SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za iPhone na Bei zake 2024 (matoleo ya iphone 16)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

September 15, 2024

Kila mwezi wa tisa kampuni ya Apple ya Marekani hutangaza simu mpya za iphone

Katika uzinduzi apple huanisha vitu vipya simu zinazokuja nazo na bei zake kwa kila toleo

Kwa mwaka 2024 apple wamezindua simu za iphone 16, simu hizo ni

  • Apple iPhone 16
  • Apple iPhone 16 Plus
  • Apple iPhone 16 Pro
  • Apple iPhone 16 Pro Max

Kwenye hizi iphone mpya zimekuja na mabadiliko madogo sana

iphone 16 series

Kiasi cha kwamba kwa mtumiaji wa kawaida wa iPhone 15 Pro anaweza asione haja ya kununua iPhone 16

Sababu kubwa hakuna tofauti ya kimuundo na wala hata vipya vya kusisimua

Hata yapo mambo mapya kwenye hizi simu

Vitu vipya vinavyopatikana

Kwanza simu zote zinatumia processor mpya kabisa

Processor hizo ni Apple A18 na Apple A18 Pro

Apple A18 na Apple A18 Pro zinatarjiwa kuwa na nguvu na ufanisi mzuri wa matumizi ya betri

chip

Hii inamaanisha nini?

Simu matoleo ya iPhone 16 zinatarajiwa kukaa na chaji muda mrefu

Katika uzinduzi, apple walianisha kuwa chip mpya zitakuwa na uimara wa kiutendaji na ufanisi wa betri kwa zaidi ya 30% ukilinganisha na toleo lilopita

Kitu kikubwa ambacho kinaonekana kipya sana ni uwepo wa akili mnemba(Artificial Intellignece-AI)

Apple wanaibrand kama Apple Intelligence pamoja na uwepo wa ChatGPT

apple intelligence'

Moja ya vitu utakavyoweza kufanya ni kuondoa kitu ambacho hukitaki kilichotokea kwenye picha

Hiki sio kitu kigeni kwenye simu za Android

Tayari zipo kwenye simu za Google Pixel, Samsung, Infinix, Oppo na nyinginezo

Pia kuna ongezeko la batani mbili zinaoitwa action button na camera control button

Action button inakusaidia kufungu baadhi ya app kama shazam, app za kutafsiri lugha nk

Camera control kama neno linavyoonesha inaweza kuzoom kamera, kubadilisha aina ya lensi, kurekodi video na mengineyo

Na uwezo wa kurekodi video za 4K kwa kiwango cha fremu 120fps

Sasa tuangalie kwa ufupi simu moja baada ya nyingine

Apple iPhone 16

Apple iPhone 16 kimo chake ni inchi 6.1

Ndio iphone 16 yenye kimo kidogo zaidi inafaa kwa wanaopenda simu portable

Ina matoleo ya GB 128, 256 na 512 huku ukubwa wa RAM ni GB 8

iphone 16

Simu ina kamera mbili zenye lenzi za wide na ultrawide na zinaweza kurekodi video za 4K kwa kiwango cha 120fps

Inatumia chip ya Apple A18

Na bei yake iliyotangazwa ni shilingi milioni 2.3 za kitanzania

Apple iPhone 16 Plus

Apple iPhone 16 Plus haina tofauti na iPhone 16

Sifa zao zinafanana na zinatofauitiana katika eneo moja tu

iphone 16 plus

Eneo hilo ni kimo, iPhone 16 Plus ni ndefu sana kuliko mwenzie

Urefu wa iPhone 16 Plus ni inchi 6.7

Apple iPhone 16 Pro

Apple iPhone 16 Pro inakuja katika matoleo manne kwenye ukubwa wa memori

Kuna ya GB 128, 256, 512 NA TB 1 yaani GB 1020

Urefu wa iPhone 16 Pro ni inchi 6.3

iphone 16 pro

Na kiutendaji ina nguvu sana kwa sababu inatumia chip ya Apple A18 Pro

Bei ya  kuanzia ya hii simu ni shilingi milioni 2.9

Apple iPhone 16 Pro Max

Apple iPhone 16 Pro haina tofauti kisifa na iPhone 16 Pro

Tofauti yao kubwa ni urefu

iPhone 16 Pro Max ina kimo cha inchi 6.9

iphone 16 pro

Hii ndio iphone ndefu zaidi kuwahi kutokea

Bei ya iPhone 16 Pro Max ni shilingi milioni 3.5

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail

[VIDEO]:Simu zote za iPhone za bei ndogo na zinazofaa

Kabla ya kununua iphone za bei rahisi ambazo mara nyingi huwa ni used, kitu cha kwanza cha kuangalia ni kama itakuwa inapata sapoti ya kupokea mfumo endeshi wa iOS Tofauti […]

iphone thumbnail

iPhone za bei rahisi za kumiliki kwa sasa(2024-2027)

Katika pitapita zangu na kuchunguza simu bora za bei ndogo na ya chini nimekuja kugundua kitu cha kustahajabisha kidogo Wapenzi wa iPhone wenye bajeti ndogo wananunua iphone used hazipokei maboresho […]

Simu bora duniani na bei zake 2024

Leo tuzungumzie kuhusu simu bora duniani na bei zake kwa mwaka 2024 Kuna matoleo mapya ya simu kali yenye ubora wa kiutendaji na wenye nguvu madhubuti katika maeneo mengi Ubora […]

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company