuna kamera tatu ila hapana ni kamera moja

Ubora wa picha hasa kwenye mwanga simu inajitahidi kupiga picha nzuri

Japo baadhi ya vitu vina uzidisho wa rangi

Kiasi cha kwamba ule muonekano wa asili unaweza potea

Simu inaweza kurekodi video za full hd na haiwezi kurekodi video za resolution kubwa zaidi

Ubora wa Software

Tecno Spark 30C inakuja na mfumo endeshi wa Android 14 na HIOS 14

Muda si mrefu Android 15 itatoka

Lakini hakuna taarifa kama spark 30c itapokea android mpya

Tukiachana na hilo, matumizi ya AI kwa sasa ndio jambo kubwa kwa matoleo mengi ya simu

HIOS 14 inakupa AI ya chatgpt ambayo utaweza kupata taarifa na majibu kwa kuiuliza maswali mbalimbali

Hivyo hutokuwa na haja ya kuidownload au kwenda kufungua chatgpt

Washindani wa Tecno Spark 30C

Simu mbadala zinazoshindana na tecno zipo nyingi

Ila chache zinazoweza leta ushindani mkubwa sana kwa hapa Tanzania ni Samsung Galaxy A06 na Redmi 14C na hata itel S24

Simu tajwa hapo juu zinaendana sana kisifa na mambo mengine

Sema kuna vitu vidogo simu zinazidiana

Kwa mfano itel s24 kamera yake ina megapixel 108 na utendaji wake mkubwa kidogo

Na bei ya itel s24 inaendana kwa sehemu kubwa na tecno

Neno la Mwisho

Kwa watu wenye bajeti ndogo za kununua simu sasa hivi wanapata ya kutumia kioo chenye refresh rate kubwa

Si hivyo na hata ubora wa kamera umeboreshwa kwa kiasi fulani

Kwa hiyo baadhi ya mambo yaliyokuwa yanapatikana kwenye simu za gharama utaweza kupata kwenye tecno spark 30c japo kwa uchache sana

Hivyo bei ya tecno spark 30c imeitendea haki sifa zinazoambatana na hii simu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A06 na Ubora wake

Samsung Galaxy A06 ina betri inayokaa na chaji muda mrefu na ni simu ya daraja la chini Hii inamaanisha watu wengi kwa hapa Tanzania wanaweza inunua Kwa sababu bei ya […]

display

[VIDEO]: Simu za tecno zenye kamera nzuri zaidi

Tazama ubora wa picha zilizopigwa na simu za Tecno Camon 30, Camon 30 Premier, camon 20 premier na nyininezo

thumbnail

[VIDEO]:Simu zote za iPhone za bei ndogo na zinazofaa

Kabla ya kununua iphone za bei rahisi ambazo mara nyingi huwa ni used, kitu cha kwanza cha kuangalia ni kama itakuwa inapata sapoti ya kupokea mfumo endeshi wa iOS Tofauti […]

tecno camon premier 30

Ubora wa simu za Tecno Camon 30 na bei zake(Pro, Premier)

Tangu mwezi wa nne kampuni ya walitoa matoleo ya Tecno Camon 30 Matoleo ya Camon 30 yapo matatu ambayo ni ya daraja la kati yaani mid range Ubora wa kiujumla […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company