SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Miongozo

Sihaba Mikole

July 21, 2023

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi

Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano na origino

Kiasi cha kwamba inakuwa ni ngumu kujua simu origino ni zipi na zipi ni feki

Kwa kifupi ni kuwa, simu origino ni zile simu zinafanana kwa 100% na sifa zilizoainishwa na mzalishaji halisi wa simu husika

Ukiona baadhi ya sifa hazifanani hata kama ni moja basi jua simu unayotakaka kununua sio orijino

Mara nyingi wahanga simu feki ni iPhone na Samsung za bei kubwa,

Swali ni kuwa unatumbuaje na kutofautisha simu feki na orijino.

Fanya yafuatayo kabla ya kununua.

Chunguza Muundo wa bodi ya simu

Kitu cha kwanza kabla ya kununua simu tazama video na fuatilia makala mbalimbali zinazofafanua sifa za simu unayotaka kununua

Tovuti ya simunzuri.com ni sehemu moja wapo kuzijua sifa za simu janja

Kwa maana angalia kwa umakini muundo wa skrini, aina ya bodi na pia muundo wa kamera nyuma na mbele

Watengenezaji wa simu feki hupata shida kunakiri kwa usahihi muundo wa simu orijino

Kwa mfano hii picha ya chini ni muonekano wa samsung galaxy s22 ultra origino na ile ambayo ile sio orijino

Samsung orijino kioo chake kimepinda kwenda wakati hii feki kioo kipo flat na upande wa juu hakijapinda kwenda

Waliotengeneza samsung s22 wamekutana na ugumu wa kupata kioo chenye muundo huu

Hivyo kwa macho unaweza kuitambua simu ambayo ni orijino ila lazima uifuatilie simu kiundani hasa kwa kutazama video na picha kabla ya kununua ndio utaweza kuzifananisha kama zinaendana.

Fuatilia aina ya Processor ya simu

Simu feki huwa hazitumii processor(cpu) zilizopo kwenye simu orijino

Mara nyingi cpu za kwenye simu orijino huwa zina gharama kubwa kitu kinachowapa ugumu kuziweka

Tuchukulie mfano wa simu ya iPhone 13 Pro Max

Processor yake inaitwa Apple A15 Bionic kama umefuatilia sifa zake hii ni moja ya taarifa inayowekwa

Simu ambayo ni feki haiwezi kutumia kutumia hii chip

Ukidownload app zinazocheki vitu vilivyopo kwenye simu utaona vitu vipo tofauti na sifa za simu husika

Hii ni picha ya iphone 13 pro max ambayo ni feki,

iphone feki 2

Kwenye upande wa CPU app inaonyesha Mediatek Qualcomm Snapdragon 888 plus kitu ambacho hakipo na ni tofauti na cpu ya iphone 13

Hapo ilipaswa isome Apple A15 Bionic

App ya CPU-Z inaweza ikakujulisha taarifa za simu lakini sio ya uhakika kwa sababu haina uwezo wa kujua kama taarifa inazozitoa simu ni feki

Kwenye hii simu CPU-Z inaonyesha memori ya simu feki kuwa ni GB 250 na RAM ya GB 8

Ila baada ya kutazamwa kiundani kwa kutumia kompyuta kwa software ya Android Studio, simu ilionekana kuwa na GB 8 na RAM ya GB 1

App nzuri kwa kiasi fulani ni kingroot na CPU X kwa ajili ya kucheki taarifa za simu

Cheki mfumo Endeshi wa simu(Operating System)

Kwenye sifa za simu yoyote kitu cha kwanza kinachoainishwa ni aina ya mfumo unaotumiwa na simu husika

Taarifa hizi unaweza kuzipata kwenye tovuti rasmi ya kampuni inayounda simu au  mitandao kama gsmarena, simunzuri ni kwingineko

Kama kampuni inasema kuwa mfumo endeshi ni Android 13 na One UI 5, basi kwenye about phone inapaswa ionekane hivyo

Ila hapa umakini ni muhimu.

Kwa sababu kuna simu feki huwekewa theme zenye muonekano wa kama wa simu origino kiasi cha kwamba unaweza usitambue

Kwa kuwa una app kama CPU X au kingroot ni rahisi kutumbua kama sifa za simu zinaendana na simu orijino

Chunguza IMEI number

Kila kifaa cha mawasiliano huwa na imei namba yake ya kipekee inayotofautiana na nyingine

Kuna tovuti na app nyingi unazoweza kutumia kuangalia iwapo imei inaonyesha simu husika

Hata hivyo kutumia imei number sio njia nzuri kwa sababu kuna apps zinaweza kubadilisha

Kama ukibonyeza *#06# kuangalia imei itakuonyesha imei iliyobadirishwa

Lakini ni njia nzuri ya kuanzia

Kuna tovuti zinaweza kukusaidia kuonyesha imei, moja wapo ni imei check

imei check

Hii inakuruhusu kuingiza tarakimu 15 utakazozipata baada ya kupiga *#06#

Taarifa itakazorudisha zinapaswa ziendane na sifa za simu yako

Ikiwa ni tofauti jua kuwa hiyo sio simu origino

Kumbuka hii sio njia kwa sababu IMEI hubadirishwa

Hitimisho

Hizi ni njia chache za kuweza kujua simu origino ni zipi

Kuna njia nyingi zinazochimba kiundani

Unapoenda kununua simu fanya settings pale pale dukani na halafu download app ya CPU X au Kingroot

Kwenye CPU X bonyeza CPU utaona jina la cpu na aina za core zilizotumika

Kisha tafuta taarifa za simu yako kuhusu processor CPU ukiona tofauti fahamu kuwa ni feki na uirudishe kwa muuzaji

Maoni 3 kuhusu “Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 30C na Sifa Zake Muhimu

Tecno wameleta toleo jipya la simu ya madaraja ya chini yenye maboresho Ina maboresho upande wa skrini(kioo) kuwa na refresh rate kubwa ambayo mara hupatikana kwenye simu za daraja la […]

No Featured Image

Bei ya iPhone 16 Pro na Sifa zake Muhimu

Kampuni ya Apple imeingiza matoleo mapya ya iphone Moja ya iPhone hiyo ni iPhone 16 Pro, ina ufafanano kwa sehemu ya kimuundo na iPhone 15 Pro Yapo mazuri lakini yapo […]

iphone 16 pro

Simu mpya za iPhone na Bei zake 2024 (matoleo ya iphone 16)

Kila mwezi wa tisa kampuni ya Apple ya Marekani hutangaza simu mpya za iphone Katika uzinduzi apple huanisha vitu vipya simu zinazokuja nazo na bei zake kwa kila toleo Kwa […]

display

[VIDEO]: Simu za tecno zenye kamera nzuri zaidi

Tazama ubora wa picha zilizopigwa na simu za Tecno Camon 30, Camon 30 Premier, camon 20 premier na nyininezo

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company